Wakubwa wa jiji, hali ya uzoaji takataka mitaani hairidhishi

Mookiesbad98

JF-Expert Member
Feb 1, 2015
2,300
2,716
Mh Makonda, Mkurugenzi wa Jiji na wengineo wote hali ya uzoaji takataka inatisha.

Tumesikia contract amepewa mtu mwingine lakini maajabu ya Mussa ni pale wakandarasi wa uzoaji takataka wanapokuwa hawana vifaa ikiwemo malori ya uhakika, hawazoi kwa wakati unaotakikana.

Kuna maeneo kama ya Upanga, Masaki huko mkandarasi wao anajitahidi sana kupita kwa wakati na kuzoa lakini maeneo mengi yaliyobaki kuna shida ya kuishi na uozo wa funza baada ya taka kukaa zaidi ya wiki majumbani mwa watu bila kuzolewa.

Unakuta ratiba labda ni Jumapili na Jumatano wazoaji na malori yao mabovu yanayoharibika kila mara hawapiti mpaka baada ya wiki 2.

Tumeona juzi Mjapani katoa msaada umesainiwa wa kujenga dampo la kisasa. Lakini hii isiwe sababu ya Procurement Unit ya jiji kutoa tenda kwa kampuni ambao hazina hata resources zingine hata ofisi hazina.

Na kwa ufuatiliaji, yupo mhasibu mmoja alikuwa katika kampuni ya takataka aliwahi kusema ni biashara ambayo inaleta pesa sana hapa Dar es salaam.

Ni wakati muafaka sasa mtekeleze vema ratiba za uzoaji taka mitaani, hili litapunguza magonjwa pia.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suala la taka ni kubwa kwa kila mji mkubwa. Na pia kuna sehemu zingine hata gari la taka halifiki kwa sababu ya barabara au jiografia kutokuwa rafiki. Pia magari ni machache ungilinganisha na taka zinazozalishwa kila siku.
 
Mh Makonda, Mkurugenzi wa Jiji na wengineo wote hali ya uzoaji takataka inatisha.

Tumesikia contract amepewa mtu mwingine lakini maajabu ya Mussa ni pale wakandarasi wa uzoaji takataka wanapokuwa hawana vifaa ikiwemo malori ya uhakika, hawazoi kwa wakati unaotakikana.

Kuna maeneo kama ya Upanga, Masaki huko mkandarasi wao anajitahidi sana kupita kwa wakati na kuzoa lakini maeneo mengi yaliyobaki kuna shida ya kuishi na uozo wa funza baada ya taka kukaa zaidi ya wiki majumbani mwa watu bila kuzolewa.

Unakuta ratiba labda ni Jumapili na Jumatano wazoaji na malori yao mabovu yanayoharibika kila mara hawapiti mpaka baada ya wiki 2.

Tumeona juzi Mjapani katoa msaada umesainiwa wa kujenga dampo la kisasa. Lakini hii isiwe sababu ya Procurement Unit ya jiji kutoa tenda kwa kampuni ambao hazina hata resources zingine hata ofisi hazina.

Na kwa ufuatiliaji, yupo mhasibu mmoja alikuwa katika kampuni ya takataka aliwahi kusema ni biashara ambayo inaleta pesa sana hapa Dar es salaam.

Ni wakati muafaka sasa mtekeleze vema ratiba za uzoaji taka mitaani, hili litapunguza magonjwa pia.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app

Uzoaji wa taka mjini hapa Dar umezorota sana. Huku Kimanga wako wanaopita wanakusanya pesa ili wachukue taka. Maeneo ya stendi taka zinakusanywa na kuoza karibu na maeneo yanayouza vyakula, matunda, mboga nk. Kuna tatizo ambalo limejitokeza siķu za karibuni.
 
Mleta uzi mada hii ni murua kabisa, hili ni tatizo kubwa sana hasa Jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa huu, Bw. Makonda kama angetilia mkazo suala hili tu pekee basi angekuwa kafanya jambo kubwa sana katika kipindi cha uongozi wake, kuliko ambavyo anafanya sasa ( haya ni maoni yangu, kila mtu ashinde mechi zake).
Kuliko kuweka mgambo au vijana wa JKT kukamata wachafua mazingira, mkuu huyu angeanza tu na hawa wakandarasi wa kuzoa taka ambao wanalipwa mamilioni ya kodi zetu.
Kwa kuwa viongozi wengi haya makandarasi ya kuzoa uchafu ni ya jamaa zao au ya kwao, jambo hili kwa kipindi kirefu limekuwa chimbo la watu kula hela za bure, hivyo hutasikia kiongozi yeyote akikemea katika hili.
Kampuni za taka hazina vifaa.
MAGARI mabovu ya kuzolea taka ambayo nayo yamekuwa uchafu na mengine kutelekezwa sehemu za taka, huku viongozi wakipita maeneo hayo Kwnye V8 zao na suti kali kali na kutazama tu, huu ndiyo upuuzi wa mtu mweusi, utashi huku anaishi pachafu.
Makampuni haya hayana wafanyakazi wa kutosha, na hao wachache wanafanyakazi bila vifaa vya usalama.
Namshauri mkuu wa mkoa, vita ya usafi wa jiji ianze na wakandarasi wa kuzoa taka walio makini, hao ukiwabana na kuwalipa vizuri, watasimamia usafi huko mitaani na hutahitaji jeshi wala JWTZ.
Ni suala la kumkagua mkandarasi na eneo lake, kama ni chafu, penalty ya malipo yake, na anayefanya vizuri alipwe vizuri hasa.
Kwa kufanya hivyo sidhani kama kuna mkandarasi atakubali raia amuangushe kwa kuchafua hovyo eneo lake.

Madiwani waache siasa na ushabiki wa siasa huku usafi tu katika maeneo yao, unawashinda, ni AIBU SANA!

USAFI KATIKA MAENEO YETU, UTAOKOA KIASI KIKUBWA CHA FEDHA ZA KUTIBU MAGONJWA YASIYO YA LAZIMA.
NI BORA KUWA NA BUDGET KUBWA YA USAFI KULIKO TIBA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huku kwetu wanachukua hela wanaondoka taka hawajawahi kutoa ukiwauliza au kuiwakatalia wanakwambia kuchukua hela ipo kisheria ukimuliza kuja kuchukua taka hawanaga jibu basi ukiwauliza sheria gani inakukinga wew mvhukua hela bila kutoa taka haijui halmashauri za miji kuweni wastaarabu basi 6000 hiyo mnachukua na taka tunahangaika kutoa wenyewe tunaumizana.
 
Back
Top Bottom