Walah tungeathirika leo endapo tungepoteza hazina hii!!!!

Huyu mama ni mama wa watoto wa4,mwanae wa mwisho amemaliza chuo mwaka juzi na ameanzisha mradi wake wa kuku wa mayai.Mume wa mama huyu alistaafu kazi mwaka 2007.Lakini maisha yake hayajabadilika kutokana na miradi ya familia iliyoanzishwa na mkewe.Mama huyu hakuwahi kusoma utotoni,hii inamaana wakati anaoelewa na mumewe alikua hajui kusoma wala kuandika.Ni mwaka 92 ndipo alipojifunza kusoma na kuandika na alikua na umri wa miaka 35!Aliolewe akiwa na miaka 14!Mumewe mama huyu hupenda kumuita huyu mama kiongozi,humuita hivyo kutokana na mama huyu huwa kiongozi hasa.Mumewe mama huyu anasema,"maduka yote matatu,mashamba ya mpunga kule Bariadi,nyuma tano tulizopangisha pamoja na dispensary vyote ni mawazo na usimamizi wa mke wangu.Unajua wakati nafanya kazi sikua napata muda wa kutulia,nilipokua narud nyumbani kutoka safari mke wangu alikua ananiweka kitako na kuniuliza kama kuna hela nimeibakisha kutokana na malipo ya safari ofisini baada ya matumizi safarini,na nilipofanya ubishi alikua mkali kwelikweli.Kutokana na mabaki hayo ya safari na akiba ya mshahara ambayo yeye ndo alilazimisha iwepo aliweza kufanya hayo niliyokueleza,na pia ameanzisha mradi wa kuwasaidia akina mama wenzake kwa kujikwamua kiuchumi kwa kuwakopesha pesa,anasema ndoto zake ni kuja kuanzisha benki".Hayo ni baadhi tu ya ushuhuda wa anayoyafanya mwanamama huyu ambae kafanya mazuri na hakuwahi kwenda shule tofauti na kujifunza kusoma na kuandika tena ukubwani.Hivi ingekua leo mama huyu angeolewa?Kwa jinsi tunavyopimana kwa elimu,rangi na pesa sidhani kama kuna kijana yoyote anaweza kuwa na mke/mume wa aina hii.Tunadhani elimu ndo inamfanya yoyote awe na ubinadamu tunaishia kujuta maishani,sisemi watu wasisome au shule haina maana,hapana,ila kuamini kwamba ukishasoma,au ukawa na hela haimaanishi una uelewa wa yote.Au ukioa/olewa na "msomi" basi ndoa yako itakua na furaha na mafanikio la hasha.Huyu mama amekua msaada kwa familia yake na jamii inayomzunguka,ingekua leo si angeonekana sio binadamu na hastahili kuolewa na msomi kama mumewe?Binadamu wote ni binadamu,vitu vya nje haviwezi kubadili ukweli huu!

anapatikana wapi huyu bibie je naweza pata contacts zake? nadhan huyu anafaa kuwa mfano wa kuigwa duniani kote
 
HorsePower,kwanza niambie bahati ni nini,halafu inakuwaje unadhani kuwa kama angekua na elimu angekua zaidi ya hapo?Kwanini unadhani aliibiwa.Kuna mzee mmoja,mpaka anafariki alikuwa hajui kusoma wala kuandika lakini alikuwa na utajiri wa mifugo,majumba,magari n.k,lakini kwenye "kalkuleta" humuibii na aliendesha utajiri wake vyema.Kama elimu iko kama unavema mbona wapo wenye eilimu ambao hata nusu ya mama huyu mama wameshindwa?Kufanikiwa maishani(kujitambua na kupata unachohitaji) hakuhusiani na sayansi wala "jogo"!

Eiyer utakuwa haukunielewa vizuri, sikusema kuwa elimu ndiyo inayoleta mafanikio ya biashara bali nilisema kuwa elimu ingemsaidia zaidi kupanua na kucontrol zaidi biashara yake. Elimu pia husaidia kumpanua mtu mawazo na pengine hata kuifanya biashara yake kuwa ya kimataifa. Na zaidi ya hapo, elimu inaweza kusaidia kupunguza kuibiwa kwa kutumia kalamu na kuingia kwenye mikataba hatarishi.
Hiyo mifano uliyoitoa ya watu wasiojua kusoma na kuandika, nakubaliana na wewe kuwa wapo na hata mimi nimekutana nao. Ila wao ni wazi kuwa walipata bahati ya kuwa na wasimamizi wazuri na waaminifu.
Hata hivyo nakubaliana na wewe na nilisema mwanzo kuwa si vyema tukawabagua wenzi wetu kwa sababu ya weakness fulani kama elimu, bali tuwatie moyo kuondoka na weakness hiyo kama kuna ulazima wa kufanya hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Niambie uzoefu wako kuhusu wamama wa makabila mengine!

Makabila mengine sio kwamba hawawezi kusimamia biashara za familia ila wanaitaji close supervision kutoka kwa waume zao ili hizo biashara zisimame.
 
Eiyer utakuwa haukunielewa vizuri, sikusema kuwa elimu ndiyo inayoleta mafanikio ya biashara bali nilisema kuwa elimu ingemsaidia zaidi kupanua na kucontrol zaidi biashara yake. Elimu pia husaidia kumpanua mtu mawazo na pengine hata kuifanya biashara yake kuwa ya kimataifa. Na zaidi ya hapo, elimu inaweza kusaidia kupunguza kuibiwa kwa kutumia kalamu na kuingia kwenye mikataba hatarishi.
Hiyo mifano uliyoitoa ya watu wasiojua kusoma na kuandika, nakubaliana na wewe kuwa wapo na hata mimi nimekutana nao. Ila wao ni wazi kuwa walipata bahati ya kuwa na wasimamizi wazuri na waaminifu.
Hata hivyo nakubaliana na wewe na nilisema mwanzo kuwa si vyema tukawabagua wenzi wetu kwa sababu ya weakness fulani kama elimu, bali tuwatie moyo kuondoka na weakness hiyo kama kuna ulazima wa kufanya hivyo.

Mimi naona hapa kinachogomba ni wewe kushindwa ku acknowlegde juhudi ya huyu mama kwa kukimbilia madai ya kuongeza elimu. Je ameweza vipi ku control biashara zake hadi kuwa na mafanikio? Mimi nadhani tunakosea sana pale tunapodhani elimu hupatikana tu darasani kumbe elimu ni kitu ambacho kiko progressive. Inaonyesha wazi kila hatua anayopiga mama inaendana na jinsi anavyojielimisha. Ni wazi atahitaji elimu zaidi ili afanikishe kuendesha benki.....
 
Last edited by a moderator:
DUU mke wangu ana digrii hata kuku hajui kufuga!lol!wanawake wa dot com tabu tupu wapo busy na facebook

badala ya kumlaumu mkeo mshirikiane kama family kuanzisha miradi atlearn tu. hakuna mtu aliyezaliwa anajua kila kitu
 
Eiyer utakuwa haukunielewa vizuri, sikusema kuwa elimu ndiyo inayoleta mafanikio ya biashara bali nilisema kuwa elimu ingemsaidia zaidi kupanua na kucontrol zaidi biashara yake. Elimu pia husaidia kumpanua mtu mawazo na pengine hata kuifanya biashara yake kuwa ya kimataifa. Na zaidi ya hapo, elimu inaweza kusaidia kupunguza kuibiwa kwa kutumia kalamu na kuingia kwenye mikataba hatarishi.
Hiyo mifano uliyoitoa ya watu wasiojua kusoma na kuandika, nakubaliana na wewe kuwa wapo na hata mimi nimekutana nao. Ila wao ni wazi kuwa walipata bahati ya kuwa na wasimamizi wazuri na waaminifu.
Hata hivyo nakubaliana na wewe na nilisema mwanzo kuwa si vyema tukawabagua wenzi wetu kwa sababu ya weakness fulani kama elimu, bali tuwatie moyo kuondoka na weakness hiyo kama kuna ulazima wa kufanya hivyo.

Sijakuelewa dada / kaka , unamaanisha elimu gani? Hizi hizi za necta na mwisho wa siku vyuo vyetu magumash au world class educations? Maana kama ni hizo wengi tulionazo hatuwezi kufuga hata kuku, tunaishia kulilia ajira tu na kuilaumu ccm
 
Last edited by a moderator:
mimi naona hapa kinachogomba ni wewe kushindwa ku acknowlegde juhudi ya huyu mama kwa kukimbilia madai ya kuongeza elimu. Je ameweza vipi ku control biashara zake hadi kuwa na mafanikio? Mimi nadhani tunakosea sana pale tunapodhani elimu hupatikana tu darasani kumbe elimu ni kitu ambacho kiko progressive. Inaonyesha wazi kila hatua anayopiga mama inaendana na jinsi anavyojielimisha. Ni wazi atahitaji elimu zaidi ili afanikishe kuendesha benki.....

like. . . Like. . . Like . . .like!!!!
 
Eiyer utakuwa haukunielewa vizuri, sikusema kuwa elimu ndiyo inayoleta mafanikio ya biashara bali nilisema kuwa elimu ingemsaidia zaidi kupanua na kucontrol zaidi biashara yake. Elimu pia husaidia kumpanua mtu mawazo na pengine hata kuifanya biashara yake kuwa ya kimataifa. Na zaidi ya hapo, elimu inaweza kusaidia kupunguza kuibiwa kwa kutumia kalamu na kuingia kwenye mikataba hatarishi.
Hiyo mifano uliyoitoa ya watu wasiojua kusoma na kuandika, nakubaliana na wewe kuwa wapo na hata mimi nimekutana nao. Ila wao ni wazi kuwa walipata bahati ya kuwa na wasimamizi wazuri na waaminifu.
Hata hivyo nakubaliana na wewe na nilisema mwanzo kuwa si vyema tukawabagua wenzi wetu kwa sababu ya weakness fulani kama elimu, bali tuwatie moyo kuondoka na weakness hiyo kama kuna ulazima wa kufanya hivyo.

Kama elimu inashindwa kumfanya mtu ajitambue,anashindwa kuanzisha hata bustani ya nyanya anabaki kuzurula na makabrasha yake kuomba kazi,itawezaje kufanya yote hayo?
 
Last edited by a moderator:
Mimi naona hapa kinachogomba ni wewe kushindwa ku acknowlegde juhudi ya huyu mama kwa kukimbilia madai ya kuongeza elimu. Je ameweza vipi ku control biashara zake hadi kuwa na mafanikio? Mimi nadhani tunakosea sana pale tunapodhani elimu hupatikana tu darasani kumbe elimu ni kitu ambacho kiko progressive. Inaonyesha wazi kila hatua anayopiga mama inaendana na jinsi anavyojielimisha. Ni wazi atahitaji elimu zaidi ili afanikishe kuendesha benki.....

Hata mimi huyu horse power simuelewi? Elimu ni uwezo sio cheti na kuna formal education na informal education, sasa huyu mama ana informal education ya hali ya juu as kila stage akipita anajifunza na hii ni nzuri zaidi ya darasani, kizaz cha sasa tunaimini sana elimu ya darasani hata kuchagua wenza ndo maana wengi hawafanikiwi as daily matatizo tu,,,

Huyu mama anapata credit za kutosha as ni kifaaa,,, hiyo elimu anayoisema horse power akaisome yeye mwenyewe imsaidie as mama anajisaidia kwa informal education na mzee alifanya wise choice kuoa huyu mama....
 
BADILI TABIA,nimefurahi kwa kuuona mchango wa mume pia,lakini uliyosema ni kweli,tatizo wanaume wengi hawajiamini,na kama hujiamini ni vigumu sana kumuamini mtu yoyote!

Mi hapo kwa red huwa napapinga sana kwani wanaofanya tusijiamini ni wanawake wenyewe! so wao ndo tatizo......
 
Wa mama wa aina hiyo
hawapo tena katika dunia hii ya leo.. Umesema mwenyewe mama alikua
akipata hela zake au za mumewe basi anafikiria kuziweka kwa ajili ya
shuhuli ya maendeleo... Wanawake wa leo hii ukimpa hela cha kwanza
kwenye akili yake ni shoppin salon ili apendeze kama wanawake wenziwe
huko makazini au mtaani akiwa holiday anataka umpeleke south africa mara
atakuambia mbona flani kanunuliwa gari zuri na yeye anataka kama hilo
sasa mwanamke wa namna hiyo utaweza kweli kumweleza mali zako au una
pesa kiasi gani si atazinyonya zote...

Uclaumu ulipoangukia angalia ulipo jikwaa,umekosea ktk uchaguzi,wezako wanakula raha na wake zao ucdhani wote wkivo,pole!
 
Biashara saa nyingine ni Kipaji na bahati na elimu huja kusaidia kuboresha zaidi na kucontrol mapato na matumizi. Naamini angekuwa na ka-elimu zaidi kidogo, yumkini huyo mama tayari angekuwa amefungua bank na kuwa hata na mahoteli makubwa au mabasi ya kwenda mikoani kama siyo kuwa na kampuni yake kubwa! Nilikuwa najaribu kufikiria, kusoma na kuandika kajifunza mwaka 92, which means kabla ya hapo alikuwa anafanyiwa mahesabu na watu, Je, hakuwa anaibiwa kweli? Hakuwa anapewa ripoti za uongo za mapato na matumizi?

Kwa upande mwingine wa shilingi, nakubaliana na wewe Eiyer kuwa saa nyingine tusikubali kupoteza wapenzi wetu tunaowapenda kwa dhati kwa sababu ya elimu duni walizonazo au kutokana na katabia fulani ambacho hakana madhara sana na kanarekebishika. Ni vyema kujitahidi kumuondoa mpenzi wako kwenye udhaifu wake (kama elimu ndogo, mpe moyo ajiendeleze!), badala ya kutafuta kitu "ready made" mara nyingi mahusiano haya huwa hayana unyenyekevu na upendo wa kweli.

Ni mtazamo wangu tu ....

HP

Enzi hizo wakati natafuta mwenza ilifikiwa mahali nikafuta kabisa kipengele cha elimu. In fact, niliondoa vipengele vyote nikabakisha cha 'love first' mengine baadae. Loh, nikajikuta nimeangukia kwa fomu 4 wakati huo mi above degree moja, lakini sasa wote tuko level sawa na tuko fresh kabisa!

Binafsi huwa nawashauri vijana wasiangalie kabisa hiki kipengele cha elimu, lakini ni kama huwa nampigia buzi gitaa, hadi yawakute ndo wanakumbuka ushauri wangu.
 
ongezea pia wako busy kwenda saloon

sasa ulitegemea wasijitunze kwa usasa jukumu lk nn ww suruali?necha ya mama ni u rembo,ndo nyie mnaotaka wake zenu wawe km ma house girl wenu.ht mkitoka ham mech,unanukia casablanka mkeo ananuka kikwapa cha moshi wa kuni,wapi mmepotea c dunia ya sasa saloon km kawa ni jukumu lk kuhudumia mavazi,malazi na mahitaji mengine lau umeshindwa kaa ndani ukune nazi yy akatafute.
 
Enzi hizo wakati natafuta mwenza ilifikiwa mahali nikafuta kabisa kipengele cha elimu. In fact, niliondoa vipengele vyote nikabakisha cha 'love first' mengine baadae. Loh, nikajikuta nimeangukia kwa fomu 4 wakati huo mi above degree moja, lakini sasa wote tuko level sawa na tuko fresh kabisa!

Binafsi huwa nawashauri vijana wasiangalie kabisa hiki kipengele cha elimu, lakini ni kama huwa nampigia buzi gitaa, hadi yawakute ndo wanakumbuka ushauri wangu.

I support you kwa asilimia 100%!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom