Wakuu, ni kwa nini kizazi hiki cha sasa kinaona ugumu kutumia herufi H kiusahihi?

Cliffhanger

JF-Expert Member
May 22, 2018
721
1,292
Wakuu, ni kwa nini kizazi hiki cha sasa kinaona ugumu kutumia herufi H kiusahihi? Neno Habari linaandikwa Abari, Hujambo inaandikwa Ujambo, Hayupo inaandikwa Ayupo. Mengine mtaongezea.

Mwanzoni nilifikiri kuwa ni uvivu wa kuandika maneno mengi, kilichonishangaza ni kuwa hata sehemu ambayo inatakiwa itumike A tupu panaandikwa Ha, Kwa mfano neno Amekubali linaandikwa Hamekubali.

Je tufanyeje kama wana Jamii kurekebisha tatizo hil?
 
Ukweli ni kwamba vyakula laini vinaharibu sana vijana wetu
Hasahasa chips
Unakuja kijana anamindevu lakini anaogea utadhani bint
Hasahasa wanaume wa dar
 
Wakuu, ni kwa nini kizazi hiki cha sasa kinaona ugumu kutumia herufi H kiusahihi? Neno Habari linaandikwa Abari, Hujambo inaandikwa Ujambo, Hayupo inaandikwa Ayupo. Mengine mtaongezea.

Mwanzoni nilifikiri kuwa ni uvivu wa kuandika maneno mengi, kilichonishangaza ni kuwa hata sehemu ambayo inatakiwa itumike A tupu panaandikwa Ha, Kwa mfano neno Amekubali linaandikwa Hamekubali.

Je tufanyeje kama wana Jamii kurekebisha tatizo hil?
Watu wameathiriwa na MOTHER TONG zao
 
Hahaja hanasema akukute pale sipendi kwa kweli kuna wale wa L na R kuna wale xx kuna wale wa k,p, hua nachoka kabisa kuendelea kujib sms za hivi
 
Ukweli ni kwamba vyakula laini vinaharibu sana vijana wetu
Hasahasa chips
Unakuja kijana anamindevu lakini anaogea utadhani bint
Hasahasa wanaume wa dar
Hata Insta live huijui bado. . . . We ni jini kisirani!!
 
Mimi hua najiuliza,hivi na huko mashuleni mwao hua wanaandika hivyo? mtu anaandika "Alafu" badala ya "Halafu"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom