Wakirejea CCM hawa na mimi najiunga live

Nelson Masaduki

JF-Expert Member
Oct 27, 2017
346
380
CCM imejivunia watu.Wote walikuwa upinzani. Nasubiri kuona Wema Sepetu, Nyalandu, Lowassa, Lissu, Sumaye, Kingunge kujiunga CCM. Ukitazama kwa makini utaona kwamba, upinzani uliobaki ni upinzani wa kupinga mazuri yanayofanywa na kuungana na watu walioko nje kuikosoa serikali hata katika mazuri yanayofanyika. Kama upinzani ungefanya kama wakati wa JK, kumkosoa mabaya anayofanya, basi tungesema upinzani unakua.

Leo tunahamasisha kumkwamisha Mh. ambaye anayafanya yale ambayo tulikuwa tunayapigia kelele kama wapinzani. Tumeongea sana kuhusu kupunguza safari, kubana matumizi, kuondoa posho zisizo za msingi, kutunzarasilimali za nchi, kupigania Utanzania wetu, kuwajibisha watumishi wabadhilifu na kuacha kuhamisha hamisha watumishi pale wanapokosea, kufanya maamuzi magumu na kupigania hali za wanyonge.

Kwa kiwango kikubwa, naona mengi anatekeleza na ndio kwanza mwaka wake wa pili huu. Tumuunge mkono, upinzani ubaki kidogo kukosoa wanapokosea sio kupinga mazuri.
 
Mazuri lazima yafanyike kwa akili, kufuata sheria na katiba na bila ya chuki na visasi. Bila hivyo hayo mazuri ni mabaya na hatuyataki.
Sisi ni binadamu na lazima tutendewe kama binadamu huku utu na heshima ya kitanzania ikizingatiwa.
Hata Gaddafi alifanya mengi mazuri kuliko yeyote Afrika lakini kwa vile hakuzingatia hayo hapo juu aliishia kuchomekwa vijiti sehemu za siri na kuuwawa kama mbwa koko
 
Hutaeleweka sana kwa kizazi cha kuhoji.

Maana, wanahoji hadi mate yao wenyewe kuwa siyo matamu wakati utamu wa pipi ni mate ya mutu binafsi.

Japo, Sepengaz siyo mpinzani wala mwanasiasa bali ni muigizaji wa kila jambo kwenye maisha yake hivyo hajui anachoigiza kabisa.

Muondoe tu kwa watu watakao rudi CCM hata kule alikoenda ni mzigo nasubiria tamko la mwenye chair wa CDM soon, ataleta mrejesho kuwa sepengaz ni mzingo.
 
CCM imejivunia watu.Wote walikuwa upinzani. Nasubiri kuona Wema Sepetu, Nyalandu, Lowassa, Lissu, Sumaye, Kingunge kujiunga CCM. Ukitazama kwa makini utaona kwamba, upinzani uliobaki ni upinzani wa kupinga mazuri yanayofanywa na kuungana na watu walioko nje kuikosoa serikali hata katika mazuri yanayofanyika. Kama upinzani ungefanya kama wakati wa JK, kumkosoa mabaya anayofanya, basi tungesema upinzani unakua.

Leo tunahamasisha kumkwamisha Mh. ambaye anayafanya yale ambayo tulikuwa tunayapigia kelele kama wapinzani. Tumeongea sana kuhusu kupunguza safari, kubana matumizi, kuondoa posho zisizo za msingi, kutunzarasilimali za nchi, kupigania Utanzania wetu, kuwajibisha watumishi wabadhilifu na kuacha kuhamisha hamisha watumishi pale wanapokosea, kufanya maamuzi magumu na kupigania hali za wanyonge.

Kwa kiwango kikubwa, naona mengi anatekeleza na ndio kwanza mwaka wake wa pili huu. Tumuunge mkono, upinzani ubaki kidogo kukosoa wanapokosea sio kupinga mazuri.
katika SIASA lolote laweza tokea na katika SIASA usisemee moyo wa mwenzio na wana SIASA sio watu wa mchezo mchezo ipo siku isiyo na jina wanaweza watarudi ati.
 
katika SIASA lolote laweza tokea na katika SIASA usisemee moyo wa mwenzio na wana SIASA sio watu wa mchezo mchezo ipo siku isiyo na jina wanaweza watarudi ati.

Nasikia wanasiasa siyo watu wa kisportsport kabisa.
 
Tatizo unachukulia siasa kama ndoa ukishaingia hutakiwi kutoka. Siasa ni kama burudani kama mpira sema huku watu wanacheza na ulimi refa jecha.

Kuhama ni sehemu ya maisha ya siasa yoyote anaweza kuhamia popote na akaponda alipotoka hiyoo ni kawaida.

Umemezeshwa siasa za chuki,visasi na ubinafsi ndo maana unaona ajabu watu kuhama.
 
Tangu zamani tulionya kuwa chama ni taasisi inayohitaji misingi, tukajibiwa chama ni watu na siyo misingi!!!

Mbowe must Go
 
Sasa Sumaye ana mchango gani kwa taifa? Amekuwa waziri mkuu miaka 10 lakini hakuna lolote
 
Kama maisha yanazidi kuwa magumu zaidi inamaanisha hayo yanayofanyika si mazuri tuliyoyataka, bali ni maigizo yake.
 
Wewe tayari ni ccm unasemaje kuwa utajiunga live, hebu rudia ulichokiandika na kichwa cha habari yako..
 
Wewe tayari ni ccm unasemaje kuwa utajiunga live, hebu rudia ulichokiandika na kichwa cha habari yako..

Sijawahi kutangaza rasmi kuwa ni mwana CCM. Ila nilitangaza rasmi kuwa namuunga mkono kwa kuwa anafanya yale ambayo viongozi wetu wa upinzani walikuwa wanayapigia kelele. Sioni haja ya kuendelea kumpinga na kumsumbua Rais wangu. Huyu ni rais wetu wote nje ya chama na ndani ya chama chake. Hivyo, mpango wangu wakija hao jamaa na mie nitakwenda jukwaani nitamke japo maneno machache kuwa narudi katika CHAMA CHAO
 
Back
Top Bottom