Wakina mama kwa nini ni wagumu kuwalipa wafanyakazi wa ndani...

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Yaani housegirl anamiaka sita hajawahi kulipwa mishahara....
Akidai anaambiwa kwani mbona nakununulia nguo nakukulisha...
Akikomaa utasikia mbona nakulea hapa kama mwanangu
Akizidi zaidi utasikia ukirudi kwenu utapata tabu sana, Umesahau ulivyokuja umepauka!!!!

Wana wakike tatizo ni nini kuwafanyia ufisadi watoto wa wa wanawake wenzenu ?...
Kwa nini inakuwa vigumu kuwalipa wadada wa kazi?
Je mkiambiwa mwawekee na pesa mifuko ya jamii mfano NSSF/PPF inakuwaje....

Nini Chanzo cha tatizo?
 
Wanawake wengi wanachuki za kijinga,hawana roho ya upendo hasa kipengele cha"wao kwa wao".


Ma-housegirl walio wengi wanapata taabu sana,manyanyaso,matusi wakati mwingine na kipigo cha hali Juu.

Wanawake,mama zetu badilikeni sana.
 
Wanawake wengi wanachuki za kijinga,hawana roho ya upendo hasa kipengele cha"wao kwa wao".


Ma-housegirl walio wengi wanapata taabu sana,manyanyaso,matusi wakati mwingine na kipigo cha hali Juu.

Wanawake,mama zetu badilikeni sana.
Tatizo litaanza atakapoanza kupendeza...
Hawana tofauti na wezi wa makinikia, kumnyonya msichana wa watu alafu mrabaha sufuri...
 
Huyo ana roho mbaya tu, ni wajibu wako kumnunulia nguo, mafuta na kumpa hela ya nywele na mshahara wake uwe pale pale. Kazi za nyumban zinachosha sana jamani, hawa wadada wanajitahidi sana.

Ni vile tu wamama wengine hawajielewi hivi mtu anakaa na watoto wako na unawakuta salama kwanini usimpende binti wa kazi kama ndugu yako?
 
Huyo ana roho mbaya tu, ni wajibu wako kumnunulia nguo, mafuta na kumpa hela ya nywele na mshahara wake uwe pale pale. Kazi za nyumban zinachosha sana jamani, hawa wadada wanajitahidi sana.

Ni vile tu wamama wengine hawajielewi hivi mtu anakaa na watoto wako na unawakuta salama kwanini usimpende binti wa kazi kama ndugu yako?

wewe unajitambua vizuri sana. good mum!
 
Kuna Jirani Yetu Pamoja Na Mapungufu Yake Ila Suala La Kulipa Mishahara Yuko Vizuri Huwa Wakishindwa Kuelewana Na Wafanyakazi Wake Huwa Anawaita Tu Jamani Ee Kama Kuna Mtu Kachoka Kazi Aniambie Anadai Sh Ngapi? Tuachane Salama Isifike Hatua Tuanze Kulaumiana
 
Back
Top Bottom