Wakumbuka nini enzi za shule ya msingi?

zingine ni
sikiri mimi maskini,
uvivu wangu nyumbani,
ukiwa huu njiani,
nakufa hapa kwa nini......

kofia nyekundu tarabushi inanipendeza mama..........
Nalalia kulia leo...................... Bibi tarabushi. Nakwambia hapo ndio darasa la tatu nafikiri.


asiyependa shule ni mjinga kabisa, barua ikija aitembeza kote....


karudi baba mmoja,
toka safari ya mbali,
kavimba yote mapaja na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja ili kumtaka hali............


halafu pia enzi hizo watu wa mazingaombwe wanakuja kutuletea mazingaombwe yao mara unatolewa shati jipya la shule, mara hela do!

azimio, azimio, azimio la arusha, lilitangazwa tano mbili sitini na saba azimio la arusha.

kaka yangu sikiliza
nataka kukuambia,
azimio la arusha,
lilizaliwa arusha.............


halafu mambo ya kucheza rede, uki, mdako, kujipikilisha, kiboleni, hahahaaaa we acha tu...

aah jamani mbona mnafurikisha kikombe cha moyo wangu kwa furaha? Laiti kama ingeliwezekana ku- rewind kipindi cha maisha ningerudi hadi wakati wa shule ya msingi!!
 
Nimekumbuka mengi sana lakini kubwa zaidi ni kwenda kulima shamba la mwalimu mkuu, kupalilia hadi kuvuna. It was very interesting manake hakuna aliyekuwa analalamika kuanzia wanafunzi hadi wazazi wenyewe. Ila leo hii things have completely changed hata mwanafunzi kuchapwa tu kwa kukimbia kipindi lazima liwe tifu kubwa. Nway
 
ukifika karibu na nyumbani unaanza kimdalio, cha baba yako, cha mama yako cha dada yako halafu unakimbia.

au tunapinga saliapoo ( ukiwahi kuziona unampiga mwenzako mabao ya mgongoni)

au kuruka kamba
angweke hiyo hiyo angwekwe........... ;

kuwa kuwa mwanangu amina kuwa,
kuwa nikutume kuwa,
majani chai kuwa.................

nilikwenda kwa dada,
nikamkuta shemeji ,
anadishi ugali,
nikadishi kidogo,
funguliarekodi, tukanza kucheza,
Nikacheza kidogo.............................. ha ha haa kweli ya kale dhahabu

ukirudi nyumbani unakuta bibi tukishakula usiku kabla ya kulala lazima bibi atusimulie hadidhi kama akili kufundishwa; nyoka mwenye vichwa kumi na mbili, mtoto wa dawa n.k.
 
Tulikuwa tunapenda sana kuchezea maji na utelezi hasa mvua inponyesha tena bila viatu kama picha hii inavyoonyesha

kitt-713792.jpg
Bila shaka wewe ndiye huyo aliyeshikilia nyeti.
 
..........Nakumbuka nyimbo tu za darasa la kwanza, maana madarasa mengine sikusoma hapa bongo.
Mabata madogo madogo yanaogelea, yanaogelea ktk shamba nzuri la bustani.............
Hesabu mama ohhh hesabu, hesabu ninakupenda ahhhh hakika.....................
...........Vile vile nakumbuka kababu, ice cream, sambusa na uji wa mchele...........I wish enzi hizo zirudi.

Swala ni kukumbuka shule ya msingi iwe umesoma kuzimu au jehanamu. Swa?
 
Nakumbuka ile MIALIMU mianaharamu vitoto vidogo inatumendea..njoo jumamosi kufanya usafi ofisini kwangu...kumbe inataka kukubaka...nyooooo! Nikikutana nayo leo ntaikumbusha..mianaharamu kabisa!
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu, Cheyo primary school then Mwenge Practical Primary school--Tabora
 
umenikumbusha mbali sana mkuu, mimi nilikuwa napiga ngoma katika bendi ya chipukizi huko Cheyo na mwenge primary school Tabora mjini-life was fun!
 
Walimu wenye majibu ya mkato mkato..."kaulize mamako"
Kwa kweli jibu hilo halikuwa sahihi.

Kunywa maji wakati unaona bomba limepasuka chini na kuna vyura kibao-chura!!!!
Viboko vitatu asubuhi na vitatu vingine wakati wa kutoka.
 
Nakumbuka mwalimu mmoja aliwakamata wanafunzi wawili (std 3) darsani wakitukanana eti we una m***zi basi mwalimu ile kuingia tu, akasikia akasema haha leo mtaniambia Ma**zi ni nini wakashindwa kujibu. akawapelekeka ofisini, Kufika ofisini akawauliza walimu eti nimewakuta hawa wanatukanana wanaambiana eti we una Ma**zi sasa walimu mimi natataka waniambie hayo Ma*uzi ni nini?

Mwalimu mmoja akajibu mimi ninachojua hayo mav**i ni matunda ya uwemba si ndiyo walimu hicho kicheko kilichotokea ilibidi wale wanafunzi wapigwe viboko viwili tu. hahaha.
 
nilikuwa mvivu sana kuamuka asubuhi mama akiniamsha nilikuwa namdanganya leo tumeambiwa twende mchana, sikumoja nikakosea step nikamwambia shule imefungwa eebwanaa.. alinibeba kimsobesobe hadi shuleni nikakuta wenzangu wako mstarini mwl mkuu alikuwepo nililambwa mboko kwanza mama akaja mwl wa darasa akaja mwl wa zamu mwisho mkuu mwenyewe wiki nzima matak o yakawa yamevimba sikurudia tena.

Yaani nimecheka mpaka nimelia LOL,mie nakumbuka Juma na Rosa,Juma ana dada,dada wa juma ni Rosa,Juma ni mrefu kuliko.......
 
wandugu,

thread hii ni mahususi kwa chochote unachokumbuka enzi unasoma shule ya msingi.

Mimi binafsi nakumbuka enzi zile nasoma issale primary school kule wilayani mbulu miaka ya 1986-1991 wanafunzi tulikuwa nadhifu, tunaopenda shule, wenye heshima sana. Pia nakumbuka tulikuwa tunacheza halaiki shuleni na hata kwenye matukio kama ya mbio za mwenge au kiongozi wa kitaifa akitembelea wilaya yetu. Moja ya nyimbo za halaiki zinazonikuna mpaka leo ni hii hapa;

" chama chetu kilituongoza hadi uhuru tulipoupata na kinaendelea kuongoza kufikia lengo ujamaa... Mwenyekiti mwl. Nyerere mwenye hekima na wingi wa sifa tanzania..."

ama kwa hakika enzi hizo zilikuwa tamu sana na tulipokuwa tukiimba nyimbo hizi tulikuwa tunanyoosha mkono kuelekea kwenye picha ya baba wa taifa wakati huo akiwa mwenyekiti wa chama na raisi wa tanzania.

Pia nakumbuka kuna waalimu fulani ambo walikuwa wamepitia mafunzo wa jkt basi zamu zao zikifika wanapiga magwanda na wiki hiyo inakuwa mchaka mchaka sio mchezo. Bila kusahau kukimbia mchaka mchaka asubuhi au tukienda kuchota maji lambo na madumu ya lita tano huku tukiimba nyimbo za uhamisishaji kama;

" mchaka mchaka chinja... Aliselema....na mbuga za wanyama tanzaniaaaah ya kwanza ni serengetiii ngorongoroooh manyaraaa na mikumiii oooh tanzania hoooye....

ni hayo tu kwa leo je na wewe ulisoma shule gani ya msingi na wakumbuka nini???

kheh?? Kumbe avatar niliyoikimbia ndio mtumaji wa hii tread pia? Naondoka kama ifuatvyo vuuup!!!
 
Duuhh enzi hizo tution mtawala kwa mng'ong'o, nakatisha mjini yoote toka mitaa ya uhuru mpk mtawala primary kusoma hisabati, hata kuchoka ukirud tuu home tution yazaman jaman
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom