Wakuu wa Mkoa na wilaya wachaguliwe kidomokrasia

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,606
8,744
Raisi hawazi kuweka maendeleo kwa kuchagua wakuu wa mkoa ambao wanahama kila siku na wengi wao hawajui mazingara ya mkoa wanaoongoza. Kikubwa na kibaya zaidi ni kwamba kama mkuu wa mkoa akifanya kazi nzuri anahamishwa kwenye mkoa mkubwa na wenye maendeleo zaidi na wale wabaya au ambao hawana uzoefu wanapewa mikoa yenye hali ngumu zaidi kiuchumi. Wakuu wa mikoa wengi kwenye mikoa midogo wanapiga kampeni kucha za kuhamishwa hii ni kutokana na hali ya sasa kwamba hawa wakuu wa mkoa hawachaguliwi na si wenyeji wa mikoa wanayoongioza. Mimi ningependa wakuu wa mikoa wachaguliwe kila miaka minne na wananchi wa mkoa. Hii itafanya kwanza wapiganie maendeleo ya mikoa yao na pili inaleta serikali ya watu iwe imara. Raisi wa Tanzania anateua watu wengi na serikali ni kubwa sana kwasabu wafanyakazi wengi wanafanya kazi za serikali maisha yao yote. Kama tukileta kura tutapunguza hawa wafanyakazi kufikiri kwamba kazi yao ni ya kudumu. Kwasabu hatuna ma Gavana kama nchi nyingine basi tuchague wakuu wa mkoa na wakuu wa wilaya.
 
Tatizo co rais ila ni ubov na uozo wa katiba ya ccm (sijakosea ni katiba ya ccm) na si ya tanzania kwan inampa nguvu,ubabe na kila kitu rais alie madarakan tusali tuombe katiba ibadilishwe
 
Naunga mkono hoja.

Hili ni tatizo la Katiba ya nchi hii, ni lazima mambo haya yatizamwe vema katika katiba mpya tuitakayo Watanzania. Mkuu nakuunga mkono ila naomba kuongezea pia kuwa, Wakuu hao wa Wilaya na mikoa wengi wao hawana hata elimu za viwango na integrities za kuwa viongozi. Kwa mfano ni mara ngapi tumekuta wakuu wa Wilaya ambao formerly walikuwa ni walimu wa primary au secondari? Ni mara ngapi tunakuta wastu wamepewa ukuu huo kwa fadhila?Mnakumbuka issue ya Nape baada ya mzozo wa pale UVCCM. Ni mara ngapi tumeshuhudia wakuu wa wilaya wamekuwa ni mabinti tu tena hata wasio na background ya uongozi?

Hili ni lazima tulivalie njuga ili lishughulikiwe vilivyo katika katiba tutakayoiunda wananchi.

Nawasilisha.
 
uchaguzi wa tanzania uliojaa rushwa majimboni hata hao wanaweza kuchaguliwa kwa pesa zao na sio kwa uwezo wao mimi waliopo nawaona wanafanya kazi zao vizuri sana kuliko hata hao wabunge kwenye maeneo yao km vipi nendeni wenyewe mkachunguze!
 
Hatuhitaji hata wachaguliwe. Kwani wanafanya kazi gani? Dar haina mkuu wa mkoa kwa muda gani sasa na kila kitu kinaenda shwari? Nape Nnauye ambaye ni mkuu wa Wilaya ya hiko kusini hayuko ofisini kwa muda wote na kila kitu kiko shwari. Dawa ni kufuta hivyo vyeo tu. Anayetakiwa kuchaguliwa awe ni Mkurugenzi wa Wilaya na RAS
 
Faithful huwezi kuwalinganisha na wabunge kwasababu wabunge hawana utawala ni wawakilishi tu. Hawa wana budget, sera, na malengo hivyo wabunge si watendaji. Na hii vilevile ni sababu nyingine ya kuchagua wakuu wa mikoa na wilaya. Ni kwanini mbunge akiwa wa upinzania wakuu wa mkoa wanamwona kama ni adui wakati yeye ndiyo mwakilishi wa wananchi, kwanamna nyingine wananchi ni kama maadui sasa wanamwongoza nani?. Kupunguza hili wachaguliwe hata kama kutakuwa na matatizo ni ya wananchi na ni mtu wao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom