Wakurugenzi wa PSSSF wanafanya kazi gani Ofisini? Mambo mengi hayaendi kwa wakati!

kamtesh

JF-Expert Member
Jul 26, 2014
1,395
512
Kama kuidhinisha malipo ya mafao kwa wastaafu walio kokotolewa na kudhibitika wanastahili kulipwa inachukua zaidi ya wiki tena.

Huu ni uzembe wa hali ya juu. Faili la mtu halina tatizo, kusaini ili liende kwa wahasibu ni shida. Au shirika halina hela? Haiingii akili mtu amekokotolea mafao yake baadae ichukue tena wiki au wiki mbili ntu kupata hela yake.

Sasa muingiza ujanja mwingine eti ngazi tatu au tano. Hizo kazi ziko Mbinguni? Watumishi kama nyie ndo mnaofanya mfuko uonekane huna kwa wadau. Kwa urasimu huu, hamuwezi kupata Wanachama wapya.

Sisi wastaafu ndo mabakozi wa mfuko kuhusu huduma zenu. Kama sisi tulioko ndani tunapitia matatizo kama haya ya ucheleweshwaji na urasimu kulipwa, munafikiri tutawahamasisha watu kujiunga kweli?

Wakurugenzi chapeni kazi, ondoeni mafaili ya wateja wenu ofisini. Sio kuwa na mrundikano wa mafaili ofisini. Nk uzembe kwa Mtumishi, badilikeni, lipeni kwa wakati jamani. Value for money please

Kwa menendo huu, wengi watatumbuliwa tuu, hakuna ufanisi PSSSF.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njia sahiii naona wange deligate to director of operation baadhi ya kazi mambo ya ku approve na kutia sign michango ya mwanachama kulipwa baada ya uchunguzi kufanyika, kuna mengi mengi yanatakiwa yapitiwe ili kurahisisha njia za kutoa huduma kwa wanachama.

Anything for love
 
Wamekokotoa, imeonekana ni sahihi, sasa unaulizia wanakwambia, wamemaliza Ila ikiwa ni chini ya milioni 50 itapitia ngazi tatu za maidhinisho na ikiwa ni zaidi ya 50 million, itapitia ngazi tano za kuidhisha.
Swali ni nje inachukua muda gani kuidhinisha mpaka unaambiwa subiria wiki mbili tena eti kuidhisha. Hapo mtu umesota miezi tisa tangia uombe mafao yako. Hii imekaaje? Ndo hoja, wanafanya mini maofsini? Kwasababu mpaka faili linafikia level hii, basi halina tatizo.
Njia sahiii naona wange deligate to director of operation baadhi ya kazi mambo ya ku approve na kutia sign michango ya mwanachama kulipwa baada ya uchunguzi kufanyika, kuna mengi mengi yanatakiwa yapitiwe ili kurahisisha njia za kutoa huduma kwa wanachama.

Anything for love

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nachojua kwa mfano upande wa NSSF ukiwa una withdraw kiwango kikubwa wana viwango vyao, basi nilizima mafile yako yapitie ngazi za juu kwa approve, na kama upo mikoani ni lazima mafile yako yatapelekwa makao makuu ili mkurugenzi aidhinishe malipo,sasa kwa upande wa psssf kama utaratibu upo hivyo basi vumilia taratibu zao zikamilike, hizi ni protocol za mashirika yetu katika uendeshaji wa haya mashirika,
Wamekokotoa, imeonekana ni sahihi, sasa unaulizia wanakwambia, wamemaliza Ila ikiwa ni chini ya milioni 50 itapitia ngazi tatu za maidhinisho na ikiwa ni zaidi ya 50 million, itapitia ngazi tano za kuidhisha.
Swali ni nje inachukua muda gani kuidhinisha mpaka unaambiwa subiria wiki mbili tena eti kuidhisha. Hapo mtu umesota miezi tisa tangia uombe mafao yako. Hii imekaaje? Ndo hoja, wanafanya mini maofsini? Kwasababu mpaka faili linafikia level hii, basi halina tatizo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Anything for love
 
Point taken, basis wako hivo hivo nao. Ila time factor matters a lot.
Mkuu nachojua kwa mfano upande wa NSSF ukiwa una withdraw kiwango kikubwa wana viwango vyao, basi nilizima mafile yako yapitie ngazi za juu kwa approve, na kama upo mikoani ni lazima mafile yako yatapelekwa makao makuu ili mkurugenzi aidhinishe malipo,sasa kwa upande wa psssf kama utaratibu upo hivyo basi vumilia taratibu zao zikamilike, hizi ni protocol za mashirika yetu katika uendeshaji wa haya mashirika,

Anything for love

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila licha ya taratibu hizo, wengi wanakua wazembe katika utekelezaji wamajukumu. Nakumbuka boss wangu, alikua hakai na faili la mtu ofsini kwake. Mafaili yakifika anasoma na kuyapitisha on the same day. Unless faili linamadai yasioeleweka ndo ataliweka pembeni.
Alikua huwezi singizia kwamba faili lipo kwa mkurugenzi. Lakini wengi hawapo hivo, wanarundika mafaili ofsini kwa kisingizio cha tupo kwenye kipindi cha mpito. Kabla yakuunganisha mifuko, tayari logistic nyingi zingekua zilishawekwa tayari kwa kufanya kazi. Data zote muhi za wanachama zipo available tayari.
Sasa kwa hali hii, PSSSF, wanachemka. Lakini kila mwanacha chama salary slip yake inaonyesha alikua anachangia. Mfuko gani, data zake zikoje.
Kiukweli, huu mfuko dina hamna nao, ni kero kwa kwenda mbele.
Njia sahiii naona wange deligate to director of operation baadhi ya kazi mambo ya ku approve na kutia sign michango ya mwanachama kulipwa baada ya uchunguzi kufanyika, kuna mengi mengi yanatakiwa yapitiwe ili kurahisisha njia za kutoa huduma kwa wanachama.

Anything for love

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kero tupu kiukweli Mimi ndio nimepeleka fomu zangu wiki iliyopita.
Je kwa kawaida huwa inachukua wiki ngapi hadi kuipata pesa?
Na je Kuna wanachama ambao wameshaanza kupokea pesa mwaka huu?
Naombeni majibu wadau kwa yeyote anayefahamu ili nijue najipangaje.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukitaka usipate pressure kwa kuidai PSSSF, Wewe ukishajaza fomu, fanya kama umesahau, wala usiangaike kukumbuka.
 
Subiria miezi mi NNE na week tatu. Lakini huko mbele, milundikano ya madai itapungua. Usishangae ikachukua miezi miwili tiu au chini ya hapo.
Ni kero tupu kiukweli Mimi ndio nimepeleka fomu zangu wiki iliyopita.
Je kwa kawaida huwa inachukua wiki ngapi hadi kuipata pesa?
Na je Kuna wanachama ambao wameshaanza kupokea pesa mwaka huu?
Naombeni majibu wadau kwa yeyote anayefahamu ili nijue najipangaje.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wamekokotoa, imeonekana ni sahihi, sasa unaulizia wanakwambia, wamemaliza Ila ikiwa ni chini ya milioni 50 itapitia ngazi tatu za maidhinisho na ikiwa ni zaidi ya 50 million, itapitia ngazi tano za kuidhisha.
Swali ni nje inachukua muda gani kuidhinisha mpaka unaambiwa subiria wiki mbili tena eti kuidhisha. Hapo mtu umesota miezi tisa tangia uombe mafao yako. Hii imekaaje? Ndo hoja, wanafanya mini maofsini? Kwasababu mpaka faili linafikia level hii, basi halina tatizo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Wastaafu wanakula msoto miaka 4 hapo PSSSF,wafanyakazi wakiulizwa wanasema Rais hajasaini pesa hizo kutoka.
 
Back
Top Bottom