Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi waliokula pesa za Maabara za wananchi, nao pia watakamatwe

robinson crusoe

JF-Expert Member
Oct 22, 2020
740
1,214
Rais Samia. Tafadhari sana.

Wakuu wa wilaya wenye tabia ya Sabaya ni wengi.

Wilaya nyingi watu wana vilio vya wakuu hawa ambao walikula michango ya wananchi na hasa kwenye ujenzi wa maabara na madarasa.

Wananchi walitoa michango kwa nguvu, lakini bila huruma pesa zimeliwa.

Hawa nawaona ni kundi moja la akina Sabaya. Siyo wauaji, ni wezi, wanyang’anyi!

Kuthibitisha hilo majina yataanza kutajwa hapa hapa!
 
CAG/TAKUKURU lini mtaanza kukagua matumizi ya Bunge? Au KINGA

Ikiwa mliwahoji wabunge wa upinzani kwanini hawa wanaolipwa huku hawana chama?
 
Sabaya anatosha
Hapana! Ukitaka haki nchi hii wakuu wa wilaya na wakurugenzi waliozulumu haki za wananchi ni wengi. Labda kama unaliangalia jambo hili kiukabila maana nimeanza kuona dalili hizo.
 
Hapana! Ukitaka haki nchi hii wakuu wa wilaya na wakurugenzi waliozulumu haki za wananchi ni wengi. Labda kama unaliangalia jambo hili kiukabila maana nimeanza kuona dalili hizo.

Haki inatendeka kwa aliyekuwa anatenda haki.

Sabaya alitenda haki ndo maana anatendewa haki
 
Back
Top Bottom