Wakuu wa Mikoa kama mnagawa mashamba pori muanze na haya yaliyo karibu na jiji la Dar es Salaam

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701


Ukianzia Msata hadi Bagamoyo kupitia Kiwangwa na Fukayose kuna mashamba-pori mengi tu. Ukianzia Mlandizi hadi Chalinze hapo kuna shamba-pori za kufa mtu.

Ulielekea Mtwara kutokea Mbagala huko ndio usiseme utadhani kuna kilimo cha vichaka.

Tunaomba mkoa wa Pwani uwe mfano. Zile sifa eti nina hekari 300 mwingine 3000 wakati zaidi ya matunda pori hakuna hata mpapai zifike mwisho.

Nimesema karibu na Jiji kwa sababu jiji la DSM ni lenye watu wengi wenye rasilimali fedha lakini hawana hata shamba 1/8 ya heka.
 
Basi kusikia wagawe imekuwa nongwa.
Kumbuka miaka inaenda na watu wanaongezeka tutahitaji shule,hospital. Na Malazi ya watu.
Au kila mmoja achukue chake na vizazi vya baadae to hell with them
 
Basi kusikia wagawe imekuwa nongwa.
Kumbuka miaka inaenda na watu wanaongezeka tutahitaji shule,hospital. Na Malazi ya watu.
Au kila mmoja achukue chake na vizazi vya baadae to hell with them
Ubinafsi na ufisadi wa akili wanajifikiria wenyewe tu...hawafikirii kuhusu sustainability
 
Kwanini Tupore Mashamba yasiyoendelezwa badala ya kugeuza Mapori kuwa Mashamba!

Ni sawa kwenda kupora Majumba yasiyoendelezwa kwa hoja hayajaendelezwa wakat kuna Viwanja vingi tu ambavyo havina hata Msingi wa Nyumba
 
Kwanini Tupore Mashamba yasiyoendelezwa badala ya kugeuza Mapori kuwa Mashamba!

Ni sawa kwenda kupora Majumba yasiyoendelezwa kwa hoja hayajaendelezwa wakat kuna Viwanja vingi tu ambavyo havina hata Msingi wa Nyumba
mkigawana mapori yote..vizazi vijavyo vitaishi wapi?
 
Kwanini Tupore Mashamba yasiyoendelezwa badala ya kugeuza Mapori kuwa Mashamba!

Ni sawa kwenda kupora Majumba yasiyoendelezwa kwa hoja hayajaendelezwa wakat kuna Viwanja vingi tu ambavyo havina hata Msingi wa Nyumba
Unakuta mtu/kampuni amezuia hekari kama 20000 zote ziko stratergic area kiasi kwamba hata mwanakijiji asiye na mtaji akapata hata hekari moja tu anamudu maisha yake na kutokuwa mzigo kwa serikali.
Miaka zaidi ya 20 hakuna shughuli yoyote ya maendeleo huoni kwenda kwenye mapori mapya ni kuongeza mapori tu...
 
Serikali hii haitaki watu wapumue? Kila siku Tukio wawape watu muda hata mwaka mmoja wajitafakari
 
IMG-20170611-WA0048.jpg
 
Basi kusikia wagawe imekuwa nongwa.
Kumbuka miaka inaenda na watu wanaongezeka tutahitaji shule,hospital. Na Malazi ya watu.
Au kila mmoja achukue chake na vizazi vya baadae to hell with them
Wangekuwa hawajui wanachofanya kariakoo hadi leo kungekuwa na mtu anahekari 100 za mpunga.
Nadhani ardhi inabadilishwa matumizi muda wowote mahali popote kulingana na maslahi mapana ya wananchi na serikali yao...
 
Unakuta mtu/kampuni amezuia hekari kama 20000 zote ziko stratergic area kiasi kwamba hata mwanakijiji asiye na mtaji akapata hata hekari moja tu anamudu maisha yake na kutakuwa mzigo kwa serikali.
Miaka zaidi ya 20 hakuna shughuli yoyote ya maendeleo huoni kwenda kwenye mapori mapya ni kuongeza mapori tu...

Ukiona umeweza kutofautisha Kati ya Shamba na Pori jua Basi huyo Mtu ndio kufanya Wewe uweze kutofautisha na kutamani kupora!

Kama angekuwa Hakuna alichofanya lingeitwa Pori na si Shamba
 
mkigawana mapori yote..vizazi vijavyo vitaishi wapi?

Kwani Ukigawanya Mapori maana yake unayala na kwenda kuyanya?

Akili za Maskini wengi wanadhani Nafuu Yao ya Maisha itapatikana kwa kupora au kujimilikisha Mali Hovyo hovyo!

Kama Suluhu la Umaskini ni kupora Mali za Watu Basi Azimio la Arusha la 1967 lingekuwa ndio Muarubaini wa Matatizo yote ya Maskini
 
Ukiona umeweza kutofautisha Kati ya Shamba na Pori jua Basi huyo Mtu ndio kufanya Wewe uweze kutofautisha na kutamani kupora!

Kama angekuwa Hakuna alichofanya lingeitwa Pori na si Shamba
Shamba pori ni jina la kumpa unafuu mmiliki lkn ukweli lile ni pori tu kama hujawahi kusafisha hakuna chochote chako ulichoongeza tangu dunia iumbwe au iibuke...
 
Kwani Ukigawanya Mapori maana yake unayala na kwenda kuyanya?

Akili za Maskini wengi wanadhani Nafuu Yao ya Maisha itapatikana kwa kupora au kujimilikisha Mali Hovyo hovyo!

Kama Suluhu la Umaskini ni kupora Mali za Watu Basi Azimio la Arusha la 1967 lingekuwa ndio Muarubaini wa Matatizo yote ya Maskini
sijakusoma..mara kula mara kunya..inawezekana unapoint nzuri..embu zipangilie uziweke hapo tukuelewe....mm hoja yangu ni kwamba si vyema mapori yote wakagawiwa watu as bado watu wanazaliwa na watazidi kuongezeka watahitaji maeneo ya kukaa..serikali nayo itahitaji kujenga mashule masoko, vyuo n.k..so lazima matumizi ya ardhi yawe planned kwa kuzingatia mipango ya baadae..sasa na ww toa hoja yako.
 
Wangekuwa hawajui wanachofanya kariakoo hadi leo kungekuwa na mtu anahekari 100 za mpunga.
Nadhani ardhi inabadilishwa matumizi muda wowote mahali popote kulingana na maslahi mapana ya wananchi na serikali yao...

Lakini ikumbukwe pia kulikuwa na sehemu za mapumziko na hata viwanja vya mazoezi ambavyo Leo vimeuzwa.
Nani kaviuza?
 
Lakini ikumbukwe pia kulikuwa na sehemu za mapumziko na hata viwanja vya mazoezi ambavyo Leo vimeuzwa.
Nani kaviuza?
Nakubaliana na wewe.
Hapo waliouza waliamua kunyonga michezo nchini. Ndio maana huwa sifurahi hata taifa stars ikishinda maana ninauhakika haiwezi wala haitakuwa na consistence kama hakuna basics za michezo.
Ila hapa tunazungumzia mashamba pori mkuu.
Mfano kijiji kinagawia watu hadi heka hata 300 ili paendelezwe leo mwaka wa kumi pamoja na shamba pori hilo kuwa na mito mabonde safi lkn unakuta bado Kuna miti na vichaka vya tangu dunia iumbwe. Hapa naona Kuna tatizo...
 
Back
Top Bottom