Kyenju
JF-Expert Member
- Jun 16, 2012
- 4,621
- 1,706
Habari wanajamvi, Hii topic ilitakiwa iende kwenye Jukwaa la Siasa lakini kwa kuwa walengwa wakuu wako huku nimeona ni vema niitupe huku. Nimekuwa najiuliza swali, kwanini Wakinadada/mama wengi huwa wanatoa michango yao kwa wingi kwenye Jukwaa la MMU lakini kwenye majukwaa mengine hasa lile la Siasa hawaonekani kabisa tofauti na Wanaume/Vijana wa Kiume maana wengi wao wanacheza pande zote. Naomba walengwa waniambie, tatizo ni nii, je, ni waoga wa siasa? Na kama ni waoga wa Siasa je, hii Hamsini, Hamsini wanayoitaka kwenye Uongozi wataipata, au waendelee kupata upendeleo? Acha kunywa maziwa tu jaribuni na nyama ngumu. CC Faizafoxy a.k.a Mrembo. Mamdenyi na wengine wanaothubutu.