Wakristu 23 wauawa na kundi la Islamic State nchini Misri

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Watu wenye silaha nchini Misri, wameshambulia basi moja lililokuwa limewabeba wakristo wa dhehebu la Coptic na kuwauwa watu kadhaa.

Gavana wa jimbo hilo, anasema kuwa watu 23 walimiminiwa risasi na kuuwawa, huku wengine wapatao 25 wakijeruhiwa, katika shambulio hilo lililofanyika kusini mwa Misri.

Wakristo wa dhehebu la Coptic nchini Misri, wamekuwa wakishambuliwa mara kwa mara, hasa katika miezi ya hivi karibuni, ambapo tawi la kundi la wapiganaji wa Islamic State nchini Misri, wamekiri kutekeleza mashambulio hayo.

Mnamo Aprili mwaka huu, watu 40 waliuwawa, baada ya makanisa ya Coptic yalipolipuliwa mabomu.


Chanzo: BBC
 
Mimi mkristo, tusichanganye uislam na Islamic State japo vina mahusiano. Kundi lilaumiwe kwa matendo yake lakini uislam usipakwe matope kwa matukio ya hilo kundi.

Magerezani kuna majina ya kikristo na kiislam pia, lakini bado hatusemi dini hizo ni za wahalifu au majambazi.
 
Tukiwaambia hiyo dini ni aya za shetani wanatokwa povu, ona sasa, watu hao wamewakosea nini maskini!!
Leo mashambulizi ya ndege za marekani na washiriki wake,dhidi ya kundi LA ISIS,huko Syria yameua watu 102,watoto wakiwa 42,
Mambo kama haya,ndio yanawapa hasira Waislam duniani kote,wanaona Marekani na washirika wake(Judeo Christianity ) wanataka kuuangamiza Uislam,kwaiyo makundi kama ISIS,yanatafuta soft target na kulipiza kisasi,
Kila mislam anaamini kwamba,uislam na uarabu,umeshushwa hadhi na umedharaulika sana,wanataka kurudisha hadhi waliyokuwa nayo karne zilizopita,adui yao mkubwa ni Ukristo,(marekani,western culture,)
 
Leo mashambulizi ya ndege za marekani na washiriki wake,dhidi ya kundi LA ISIS,huko Syria yameua watu 102,watoto wakiwa 42,
Mambo kama haya,ndio yanawapa hasira Waislam duniani kote,wanaona Marekani na washirika wake(Judeo Christianity ) wanataka kuuangamiza Uislam,kwaiyo makundi kama ISIS,yanatafuta soft target na kulipiza kisasi,
Kila mislam anaamini kwamba,uislam na uarabu,umeshushwa hadhi na umedharaulika sana,wanataka kurudisha hadhi waliyokuwa nayo karne zilizopita,adui yao mkubwa ni Ukristo,(marekani,western culture,)
Sasa wanarudisha hadhi kwa kuua wasiokuwa vitani? Nyie na huyo Allah asiyeweza kuilinda dini yake mpaka mumsaidie kwa kuua watu ndio mnadhani mtapelekwa peponi kweli? Hebu nipe aya walioitumia kuwaua hao watu waliokuwa kwenye basi.
 
7c74a1f2cb558f56032a661b80a6e05d.jpg
apo wanafanyaje?
 
Kinachouma ni pale taratibu za Mgeni kuja Kutawala Mwenyeji; kila nabii alikuja kwa jamii yake!
Je kuwapiga Magaidi wa kiislam ndio kufanywa kwa mauaji Afghan , Irak , Libya(wanaokua wahanga ni raia wema). Sishabikii Mauaji ila ht hapa Tz nachukizwa na Tamaduni za Kizungu hasa Vinguo vifupi japo makanisa yameamka ila tuliopo sokon tunawashuhudia utandawazi unavyowatandaza!! WHEN IN ROMAN DO AS ROMAN NA SISHAURI ARABIC COUNTRIES WASHABIKIE UWESTENIZESHEN!!
 
Back
Top Bottom