Wakristo Iraq wasema hawana wa kuwalinda

Ustaadh

JF-Expert Member
Oct 25, 2009
413
19
Kiongozi mmoja wa wakristo nchini Iraq, Askofu Athanasios Dawood, ameiambia BBC, kuwa Wakristo nchini Iraq, hawana mtu wa kuwalinda, na hawana la kufanya ila kuondoka nchini humo.

090713130924_church_body226.jpg

Askari akilinda kanisa moja Baghdad

Askofu Dawood, alisema Marekani imeshindwa kutekeleza ahadi iliyotoa kuwapatia Wairaqi demokrasi, na kwamba maisha ya Wakristo yalikuwa bora zaidi, chini ya utawala wa Saddam Hussein. Askofu Dawood alisema hayo nchini Uingereza, wiki moja baada ya waumini zaidi ya 50, kuuwawa ndani ya kanisa mjini Baghdad, baada ya kutekwa nyara na wapiganaji wa Kiislamu.

Lakini mbunge mmoja Mkristo nchini Iraq, Yonadem Kanna alisema, Wakristo wanafaa kubaki nchini humo, kupigania haki zao. Inakadiriwa kuna waKristo nusu milioni nchini Iraq, maelfu kwa maelfu wakiwa wamekimbia tangu Marekani na washirika wake, kuivamia Iraq mwaka wa 2003.

....................
Inaelekea uvamizi wa marekani na washirika wake umeleta balaa kuliko neema kwa baadhi ya wananchi wa Irak. Kipi kifanyike?
 
Hilo linchi halikaliki tena, Washia wanawaua Wasuni 'n viceversa, Wakristo wanauawa kila iitwapo leo na makanisa yanachomwa moto, bora Wakristo wahamie nchi nyinginezo ambazo zina wakristo wengi kwa usalama wao maana Waislamu wakishakuwa wengi ndani ya nchi huwa ni balaa tupu. Ndio maana hatutaki mambo ya OIC na Mahakama za Kadhi Tanzania, ni kiama hicho kwa amani ya nchi yetu!
 
Wakristo kamili, hawawezi kusema hawana wa kuwalinda. Ila kama ni wale wakristo wasindikizaji wataema hawana wa kuwalinda.

Kwa kuwa ninatumaini watakuwa ni wakristo wasiowasindikizaji, basi ni kipindi kigumu sana kwa mapito ya kanisa nchini Iraq. Maandiko yanasema, Bwana asipoulinda mji wale waulindao wakesha bure. Nami nikiwa mtumishi wake Kristo Yesu, ninaagiza ulinzi wa jeshi la Mungu lipitalo jeshi la jamhuri ya Iraq na majeshi ya magaidi liwalinde watoto wa Mungu waliopo Iraq. Ninaamru haya kupitia jina la Yesu, lipitalo majina yote, Amen.
 
Wakristo kamili, hawawezi kusema hawana wa kuwalinda. Ila kama ni wale wakristo wasindikizaji wataema hawana wa kuwalinda.

Kwa kuwa ninatumaini watakuwa ni wakristo wasiowasindikizaji, basi ni kipindi kigumu sana kwa mapito ya kanisa nchini Iraq. Maandiko yanasema, Bwana asipoulinda mji wale waulindao wakesha bure. Nami nikiwa mtumishi wake Kristo Yesu, ninaagiza ulinzi wa jeshi la Mungu lipitalo jeshi la jamhuri ya Iraq na majeshi ya magaidi liwalinde watoto wa Mungu waliopo Iraq. Ninaamru haya kupitia jina la Yesu, lipitalo majina yote, Amen.

Ameni na ikawe hivyo kwa utukufu wa Mungu aliye hai juu Mbinguni ambaye uweza wake hauna kikomo,
naye hufanya mambo kwa ajili yake mwenye,
 
bora Wakristo wahamie nchi nyinginezo ambazo zina wakristo wengi kwa usalama wao
Buchanan,
wakiondoka, ni nani atawahubiria hao waislamu injili!
They have to remain there to be a light or the country will go into total darkness. Let us uphold them in Prayers!
 
nawapa pole sana wakristo wa Iraq
lakini wasije wakamwacha shetani
akaitawala nafsi yao......
na Mungu atawasaidia
 
Sisi tulioishi katika jamii za waislamu wengi tunayajua hayo, In Islam it is a crime to be a non muslim, yaani ukibadili dini ni kosa la jinai, adhabu yake ni kifo, hivyo si ajabu muislamu kukubagua kwa sababu sheria za dini yake zinaruhusu, ni part of their iman, kuchomwa kwa makanisa usiende mbali neda zanzibar utaona mambo yalivyo magumu huko if your a non muslim
 
Sisi tulioishi katika jamii za waislamu wengi tunayajua hayo, In Islam it is a crime to be a non muslim, yaani ukibadili dini ni kosa la jinai, adhabu yake ni kifo, hivyo si ajabu muislamu kukubagua kwa sababu sheria za dini yake zinaruhusu, ni part of their iman, kuchomwa kwa makanisa usiende mbali neda zanzibar utaona mambo yalivyo magumu huko if your a non muslim
Wacha uongo wako wewe!
 
Kiongozi mmoja wa wakristo nchini Iraq, Askofu Athanasios Dawood, ameiambia BBC, kuwa Wakristo nchini Iraq, hawana mtu wa kuwalinda, na hawana la kufanya ila kuondoka nchini humo.

090713130924_church_body226.jpg

Askari akilinda kanisa moja Baghdad

Askofu Dawood, alisema Marekani imeshindwa kutekeleza ahadi iliyotoa kuwapatia Wairaqi demokrasi, na kwamba maisha ya Wakristo yalikuwa bora zaidi, chini ya utawala wa Saddam Hussein. Askofu Dawood alisema hayo nchini Uingereza, wiki moja baada ya waumini zaidi ya 50, kuuwawa ndani ya kanisa mjini Baghdad, baada ya kutekwa nyara na wapiganaji wa Kiislamu.

Lakini mbunge mmoja Mkristo nchini Iraq, Yonadem Kanna alisema, Wakristo wanafaa kubaki nchini humo, kupigania haki zao. Inakadiriwa kuna waKristo nusu milioni nchini Iraq, maelfu kwa maelfu wakiwa wamekimbia tangu Marekani na washirika wake, kuivamia Iraq mwaka wa 2003.

....................
Inaelekea uvamizi wa marekani na washirika wake umeleta balaa kuliko neema kwa baadhi ya wananchi wa Irak. Kipi kifanyike?
Wataukumbuka sana utawala wa Sadam Hussein.
 
Tunaomba Bwana wa majeshi awanusuru hawa Wakristo Iraq na jamii zote duniani zinazoonewa. Amen.
 
Back
Top Bottom