Wakuu hivi rafiki akifa ndani kwako Sheria inasemaje kuhusu hilo?

Kwanza Una kwenda Lock up kupisha uchunguzi
Sasa siunajua makarao wetu uchunguzi mwaka 1 kwaiyo huo mwaka 1au zaid upo lock up
Sasa ukitoka ndio utakuwa na cha kuadisia

Sasa Usiombe Yakukute
 
Heshima kwenu wakuu.

Naomba twende moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu. Tuchukulie nina rafiki yangu amelala ndani kwangu then ikatokea bahati mbaya akafa akiwa usingizini, sheria inasemaje kuhusiana na hilo wakuu?

Naombeni muongozo tafadhali. Thanks.
Sheria kanuni na utaratibu ni kwamba atapelekwa monchuary afu atazikwa,,au ulitaka ulale nae siku inayofuata
 
Utakuwa saidia polisi kwa sababu:

1. Wewe ni mtu wa mwisho kuwa na marehemu kabla ya kifo chake.

2. Ni rafiki yako.

3. Amefia kwako

4. Yawezekana unajua chanzo cha kifo chake.

5. Yawezekana wewe ni muhusika wa kifo na au umeshiriki.

6. Kama chanzo cha kifo chake siyo ugonjwa, basi ni wewe, au unafahamu muhusika.

7. Wewe ndiye utatoa muelekeo wa mashahidi wengine mfano, majirani. Majirani wataulizwa kama walimuona mtu anaingia kwako, na je, walisikia sauti? Kishindo? Mabishano? Wataeleza pia tabia yako na Kama una urafiki kiasi gani na marehemu.

8. Utaulizwa nyendo za marehemu kabla ya kuja kwako, mlipitia wapi, alikueleza nini, nk.

9. Marehemu atafanyiwa vipimo ili kuoanisha maelezo na hali halisi ya mazingira ya kifo kama ni ugonjwa au kauawa. Kama kauawa, basi kazi inaendelea.

10. Kumbuka gheto/ nyumba yako itakuwa scene of crime kwa muda.

11. Upelelezi utaendelea na jalada likikamilika, litapelekwa kwa wanasheria wa Serikali huko litachambuliwa, Kama Kuna udhaifu wa ushahidi na au Kuna watu wanahitajika basi wanasheria watashauri.

12. Mpaka hapo, wanasheria watajua kati washukiwa ni nani anafaa kuwa mtuhumiwa yaani ambaye ushahidi unaelemea kwake. Hapo, kama ni wewe utashtakiwa.

13. Kumbuka, kwenye kuchambua ushahidi wanasheria hupima upepo, wanaangalia mfano, A akiwa mtuhumiwa na B akawa shahidi, hii kesi tutashinda?

Kwa mantiki hiyo, wewe unaweza ukawa shahidi namba moja au mtuhumiwa namba moja. Inategemea na legal opinion humo kwa DPP.

Cha msingi usiogope. Kuwa mtulivu usaidie polisi na Mahakama kutafuta haki jinai.
Safi sana mkuu
 
Ukipokea mgeni yoyote ni shart kutoa taarifa katika uongozi wa mtaa wako tatizo lolote litakalo tokea utakua mtuhumiwa wa kwanza wewe
Jambo la msingi ni kuomba tu yasitukute Mkuu, Hio ya kutoa taarifa, inawezekana katika mazingira flani na haiwezekani katika mazingira mengine mfano umetembelewa na mgeni wa jinsi totauti.unaweza kwenda kutoa taarifa kwa kiongozi kweli.
 
Jambo la msingi ni kuomba tu yasitukute Mkuu, Hio ya kutoa taarifa, inawezekana katika mazingira flani na haiwezekani katika mazingira mengine mfano umetembelewa na mgeni wa jinsi totauti.unaweza kwenda kutoa taarifa kwa kiongozi kweli.

Sheria haiangalii mazingira mkuu ni shurti kufany ivyo basi
 
Umenikumbusha mambo kama haya nilikua nawaza sana hata siku nimelala na dem wangu siku ya kwanza kabsa nilishtuka usiku kumchek kama anapumua ndo nkarudi kulala
 
Kama hakuna mwenye ushahidi kwamba alikuja kwako na una nyumba ya fensi na una gari, weka kwenye buti.. kuna misitu na mapori mengi ya kutupa.

Hiyo ndo njia 'salama' kuliko zote.

Otherwise, 'justice' system ya TZ 'itakushughulikia' kwenye 18 zake.
Okay..Tuassume hakuna aliyemuona anaingia ndani kwako..lakini kabla ya kukutana ulikuwa unachat naye mkutane na kuwasiliana naye kwa simu....Sasa hata ukimtupa mtoni hawawezi kufuatilia mitandao ya simu wakajua watu aliokuwa anawasilina nao wa mwisho wakakudaka?
 
Kama hakuna mwenye ushahidi kwamba alikuja kwako na una nyumba ya fensi na una gari, weka kwenye buti.. kuna misitu na mapori mengi ya kutupa.

Hiyo ndo njia 'salama' kuliko zote.

Otherwise, 'justice' system ya TZ 'itakushughulikia' kwenye 18 zake.
Ohooo!! Kumbe hukumuona jamaa alikuwa anachungulia kwenye upenyo wa geti , kisha huyooo kwa mwenyekiti wa mtaa!! Mkuu utanyea Dene mpaka awamu ya kumi!!!
 
Back
Top Bottom