Wakurugenzi wa Halmashauri kwenye vikao vya CCM, kutoa taarifa ni sawa?

Mapambano Yetu

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
1,121
2,064
Hii imetokea Mtwara ambapo wakurugenzi wa Halmashauri walikuwa kwenye vikao vya chama ambapo walitoa taarifa za utendaji wao. miongoni mwa taarifa walizotoa ni kufungwa kwa soko la ununuzi wa korosho. source TBC

Binafsi sijaelewa kama wakurugenzi ni wanasiasa au watumishi wa umma? Mbona serikali hii inafanya mambo kinyemelanyemela? sasa kama wakiwa sehemu ya wachangia Sera kwenye chama wataweza kusimamia chaguzi kwa haki? Tume ya uchaguzi inatakiwa kutoa onyo otherwise iwaamuru kuhudhuria vikao vya vyama vyote na watoe taarifa equally

there is a clear bolded line unaotenganisha Chama Tawala na serikali hususan katika utekelezaji wa masuala ya kiserikali. sio jukumu langu kukufundisha juu ya huo mstari. wengi wanajua ila ni ulevi wa madaraka tu. zipo njia za kisheria na kikanuni za kupima utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama kilichoshinda lakini kuita watendaji/waajiriwa wa serikali katika vikao vya ndani vya kichama si njia mojawapo. pengine kwa sasa mtu anaweza asione tatizo ila kuna siku ataliona tatizo na madhara ya ku-politicize utumishi wa umma.
 
Au ndo kutimiza kauli ya mkulu kuwa kila mwanaccm anatakiwa kuogopwa popote alipo? hii nchi tabu tupu, hata hizo tumbua tumbua inabidi ziundiwe tume, isijekuwa yanawakuta ya Mkuu wa Shule aliyekataa kuanzisha Magu - club
 
Kwani wanatekeleza ilani ya chama gani? kwani wanaccm sio watu au sio watanzania?
 
Watajuaje kama ilani yao inatekelezwa bila kupewa taarifa.
NAULIZA JE NCHI TUNAFANYA MAENDELEO KWA SERA ZA CHAMA? MBONA SIKU ZOTE INAPOTOLEWA BAJETI YA SERIKALI HAISEMWI KYWA CHAMA KINATAKA PESA KIASI FULANI ILI KUTEKEZA SERA ZA CHAMA ? MBONA WATENDAJI KAZI KATIKA SEKTA MBALIMBALI NDIO WANAOANDAA MAHITAJI YAO KWA KILA MWAKA KUENDELEZA SEKTA ZAO NA HAWAFIKIRII CHAMA CHOCHOTE KTK KUTAYARISHA BAJETI ZAO?hapa ndipo nashindwa kuelewa.
 
NAULIZA JE NCHI TUNAFANYA MAENDELEO KWA SERA ZA CHAMA? MBONA SIKU ZOTE INAPOTOLEWA BAJETI YA SERIKALI HAISEMWI KYWA CHAMA KINATAKA PESA KIASI FULANI ILI KUTEKEZA SERA ZA CHAMA ? MBONA WATENDAJI KAZI KATIKA SEKTA MBALIMBALI NDIO WANAOANDAA MAHITAJI YAO KWA KILA MWAKA KUENDELEZA SEKTA ZAO NA HAWAFIKIRII CHAMA CHOCHOTE KTK KUTAYARISHA BAJETI ZAO?hapa ndipo nashindwa kuelewa.


Mkuu usisahau kua ilani inayotekelezwa ni ya chama tawala. Chama tawala kina uwezo hata wa kukagua miradi inayotekelezwa katika maeneo husika.
 
Ukiangalia hili kwa undani, hali ya kisiasa nchini, na mwenendo wa utawala wa Serikali hii; utaona kuwa kuna mkakati wa nchi kurudishwa ktk mfuni wa chama kimoja na chama kushika hatamu.

Vv
 
Ukiangalia hili kwa undani, hali ya kisiasa nchini, na mwenendo wa utawala wa Serikali hii; utaona kuwa kuna mkakati wa nchi kurudishwa ktk mfuni wa chama kimoja na chama kushika hatamu.

Vv

Ni vema wafute mfumo wa vyama vingi. Itafikia magari ya serikali yatatakiwa kuweka bendera ya ccm kwa sababu ndicho chama tawala. & kila taasisi ya serikali iwe na bendera ya chama & taifa
 
there is a clear bolded line unaotenganisha Chama Tawala na serikali hususan katika utekelezaji wa masuala ya kiserikali. sio jukumu langu kukufundisha juu ya huo mstari. wengi wanajua ila ni ulevi wa madaraka tu. zipo njia za kisheria na kikanuni za kupima utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama kilichoshinda lakini kuita watendaji/waajiriwa wa serikali katika vikao vya ndani vya kichama si njia mojawapo. pengine kwa sasa mtu anaweza asione tatizo ila kuna siku ataliona tatizo na madhara ya ku-politicize utumishi wa umma.
 
there is a clear bolded line unaotenganisha Chama Tawala na serikali hususan katika utekelezaji wa masuala ya kiserikali. sio jukumu langu kukufundisha juu ya huo mstari. wengi wanajua ila ni ulevi wa madaraka tu. zipo njia za kisheria na kikanuni za kupima utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama kilichoshinda lakini kuita watendaji/waajiriwa wa serikali katika vikao vya ndani vya kichama si njia mojawapo. pengine kwa sasa mtu anaweza asione tatizo ila kuna siku ataliona tatizo na madhara ya ku-politicize utumishi wa umma.
nimekuelewa
 
Ni sawa kabisa maana wao wako pale kufanya kazi ya serikali ambayo inaongozwa na chama cha mapinduzi...sasa kuna ubaya gani wao wakitoa taarifa hapo?
 
Chama Chao serikali yao nchi yao wasiwasi wako wa nini? Wewe subiri siku wakiwa wataweza ambao wako systematic ndo utaona kama wataweza kufanya vikao vyao mahali patakatifu
 
Kwani wanatekeleza ilani ya chama gani? kwani wanaccm sio watu au sio watanzania?

Kwani wakurugenzi ni wanasiasa?Ameuliza swali.Kwenye Halmshauri za kisiasa wanafanya nini?Je hii siyo kazi ya mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa?
 
Tatizo la awamu hii wateule wengi ni wapya na hawajui majukumu yao. Ndio maana DC anamsimamisha kazi Mwenyekiti wa Kijiji! Mwingine kamfunga Diwani kama mtendaji wa kata na vijiji! Tangu awamu ya Mwalimu mpaka ya nne taarifa ya utekelezaji ilani ya uchaguzi imekuwa ikitolewa. Wawasilishaji kwenye vikao ni DC, RC, PM.
 
Tatizo la awamu hii wateule wengi ni wapya na hawajui majukumu yao. Ndio maana DC anamsimamisha kazi Mwenyekiti wa Kijiji! Mwingine kamfunga Diwani kama mtendaji wa kata na vijiji! Tangu awamu ya Mwalimu mpaka ya nne taarifa ya utekelezaji ilani ya uchaguzi imekuwa ikitolewa. Wawasilishaji kwenye vikao ni DC, RC, PM.
Umenena vema
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom