Wakuu wa mikoa wamestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa mamlaka ya uteuzi wao

Ngamanya Kitangalala

JF-Expert Member
Sep 24, 2012
501
1,214
Nimejaribu kuangalia sheria na kanuni kadhaa kuhusu hili swala la KUSTAAFU kwa wakuu wa mikoa.

Nimesoma sheria ya utumishi wa umma ya mwaka 2002 (The Public Service Act,2002) pamoja na mabadiliko yake.

Pia nimesoma kanuni za utumishi wa umma za mwaka 2003 (The Public Service Regulations, 2003).

Pia nimesoma sheria ya tawala za mikoa ya mwaka 1997 (The Regional Administration Act,1997).

Mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya ni afisa wa umma (Public officer) anayeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hawa ni wateule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini hawana MUDA MAALUMU kisheria wa kustaafu utumishi wa umma, mwenye mamlaka ya LINI na WAKATI GANI watastaafu utumishi wao wa umma, ni Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Hivyo basi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yeye ndio mwenye MAMLAKA ya kuamua ni LINI na WAKATI GANI mkuu wa mkoa au mkuu wa wilaya anastaafu utumishi wa umma bila kuzingatia umri wao.

Lakini Katbu mkuu kiongozi (Chief Secretary) , Katibu mkuu wa wizara (Permanent Secretary), Naibu latibu mkuu wa wizara( Deputy Permanent Secretary), Katibu tawala wa mkoa(Regional Administrative Secretary), katibu wa bunge (Cleck to the National Assembly), Wakurugenzi wa halmashauri nk, hawa wana muda rasmi wa KUSTAAFU UTUMISHI WA UMMA kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma ni miaka 60, japo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayo mamlaka ya kisheria kuwaongezea muda wa utumishi endapo akiona kuna ulazima wa kufanya hiyo.

Hivyo basi wakuu wetu wa mikoa wamestaafu utumishi wa umma kwa mujibu wa mamlaka ya uteuzi wao (Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
 
Ahsante kwa ufafanuzi!

cc: mzee Zambi - Lindi

Bakanyuka - Mtwara

Mama Mgwhira - Kilimanjaro

Mama Nchimbi - Singida

Ole sakinai - Morogoro
 
Hilo limasai la Morogoro lilikuwa ni kichekesho. Liende tu Monduli likafuge ng'ombe.
 
Ni kauli soft ya kutengua uteuzi wao sio kigezo umri.

Angalia mfano Dr Mahenge bado yupo kazini lakini Anna Mghwira amestaafu.
Anna Mgwira ni Mzee kuliko Mahenge. Au unatishika na zile mvi za ukoo?? Mgwira ana miaka 62 wakati Mahenge ana 59yrs.
 
Nimejaribu kuangalia sheria na kanuni kadhaa kuhusu hili swala la KUSTAAFU kwa wakuu wa mikoa.

Nimesoma sheria ya utumishi wa umma ya mwaka 2002 (The Public Service Act,2002) pamoja na mabadiliko yake....
Hiv braza, hizo sheria (inlcluding lately formed ones na marekebisho yake) unazipata kwenye kitabu gani au zinakuwa wapi. Kuna namna naweza kuaccess hizo sheria(sheria zote kwenye fields zote) nikazosoma zote? Au inakuwajekuwaje?
 
Makongoro ana miaka 62
Makongoro ni mzee 62 years, it’s a political appointment hata ukiwa 98 unaweza kuula. But he is useless, he just uses jina la ukoo kupata anachotaka. I doubt if he can even manage a a street but he is now going to manage a region!
 
Nimejaribu kuangalia sheria na kanuni kadhaa kuhusu hili swala la KUSTAAFU kwa wakuu wa mikoa.

Nimesoma sheria ya utumishi wa umma ya mwaka 2002 (The Public Service Act,2002) pamoja na mabadiliko yake...
Who has the power to sack civil servants, I doubt ministers wanna power hizo. Lakini kila siku wanafukuza wafanyakazi, how? Hata rais Hans mamlaka hayo! Civil servants wanaajiriwa na Utumishi.
 
Back
Top Bottom