wakuu hebu tuweni serious basi..!!

syano

Member
Jul 17, 2016
26
20
Natumai mu wazma wa afya, mkijiandaa kuupokea mwaka mpya ,kwa neema ya bwana sote tutafika 2017...!!


Mwaka 2016 utakuwa n mwaka ambao stokaa nkausahau katka historia ya maisha yangu kwasabab n mwaka ambao nimekumbana Na changamoto mbalimbali ambazo zimenifanya niamin kuwa Kila mafankio Yana historia nyuma yake...

Mwez may mwaka huu nimehtimu kidato cha sita( japo Kuna changamoto nyng Sana nmezpitia mpaka kufikia hapo), mama ndalichako kafanya yake nkajikuta nakosa sifa za kujiunga Chuo kikuu, ndoto ya kusoma udaktar (MD) ikafia hapo, japo sikuwahi kufikilia kuwa Kuna kufail kimasomo maana uwezo wangu naujua Mimi mwenyewe,
(maumivu ya kufail kufikia lengo wanayajua waliowahi kufail)

Nkaamua kutuliza akili Na kuireset upya nikaona Kuna maisha mengine nje ya hayo,nikaamua kutuma maombi kwa course za diploma Na nikachaguliwa st.joseph university college of health science (dip.in pharmaceutical science) ,, nikaona mwanga tena maana nilipanga mengi kutokea pale...

Kidonda kikatoneshwa tena baada ya wazaz kushindwa kumudu gharama za Chuo, mpango huo ukafai tena ...

Baada ya hapo mfumo ukanichagua tena Chuo cha TIA kusomea dip. in accountancy, pia ikashindikana,,( nkaudanganya ubongo ukakubali Na kuamin Kuna maisha mengine baada ya hapo)


Hali ya kiuchum nyumban iliendelea kuyumba nikaamua kutoka nymban Na kuelekea mkoa mwngne Ili kutafta cha kufanya maana kwa mwaka huu hapakuwa Na uhakika wa Chuo tena,,,

Baada ya kufika huko mkoani ( ugenini) nikatuma maombi kwny kampuni moja ya usafirshaji Kama mtoa huduma kwa wateja, interview ikapigwa tukapita watu kumi nje ya ishirin Na sita ( nikaona mwanga kwa mbaali) ghafla Giza likatanda mbele ya harakati hiyo baada ya kujitokeza kwa harufu ya rushwa( baadh ya watendaji wa kampuni Ile walihitaji hongo Ili nipewe nafasi ile) sikuweza kutoa chochote maana sikuwa Na kitu, waliotoa wakapata nafas Na mpaka Leo hii wanafanya kazi..


Nikaamua kuzba maskio Na kuamin kuwa kun maisha mengine baada ya pale , nikaamua kuzunguka viwandani nikapata matumaini ya kupata kaz katka kiwanda flan, nkapita interview hivyo nkapewa utaratib wa kujiunga , nikaandikiwa attachments znazotakiwa kuwasirshwa ofisin Ili nisubirie tareh 3/1/2017 ambapo niliambiwa ajira ztaanza kutolewa...

Nimefigh vya kutosha Na nimetumia gharama Ili kufankisha zoez Hilo, nikakamilisha..

Jumatatu hii nimeenda Ili nisubmit hizo nyaraka lakin nmeambiwa hakuna ajira mpaka mwez wa tatu mwakan Na boss huyo sijui alikuwa na hasira za nini alikataa hata kuzpokea ....
(nikarudi geto nikiwa hoi ,, maana nmefkia geto kwa rafki angu)



Point yangu Ni kwamba nimewah kuona post nyng Sana za watu wakitafta kazi humu jf lakin Mara nyng watu wamekuwa wakizchangamkia post za madada Tu..sie wanaume post zetu znapitwa Tu,

Sasa wakuu mi sitaki kuamin kuwa hum jamii forums naeza kosa msaada , maana hii sio Mara ya kwanza kutafta humu , Kuna watu wazito humu ndani heb jarbuni kutushika mkono wadogo zenu ,, hatuhtaji kuiba ndo maana tunapambana Ili kuweze kulipwa kwa jasho la haki,..


Mwaka unaelekea ukingoni,
Mungu awabariki Na abariki kaz za mikono yenu katka mwaka ujao 2017...!!

Ahsanteni..!!
 
Aisee dogo pole sana..
Ndiyo tatizo la mabadiliko ya kisiasa yanaweza kuleta mabadiliko yanayotakiwa au mabadiliko hasi.Usikate tamaa endelea kumtanguliza Mungu na vuta subira mambo yatabadilika
Asante mkuu
 
Pole sana,.. kuwa mvumilivu na majibu ya hapa maana kuna watu wankutonesha kidonda tena hapa
 
Wakuu bado nasubiria kaz kutoka kwenu..!

I need to work..
 
kumbeeeh hii ndo sababu unataka kujitoa jamii forum.
me nikushauri tu jaribu kuwa mvumilivu.
 
Back
Top Bottom