Wale ambao tunatarajia kurudi kijijini kabla hakuja kuchwa, tujuane tupeane mbinu

Pendaelli

JF-Expert Member
Feb 13, 2014
8,668
22,376
Wasalaam waheshimiwa,

Kama heading inavyosomeka. Ni aibu sana, tena sana, kuwa kwenye nyumba ya kupanga hadi una wajukuu.

Ili kuepuka dhahma hii ni kujiandaa mapema kabla jua halijakuchwa, ili kuwahi kutengeneza mazingira kule kijijini tulipokimbia toka ujana. Inabidi kurudi bado ukiwa na nguvu.

Mimi nimekuja mjini miaka kumi na tano sasa, mpaka sasa bila bila, naongeza kumi mingine kama bado ndio nifunge virago.

Hapo mwanangu atakuwa na miaka kumi na tano.

Je, nitakuwa sahihi wakuu? Nipunguze ama niongeze? Kwa sasa nina 32 years.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha ni kama mchezo wa mpira tu kama wewe ni mshambuliaji mbele hushindi goli rudi nyuma uwasaidie wenzako kama mabeki,ila kuwa makini itakapopatikana mpira wa kona wewe ushazoea nafasi ya ushambuliaji upige kichwa kuuondoa golini na siyo upige kichwa ujifunge.
 
Maisha ni kama mchezo wa mpira tu kama wewe ni mshambuliaji mbele hushindi goli rudi nyuma uwasaidie wenzako kama mabeki,ila kuwa makini itakapopatikana mpira wa kona wewe ushazoea nafasi ya ushambuliaji upige kichwa kuuondoa golini na siyo upige kichwa ujifunge.
Ufafanuzi kidogo boss, kichwani RAM ndogo inachukua muda sana kuelewa code kama hizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Plan yako ni nzuri sana, hata mimi nipo huku Dar lkn nimejiwekea time frame nikifikisha miaka 45 narudi nyumbani mkoani. Nimeshaanza maandalizi ya kujenga kibanda huko mkoani ili nikirudi nifikie kwangu. Maisha kwenye big city ni magumu sana, living expenses zipo juu sana tofauti na mikoa mingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa kweli huu mji si rafiki wa maendeleo kwa baadhi ya watu hata upambane vipo!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anko wangu katoka kijijini mimi sijazaliwa. Nimekuja Kukutana naye baada ya mimi kuja Dar.

Mpaka Sasa Ana Miaka 60 Bila Bila.

Anafanya Hustles za Hands to Mouth ( Ambazo Zilipaswa Kufanywa Na Vijana 20 - 35 ).

Kijijini Anaogopa Kurudi, Hana Pa Kuanzia
 
Alichoma sana mihogo mpaka akaja kuwa don pale soko la vyakula Mabibo.

Upande wangu naona mjini hutakiwi uwe mvivu na kuchagua kazi
Hii kazi ya Mihogo imewatoa wengi waliokuwa na juhudi nayo na kuifanya Muda mrefu



Wasalaam waheshimiwa,

Kama heading inavyosomeka. Ni aibu sana, tena sana, kuwa kwenye nyumba ya kupanga hadi una wajukuu.

Ili kuepuka dhahma hii ni kujiandaa mapema kabla jua halijakuchwa, ili kuwahi kutengeneza mazingira kule kijijini tulipokimbia toka ujana. Inabidi kurudi bado ukiwa na nguvu.

Mimi nimekuja mjini miaka kumi na tano sasa, mpaka sasa bila bila, naongeza kumi mingine kama bado ndio nifunge virago.

Hapo mwanangu atakuwa na miaka kumi na tano.

Je, nitakuwa sahihi wakuu? Nipunguze ama niongeze? Kwa sasa nina 32 years.

Sent using Jamii Forums mobile app


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inawezekana huu ni uzi wa kwanza tangu kuanzishwa JF ambao watu wanakiri waziwazi kwamba maisha ya dar ni magumu na kutoboa ni shida. Nyuzi zote hua naona watu wakisifia jinsi ambavyo dar ndio kila kitu na parahisi kutoboa kuliko sehemu nyingine yoyote nchini. Naona akili zimeanza kuwakaa sawa sasa.
 
Anko wangu katoka kijijini mimi sijazaliwa. Nimekuja Kukutana naye baada ya mimi kuja Dar.

Mpaka Sasa Ana Miaka 60 Bila Bila.

Anafanya Hustles za Hands to Mouth ( Ambazo Zilipaswa Kufanywa Na Vijana 20 - 35 ).

Kijijini Anaogopa Kurudi, Hana Pa Kuanzia
Miaka 60 amechelewa sana, alipaswa kurudi home around 40-45. Tunapokaa mjini tusijisahau sana, tutengeneze mazingira mazuri nyumbani ili mambo mjini yakiwa magumu tuweze kurudi home

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom