Wakristo mjitafakari kwenye suala la mahari, mnawakosea sana binti zenu. Kilichotokea hivi karibuni kwa jamaa yangu kina funzo

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,065
26,999
Rafiki yangu(37) ni single father with 3 kids, ana mchumba wake mganda ambaye naye ni single mother(37 yrs) with one kid. Alikuwa rafiki yake wakati wakisoma chuo, wakaja kukutana tena miaka kadhaa baada ya ku graduate, jamaa anaishi Dar, mrembo anaishi Kampala wakaanzisha uhusiano.

Muda wa kwenda kutoa mahari ulikuwa mwezi uliopita. Nilikuwa mmoja katika ujumbe uliyoongozana na rafiki yangu na matchmaker(mshenga) wake. Wakati wa kunegotiate mahari wazazi wakaanza na 15 million Ugandan ambayo ni kama milioni 9 ya Tanzania(walitaja idadi ya ng'ombe then ikawa converted to cash).

Tukakomaa wakashusha mpaka milioni kumi ya Uganda. Tutakomaa tana wakashusha mpaka milioni tano ya Uganda. Mwisho kabisa wakakomea shilingi milioni nne na point kadhaa ya Uganda ambayo ni sawa na milioni tatu ya Tanzania.

Hapo wakasema haipungui hata mia. Tukaomba tupewe muda tukatafakari kisha tutatoa taarifa ni lini tutarejea tena ukweni kukamilisha hiyo mahari. Kumbuka hapo tumefikia hotelini. Basi tulipoenda kujadiliana tukamuuliza muoaji kama bajeti yake ina mruhusu kulipa milioni tatu cash akasema no way out hawezi kulipa mahari yote hiyo.

Akasema alitegemea wangesema milioni moja halafu yeye angetoa laki tano au saba huku akitoa ahadi ya kumalizia mahari iliyo baki(waganda hakunaga kubakiza mahari). Wakati hapa Tz kutokumalizia mahari ni heshima kubwa sana kwa wakwe, kwasababu kwanza, inaonyesha kwamba bibi harusi sio bidhaa unayo weza kuinunua dukani na kwamba wazazi wa bibi harusi wamekutunuku binti yao ukaanzishe nae familia. Lakini pili Inaonyesha kwamba wewe muoaji unampenda sana mkeo kiasi kwamba haupo tayari kusubiri mpaka upate mahari kamili.

Mshenga akamuuliza bwana harusi. Hauna alternative mahali kwingine, yaani hauna mchumba mwingine?
Jamaa akajibu nina mchumba mwingine yupo Tanzania ila yeye ni muislamu na kwao wanataka tufunge ndoa ya kiislamu(mshenga akajibu nilitaka kushangaa unakosaje alternative?!).

Kisha akamuuliza. Upo tayari kufunga ndoa ya kiislamu? Jamaa akajibu yupo tayari. Mshenga akajibu tunasubiri nini? Mshenga akaenda kutoa taarifa ukweni kwamba tunarudi Dar kujipanga na tutarejea tutakapo kuwa tayari.

Jamaa karudi Dar ndani ya hizo wiki mbili kavuta jiko na harusi ikafanyika kwa gharama ya kawaida sana, na mtoto mwenyewe mbichi kabisa ndiyo kwanza kamaliza form four(anaweza kuwa bado hajawa dis flowered).

Baada ya kuoa jamaa kamjulisha mchumba wake wa uganda kwamba hayupo tena interested na ndoa kwa sababu hizo gharama haziwezi na kwamba ameamua kuoa sehemu nyingine. Mwanamke wa kiganda kachanganyikiwa sasa hivi anawalaumu wazazi wake tu.

Wakristo hizo zama za wanaume kutoa mahari za mamilioni hazipo tena. Jifunzeni kwa waislamu, mnawakosesha binti zenu ndoa kwa sababu ambazo hazina msingi. Kwanza karne hii ukiona mtu "amepandwa na kichaa " cha kutaka kuoa unapaswa kumpa mke haraka kabla kichaa hakija toweka, ili kichaa kiondoke tayari akiwa na mke ndani ndiyo akumbuke 'kumbe mimi fala hivi'.

NB: Kwa sababu ya complications zake, familia nyingi za kikristo huwa zina experience ndoa chache sana ikilinganishwa na familia za kiislamu. Dini ya kiislamu imerahisisha sana suala la ndoa. Matokeo yake familia nyingi za kikristo huwa hazifahamu saikolojia siasa za waoaji.

Ni hivi muoaji anapo kuja kwenye familia yako, usifikiri hajaona mwanamke mwingine au hana option nyingine. Most of the time muoaji anapofikia hatua ya kuja kujitambulisha nyumbani kwenu tayari anakuwa na option zingine kama mbili, tatu au hata nne.

Nikija kwenye familia yako kuchumbia, halafu ukaniletea complications ngumu, mimi nitakacho kifanya nita kuachia binti yako nitaenda kwenye familia ambayo haitaniwekea complications ngumu.

Ninapokuja kwenye familia yako usinichukulie kwanza kama mtu ambae ninataka kumuoa binti yako, nichukulie kama mtu ambae nimekuja kutazama kama familia yako ina complications au la!
 
Moja ya vitu vinavyosingiziwa ukristo ni swala la mahari.
Ukristo haupo specifically kuhusu insu ya mahari..ukristo ni mtu kumuacha Baba yake na Mama yake, swala mahari kiasi hiki ama kile ni tamaa za wakristo si ukristo.
Huwezi lipa mahari uwezo huna usioe nenda kawe padri wa katoliki

Lofa hatakiwi kuoa atasumbua watu na mke kwa ulofa wake

Kipimo cha kuonyesha mwanaume.yuko fit sio tu ule mkuki wake ulioko ndani katikati ya suruali yake ndani ni uwezo wa kulipa mahari
 
Kirahisi hakidumu
Mwanamke ameshazishwa halafu eti unahitaji mahari ya milion? kwa kipi? Yaani hawa ambao wakija wanataka uwahuudumie kuanzia chupi hadi nywele vyote kwako yeye hana chopchote cha kuoofer zaidi ya stress na mawivu yasiyo na kichwa wala miguu.

Bado akutie ukilema wazazi ukiona kweli Mwanaume amejitokeza kuja kukuondolea hilo tatizo nyumbani kwako shukuru Mungu mruhusu kwa moyo mmoja kuliko kugeuza mwanamke kuwa saleable products
 
Mwanamke ameshazishwa halafu eti unahitaji mahari ya milion? kwa kipi? Yaani hawa ambao wakija wanataka uwahuudumie kuanzia chupi hadi nywele vyote kwako yeye hana chopchote cha kuoofer zaidi ya stress na mawivu yasiyo na kichwa wala miguu.
Bado akutie ukilema wazazi ukiona kweli Mwanaume amejitokeza kuja kukuondolea hilo tatizo nyumbani kwako shukuru Mungu mruhusu kwa moyo mmoja kuliko kugeuza mwanamke kuwa saleable products
Mkuu mnawaonea sana wanawake..mbona jamaa anaongoza kwa goli 3?
 
Huwezi lipa mahari uwezo huna usioe nenda kawe padri wa katoliki

Lofa hatakiwi kuoa atasumbua watu na mke kwa ulofa wake

Kipimo cha kuonyesha mwanaume.yuko fit sio tu ule mkuki wake ulioko ndani katikati ya suruali yake ndani ni uwezo wa kulipa mahari
Sijui chochote zaidi kuwa swala la mahari halipo specific ndani ya Biblia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom