DOKEZO Wakulima wa Tumbaku - Mbogwe tunapata shida kutozwa Fedha Kupitishiwa/kusainiwa Malipo ya Wakulima na Ofisi ya Meneja MBCU LTD

DOKEZO Wakulima wa Tumbaku - Mbogwe tunapata shida kutozwa Fedha Kupitishiwa/kusainiwa Malipo ya Wakulima na Ofisi ya Meneja MBCU LTD

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
MBOGWE .jpeg
1. Viongozi wa AMCOS tunatozwa pesa kila tunapoenda kusainisha/kupitishiwa malipo ya wakulima katika chama kikuu MBCU, Kila malipo tunatozwa Meneja Ndg. Paulo Samweli kuanzia 4mil hadi 10mil kulingana na shedo ya malipo na fedha hii si ya vuongozi bali na yawakulima.

2. Tunahofia msimu huu kutowalipa wakulima kwa asilimia mia sababu fedha nyingi ishachukuliwa na meneja

3. Tumejaribu kuwashirikisha afisa ushirika wilaya pamoja na mrajis wa mkoa lakini hatujapata majibu mpaka sasa.

4. Tunaomba msaada kuondoa hii kero kwani maisha yetu yako hatarini tusipowalipa wakulima fedha zao zote.

5. Mwenyekiti na Bodi ya Chama Kikuu cha ushirika cha Mbogwe na Bukombe pamoja kufikishia malalamiko yetu pia wameshindwa kutatua hii kero, tunaelekea kwenye masoko ya tumbaku lakin hatujapata majibu ya kero yetu.

6. Tunaomba ofisi ya mrajis dodoma ichukue hatua kali ili kunusuru uhai wa Wakulima.
 
Lengo muache kulima, kununua na kuuza tumbaku. Taja hasara 2 za kutumia tumbaku
 
Tumbaku ni zao Haramu kwasababu ndio linachangia kiasi kikubwa kusababisha kansa za koo na mapafu kutokana na uvutaji wa Sigara na ugoro
 
Watanganyika woote Kila sehemu wanalia na bila msaada wwte kwenye taifa lao. Chura aka kizimkazi utackia mm haya sio mambo yangu.
Kazi ni kipimo cha utu
 
Back
Top Bottom