MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Sina shida na Kipaji chake Kikubwa alichonacho ila Kiufundi kwa Kocha Mweledi na ambaye haingiliwi na Uongozi wa Timu hawezi Kumuanzisha Clatous Chama katika Mechi za Ushindani hasa.
Hii ni Mechi yangu ya Saba namtizama (namfuatilia) Clatous Chama na Kugundua kuwa ndiyo Mchezaji Kinara wa Kuharibu ( Kufifisha ) Mashambulizi ya Simba SC kwenda kwa Timu pinzani.
Leo tena amerudia Kosa lile lile kama alilolifanya dhidi ya Azam FC ambapo kuna nyakati Mchezaji mwenzake Kapombe au Dilunga alikuwa katika nafasi nzuri ya Kufunga ila kama Kawaida yake akaupooza mpira na Shambulizi Kufifia.
Yapo matukio yake mengi tu ila Kwangu Mimi itoshe tu kusema Clatous Chota Chama anatakiwa awe anaingia pale tu Timu ikiwa imeshashinda tayari ila siyo ikiwa inausaka (inatafuta) Ushindi kwani anatuchelewesha na atatuchelewesha mno katika Ushindi.
Na sishangai Kumsikia Mmoja wa Waandishi wa Habari za Michezo nchini Zambia na Mchambuzi Siku moja alipohojiwa na Mtangazaji wa Clouds FM alishangaa kusikia kuwa Chama huku Tanzania ni Mchezaji Mzuri na Mkubwa wakati kule Kwao nchini Zambia ni Kawaida mno ila akasema Mchezaji mwenye Kipaji cha hali ya Juu Zambia na hata Wachezaji wenzake wanamkubali ni Larry Bwalya.
Mlio karibu pia na Chama mrekebisheni.
Hii ni Mechi yangu ya Saba namtizama (namfuatilia) Clatous Chama na Kugundua kuwa ndiyo Mchezaji Kinara wa Kuharibu ( Kufifisha ) Mashambulizi ya Simba SC kwenda kwa Timu pinzani.
Leo tena amerudia Kosa lile lile kama alilolifanya dhidi ya Azam FC ambapo kuna nyakati Mchezaji mwenzake Kapombe au Dilunga alikuwa katika nafasi nzuri ya Kufunga ila kama Kawaida yake akaupooza mpira na Shambulizi Kufifia.
Yapo matukio yake mengi tu ila Kwangu Mimi itoshe tu kusema Clatous Chota Chama anatakiwa awe anaingia pale tu Timu ikiwa imeshashinda tayari ila siyo ikiwa inausaka (inatafuta) Ushindi kwani anatuchelewesha na atatuchelewesha mno katika Ushindi.
Na sishangai Kumsikia Mmoja wa Waandishi wa Habari za Michezo nchini Zambia na Mchambuzi Siku moja alipohojiwa na Mtangazaji wa Clouds FM alishangaa kusikia kuwa Chama huku Tanzania ni Mchezaji Mzuri na Mkubwa wakati kule Kwao nchini Zambia ni Kawaida mno ila akasema Mchezaji mwenye Kipaji cha hali ya Juu Zambia na hata Wachezaji wenzake wanamkubali ni Larry Bwalya.
Mlio karibu pia na Chama mrekebisheni.