kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
naomba kujua hivi ni ruksa kwa mfanyakazi wa serikali kuhama wizara??kwa mfano mimi ni mwalimu katika shule moja ya msingi hapa tanzania ila kwa sasa nipo chuo nasoma na nimeamua kusoma mambo ya utawala yaani public administration lengo langu ni kwamba nikishamaliza degree na masters yangu niombe kuhama wizara yaani toka wizara ya elimu mfano kuhamia wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa kwenye kitengo cha utumishi au mipango sasa ni hatua zipi za kufuata ili niweze kuhama wizara?maana nimeshashuhudia waalimu wengi wanapobadili kozi wakiwa chuo yaani wanaposoma kitu tofauti na education mara tu warudipo kazini wizara ya elimu huwa inawakataa kwa kuwa wamesoma kitu tofauti na elimu hivyo huwa wanasema kwamba bachelor ambayo haina education ndani yake haina msaada kwao hivyo naomba msaada na ushauri kwa hilo!