Wale ambao wameshawahi kupita makaburini wakati wa usiku

BARDIZBAH

JF-Expert Member
Jan 11, 2017
4,772
8,429
Habar wana jamvi ?? Natumai tuko vzr tukiendelea kupambana na nchi yetu ambayo imesha kosa muelekeo . Anyway tusahau hayo nimeanzisha uzi ile nione wale wenzangu ambao wamesha wahi kupita makaburini endapo kama kuna njia mitaa hiyo ambayo inaweza kukufikisha mahali husika kwa haraka zaid hivyo mtu unakua hunabudi kukatiza makaburini .je kwa usiku vipi hali ya uoga kwao inakuaje au ilikuwaje??dah kwa upande wangu nimeshaga wahi kupita mara moja nilihisi kama nanyemelewa na kivuli cha maiti maana pako kimyaa usiombe hata panya apite duh unaweza ukaacha ndala. .
 
Ni hisia tuu, hakuna lolote muda wowote kupita makaburini. Ni uoga tuu. Mbona watu wanafanya mambo ya kishirikina na wengine mpaka ngono makabirini na hakuna madhara yoyote? Sembuse kupita njia tuu? Ww pita hakuna shida
 
Unapita tu harafu unatoa hai,huo ndio ustaarabu.

Balaa ni pale utakapojibiwa.
Waislam tumefundishwa kutoa salam tukipita makaburini...

Asalam alykum ya ahlul kabri
"Amani iwe juu yenu enyi watu wa makaburini"
 
Muulizeni mshana jr. Ndio atatueleza vizuri ila kwa upande wangu mimi hua sifanyi mchezo na kwenye makaburi kupita sipiti hata iweje kwani lazima kupita hiyo njia
 
Ni hisia tuu, hakuna lolote muda wowote kupita makaburini. Ni uoga tuu. Mbona watu wanafanya mambo ya kishirikina na wengine mpaka ngono makabirini na hakuna madhara yoyote? Sembuse kupita njia tuu? Ww pita hakuna shida
Kama kuna mambo ya kishirikina basi kunatisha sana. Unajaribu kujifariji
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom