Wakuu wa Mikoa tafakarini tena uamuzi wa kuzuia wakulima kuuza mazao nje ya Mikoa

Jabman

JF-Expert Member
Jul 27, 2016
1,005
1,335
Natafakari jambo la busara la wakuu wetu wa mikoa kuzuia wakulima kuuza mazao yao nnje ya mikoa yao. Je wanajua kuwa ni kwanini wanauza nje ya mikoa yao? Je wakulima wanapotafuta soko zuri nje ya mikoa yao ni dhambi? Je mfanyakazi akipata mshahara wake na azuiliwe kuupeka nje ya mkoa wake? Maana mshahara Wa mkulima ni mazao yake.

Naiomba serikali sikivu badala ya kuzuia mkulima kuuza mazao yake iyanunue hayo mazao kwa bei nzuri. Hebu fikiria kama kila mkoa utazuia mazao yake yasitoke , mikoa ambayo kila mwaka in njaa tupu si wataendelea kula viwavi? Basi mzuie pia mazao kuingia mikoani kwenu.

Najua serikali ina nia nzuri ila approach hii si nzuri. Hivi mtendaji wa kijiji naye akizuia itakuwaje?
 
Natafakari jambo LA busara LA wakuu wetu Wa mikoa kuzuia wakulima kuuza mazao yao nnje ya mikoa yao. He wanajua kuwa nikwa nini wanauza nnje ya mikoa yao? Je wakulima wanapotafuta soko zuri nnje ya mikoa yao no dhambi? Je mfanyakazi akipata mshahara wake na azuiliwe kuupeka nnje ya mkoa wake? Maana mshahara Wa mkulima in mazao yake.
Naiomba serikali sikivu badala ya kuzuia mkulima kuuza mazao yake iyanunue hayo mazao kwa being nzuri. Hebu fikiria kama kila mkoa utazuia mazao take yasitoke , mikoa ambayo kila mwaka in njaa tupu si wataendelea kula viwavi? Basis mzuie pia mazao kuingia mikoani kwenu.
Najua serikali INA nia nzuri ila approach hii si nzuri. Hivi mtendaji Wa kijiji naye akizuia itakuwaje?
Hilo zuio limetangazwa na nan?
 
Ni busara kuzuia uuzwaji wa chakula kwenda nje ya nchi na hasa kama kuna uhitaji mkubwa ndani ya nchi yako. Ila hii ya kuzuia chakula kisiuzwe kwenda mkoa mwingine tena ndani ya nchi moja ni hatari sana. Fikiria kila Mkoa uzuie mazao yake yasitoke nje ya mkoa, hivi Dar Es Salaam si watakufa njaa? Singida hawalimi ndizi, hivi tukizuia ndizi toka Bukoba na Mbeya, hali yao itakuwaje? Makatazo mengine watoaji wafikirie mara mbili vinginevyo tutaiua nchi yetu kwa vinywa vyetu!
 
Ni busara kuzuia uuzwaji wa chakula kwenda nje ya nchi na hasa kama kuna uhitaji mkubwa ndani ya nchi yako. Ila hii ya kuzuia chakula kisiuzwe kwenda mkoa mwingine tena ndani ya nchi moja ni hatari sana. Fikiria kila Mkoa uzuie mazao yake yasitoke nje ya mkoa, hivi Dar Es Salaam si watakufa njaa? Singida hawalimi ndizi, hivi tukizuia ndizi toka Bukoba na Mbeya, hali yao itakuwaje? Makatazo mengine watoaji wafikirie mara mbili vinginevyo tutaiua nchi yetu kwa vinywa vyetu!
Hakuna jema lolote kwa mustakabali wa ukuaji wa kilimo kuzuia wakulima kuuza popote iwe ndani au nje ya nchi. Kilimo kama biashara yoyote mtu anakuwa amefanya business plan kabla ya kuwekeza. Inawezekana mkulima alipanga kuuza mahindi kwa bei alizopata nje ndio akawekeza. Sasa serikali inapozuia imeuliza mipango wakulima ilikuwa tangu awali.
Tanzania hatujielewi
 
Alikuwa anajifurahisha tu Ili mdomo usichache aonekane japo kaongea kitu..ila swala hilo haiwezekani mkoa kama dodoma unataka waendelee kula viwavi jeshi
 
Dar jiandaeni kufa njaa mtakula pweza mpaka ziwaue
Sasa mkuu wakikomalia Pweza tu si mwisho wa siku watabaka mpaka vichaa? Hilo tamko ni la kipumbavu sana na kilofa! Ukisema Shinyanga tusisafirishe mchele si utashuka bei sawa na bure huku kwetu? Bukoba wasilete ndizi Shinyanga si bei itakuwa sawa na bure? Waache ujinga hawa!!
 
Haiwezakani nina hamu ya kula nyama ama kufanya manunuzi ndani nina ziada then mtu anizuie kuuza as if tulishika wote jembe...
 
Hakuna jema lolote kwa mustakabali wa ukuaji wa kilimo kuzuia wakulima kuuza popote iwe ndani au nje ya nchi. Kilimo kama biashara yoyote mtu anakuwa amefanya business plan kabla ya kuwekeza. Inawezekana mkulima alipanga kuuza mahindi kwa bei alizopata nje ndio akawekeza. Sasa serikali inapozuia imeuliza mipango wakulima ilikuwa tangu awali.
Tanzania hatujielewi
hatujielewi hasa. na watu wanatakiwa kujua kama ilivyo kwa mikoa pia kuzuia mazao kwenda nje ya nchi ni ujinga mkubwa. hatuwezi kuwa bread basket kama tunazuia kuuza nje, hatuwezi kuwa na kilimo cha umwagiliaji, kilimo hakitaweza kuwa ajira, kutakuwa hakuna uwekezaji wa maana na mabaa ya njaa hayataisha.
 
Should that be true, basi RCs waliotangaza hawajui kuwa mikoa yao ni sehemu ya Tanzania au wanadhani mikoa yao ni nchi.
 
Back
Top Bottom