chongoe
JF-Expert Member
- Mar 22, 2019
- 1,128
- 2,717
Nakusudia sisi ambao tukiongea jambo Mara nyingi huwa linatokea mpaka mda mwingine watu wanahisi labda mchawi naleta Kisa changu wakati nipo mdogo nikiwa nasoma shule darasa tatu nakumbuka hio siku ilikuwa naitaj daftari mbili na pesa bibi hakuwa nayo kwakuwa wazazi wangu wamefariki kwa ajali kuzama baharini wakaniacha nikiwa na miaka miwili kwaiyo ilikuwa naishi na bibi tu.
Sasa wakati naelekea shule nikakutana na jamaa mmoja ambae tuna udugu nae alafu maisha yake sio mabaya baada ya salamu Mimi nikamuomba pesa nikanunue madaftari mawili yule jamaa akanambia pesa anayo Ila hanipi nikimuuliza sababu akasema sikupi tu basi jamaa kwa kuniringishia akatoa pesa zile ili nizione makusudi tu baaada kutoa pesa japo sio zangu ila nilihuzunika mno nikajikuta naropoka tu zitapotea hizo maana alikuwa nazo shilingi laki na nusu baada hapo mi nikaondoka zangu.
Sasa yule jamaa Akaelekea zake pwani kununua samaki baada ya mda ilichukua kama SAA moja akaja maeneo ya nyumbani kuniulizia alipoulizwa imekuaje ndio akatoa mkasa mzima kuwa pesa zake zipotea na wala hakuna hata sehem aliyokaa baada kutoka ongea na Mimi ikabidi jamaa anivumishe mj mzima kuwa Mimi mwanga ila ilimpa tabu sana bibi ile hali ila mi niliona kawaida.
Kisa cha Pili kilimkuta mwalim wangu wa shule alisingiziwa anazini na mwanafunzi wake ila ilikuwa uongo tu wanamzushia sasa mida ya jioni kuna siku nilienda kumsalimia Mimi maisha yangu unga unga mwana kama nilivyosema naishi na bibi tu hali zake ngumu kwaiyo mda mwingine napiga msosi kwa mwalimu nilipofika kwake alikuwa mtu wa huzuni tu kwakuwa lile jambo lina muharibia Kusingiziwa basi pale pale nikasema kumwambia mwalimu kama umesingiziwa Mungu awaangamize waliozusha huu uzushi mwalimu aliitikia ameen.
Nikapiga msosi nikarudi home sasa kufika usiku nakuja kuamshwa kuna watu wamekufa wa familia moja baada ya samaki aina ya kasa na ile familia ndio iliozusha uongo kwa mwalim. Nakumbuka baada kupata ile habari ya msiba haikuchukua mda mwalim alikuja nyumbani akiwa na mkewe usiku ule ule tulikaa nje watu wa nne Mimi nikiwa na bibi yeye akiwa na mkewe alikuja kuniambia nisisimulie Yale maneno na wala nisiwe na tabia ya kuongea nikiwa na hasira kwakuwa nilikuwa mdogo niliona kawaida tu , ninavy visa vingi tena vya watu wadoria walivyo potea siku nne baharini letenu na nyie wenzangu wenye midomo mibaya.
Sasa wakati naelekea shule nikakutana na jamaa mmoja ambae tuna udugu nae alafu maisha yake sio mabaya baada ya salamu Mimi nikamuomba pesa nikanunue madaftari mawili yule jamaa akanambia pesa anayo Ila hanipi nikimuuliza sababu akasema sikupi tu basi jamaa kwa kuniringishia akatoa pesa zile ili nizione makusudi tu baaada kutoa pesa japo sio zangu ila nilihuzunika mno nikajikuta naropoka tu zitapotea hizo maana alikuwa nazo shilingi laki na nusu baada hapo mi nikaondoka zangu.
Sasa yule jamaa Akaelekea zake pwani kununua samaki baada ya mda ilichukua kama SAA moja akaja maeneo ya nyumbani kuniulizia alipoulizwa imekuaje ndio akatoa mkasa mzima kuwa pesa zake zipotea na wala hakuna hata sehem aliyokaa baada kutoka ongea na Mimi ikabidi jamaa anivumishe mj mzima kuwa Mimi mwanga ila ilimpa tabu sana bibi ile hali ila mi niliona kawaida.
Kisa cha Pili kilimkuta mwalim wangu wa shule alisingiziwa anazini na mwanafunzi wake ila ilikuwa uongo tu wanamzushia sasa mida ya jioni kuna siku nilienda kumsalimia Mimi maisha yangu unga unga mwana kama nilivyosema naishi na bibi tu hali zake ngumu kwaiyo mda mwingine napiga msosi kwa mwalimu nilipofika kwake alikuwa mtu wa huzuni tu kwakuwa lile jambo lina muharibia Kusingiziwa basi pale pale nikasema kumwambia mwalimu kama umesingiziwa Mungu awaangamize waliozusha huu uzushi mwalimu aliitikia ameen.
Nikapiga msosi nikarudi home sasa kufika usiku nakuja kuamshwa kuna watu wamekufa wa familia moja baada ya samaki aina ya kasa na ile familia ndio iliozusha uongo kwa mwalim. Nakumbuka baada kupata ile habari ya msiba haikuchukua mda mwalim alikuja nyumbani akiwa na mkewe usiku ule ule tulikaa nje watu wa nne Mimi nikiwa na bibi yeye akiwa na mkewe alikuja kuniambia nisisimulie Yale maneno na wala nisiwe na tabia ya kuongea nikiwa na hasira kwakuwa nilikuwa mdogo niliona kawaida tu , ninavy visa vingi tena vya watu wadoria walivyo potea siku nne baharini letenu na nyie wenzangu wenye midomo mibaya.