Wale Mliowahi Kupanda Treni ya Tazara Tukutane Hapa

Wazambia wanapenda sana pombe! Kuhusu suala la kuku wa Kisaki ni sawa na wale kuku wa Salanda kwa reli ya kati. Unakutana na kuku mkubwa kama mwewe afu bei chee hadi mwenyewe unaweza tamaa inakuisha.
Kabisa mkuu,mimi nina uchu lakini nikifika kisaki uwa nafunga mdomo.Ila stimela ni usafiri poa sana.
 
Bila kupoteza muda, mliowahi kupanda Treni ya Tazara, Dar, Mbeya, Kapirimposhi. Ni kitu gani unakikumbuka katika safari zako ndani ya treni hiyo? Vipi yale mahandaki na kona za hatari?
Karibuni kwa mjadala...
Nakumba madaraja makubwa , treni ikiwa inapita kwenye mahandaki ,na good view hasa ukiwa buffet unafanya mambo yako
20181011_080245.jpeg
20181010_202143.jpeg
20181010_202218.jpeg
20181011_091226.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku niliona kwenye documentary moja tbc kuhusu ujenzi wa Reli hii, ambapo wachina takribani 300 walipoteza maisha, wabongo na wazambia 400. Hiyo ni kutokana na ujenzi huo kupita sehemu zenye wanyama wakali hivyo ikahatarisha maisha ya wajenzi.

Ni reli ambayo imegharimu maisha ya watu wengi sana.
Kwa hiyo katika hiyo vita ya ujenzi wa reli ya Tazara walikufa wajenzi wengi zaidi ya wale askari waliokufa kwenye vita halisi ya Kagera kati ya Tanzania na Uganda?
 
Bila kupoteza muda, mliowahi kupanda Treni ya Tazara, Dar, Mbeya, Kapirimposhi. Ni kitu gani unakikumbuka katika safari zako ndani ya treni hiyo? Vipi yale mahandaki na kona za hatari?
Karibuni kwa mjadala...
Umenikumbusha mbali sana nakumbuka tulikuwa tunatoka Mbeya kwenda dar kuna jamaa yangu alikunywa pombe aina ya amarula akaanza fujo na tulipofika makambako walimshusha askari wakampeleka kituoni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi nauli kwa wakati mwaka 2019 zikoje familia wanataka kusafiri kwenda mbeya mbalizi. Na wanataka za vitanda.
 
Nilijaribu safiri bure bana wee!, km tulivo zoea reli yetu ya kati, si mwenzenu huko mbele ya safari, nika kamatwa na wapambe -TT wanoko. sura zimewakomaa! hawaogopi mtu, basi!!! tukafungwa mashati!

Utasikia ''songa mbere!'' afande Mwita tuyaache vwawa kituoni haya? ..... sawa afande! japo hakuna maji pare! ........yatachota!

Bahati nzuri ktk kufungwa, nikawa the last victim's chain, shati langu halikukazwa sana, nikalifungua taatibu, huku tunasonga mbele, hivo nikawa km nawafuata tu kwa nyuma kidogo,

huku nawaza bila kujali matokeo nayoweza kumbana nayo, pindi tu wakigundua janja yangu!

Boss wao mdada tu, upper middle aged, kazuriii, akawa anajongea kuelekea tulipo, nilipo mtia machoni tu, jamani mjue jichooo!.
kiroho cha mahabati kikaripuka pwaa! ti i! tii! tii ! Whaaat!

bila kuchelewa nikatumia mbinu aliyo nielekeza Bibi yangu kitambo sana, pindi nikiwa katika hali km hii! kandamiza kona ya utosi ki aina na kidole kidogo'' huku nimemkazia macho! mtoto wa kike?

Wazi kabisa na yeye bila kujua nikamuambukiza ona kiroho pap! akasema ''yaani wewe kaka weweee! hee! njoo '' ki afande afande vile! si nikasimama naye palepale,

wale wakasonga mbele, Sasa basi kilichoendelea na afande huyu, tangia pale!????!!!!!!, ninasema
Sintokaa niisahau Tazara maisha yangu yote!
 
Oooh aise ilikuwa hatariii, yule dada Ni shida sanaaaa mwaka huo huo km sijakosea alipewa kipande Cha mlimba to mang'ula aise alikuwa anakimbiza hatariiiii...kufika mngeta 1km Kabla kufika stesheni ngoma ikahama Reli ikapasua katikati ikakata taluma nyingi Sana, vumbi likilotokea ilikuwa si mchezo behewa 2 za mwisho zikalala chini bahat nzuri Hakuna aliyekufa, dada yule noma sana
Huyo mdada Sasahivi anaendesha Treni la TAZARA to MWAKANGA
 
Bila kupoteza muda, mliowahi kupanda Treni ya Tazara, Dar, Mbeya, Kapirimposhi. Ni kitu gani unakikumbuka katika safari zako ndani ya treni hiyo? Vipi yale mahandaki na kona za hatari?
Karibuni kwa mjadala...
Umenikumbusha mbali kuna safari moja nilipanda treni, vituo kama 2 kabla ya kufika Mlimba kichwa cha tren kikataka kuwaka moto hivyo ikabidi wakitenganishe na mabehewa hivyo watu wote walishuka chini kwa mshtuko. Kusolve ikabidi waende kufuata kichwa kingine Mlimba basi tulikaa muda mrefu sana mpaka watu wakawa wameishiwa pesa, Sasa kuna watu walibeba zawadi za machungwa wakaanza kuuza Mia Mia mpaka muda yakafikia sh 700 nilishangaa sana maana kabla ya hiyo shida ata bure mtu anakupa.
 
Enzi zile Niko uboyizini mbeya huko

Nilikuwa navutiwa sana na watoto wa mlimba girls

Yaaani nipade "gogo" bila mlimba girls safari inakua ndefu saaana

Nilikuwa napenda pia kupamda like behewa la "super seat car" liko very comfortable kuliko kule third

Nimemiss sana enzi hizo

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom