Wakina Dada/Mama wa JF mbona mnalikimbia jukwaa la Siasa.

Kyenju

JF-Expert Member
Jun 16, 2012
4,621
1,706
Habari wanajamvi, Hii topic ilitakiwa iende kwenye Jukwaa la Siasa lakini kwa kuwa walengwa wakuu wako huku nimeona ni vema niitupe huku. Nimekuwa najiuliza swali, kwanini Wakinadada/mama wengi huwa wanatoa michango yao kwa wingi kwenye Jukwaa la MMU lakini kwenye majukwaa mengine hasa lile la Siasa hawaonekani kabisa tofauti na Wanaume/Vijana wa Kiume maana wengi wao wanacheza pande zote. Naomba walengwa waniambie, tatizo ni nii, je, ni waoga wa siasa? Na kama ni waoga wa Siasa je, hii Hamsini, Hamsini wanayoitaka kwenye Uongozi wataipata, au waendelee kupata upendeleo? Acha kunywa maziwa tu jaribuni na nyama ngumu. CC Faizafoxy a.k.a Mrembo. Mamdenyi na wengine wanaothubutu.
 
Well..mtazamo wangu!
Jukwaa la siasa!

Limejaa siasa chafu na uropokaji..usiokuwa na tija! Watu wanaenda kishabiki ,kuumbuana,kutukanana,kushadadia yasionamaana! Kiasi kwamba maana nzima ya kujenga nchi haipo! Ccm na chadema kazi kubishana tuu...wanachotaka hakieleweki..kelele tuu ka walevi wa minazi!(sorry to say,but thats the truth)

though
Sio wote.. Wapo wanaota points za maana ambazo kiukweli ni wachache sana tofauti na waropokaji!
Me kwaujumla siasa ya Tanzania,wengi ni ushabiki mandazi ili wapate hela,ila wazalendo walishazikwa na imani zao!

Kuna watu wana mitusi na midomo michafu mule...ambao nadhani ukimeet nao personal uwaulize whats their problem,hawawezi kujibu..zaidi ya ushabiki wa chama.

Hao wanachama na viongozi nao ndo walewale hamna kitu..wapo kimaslahi zaidi.

Mmu..humu kuna ishu za kujenga ambazo zinalenga maisha yetu tunayoyaishi directly or indirectly. Ingawa ndio wehu na waropokaji wapo ila tunawajua na kuwapa dosage zao vizuri cos kila kinzchoongelewa humu atleast kitakugusa ama utaelewa! Kuliko mafumbo ya kisiasa yanayohusu vyama.

Mmu ni mapenzi,mahusiano na urafiki... Ambapo ndo kunagusa mioyo ya wadada kwa urahisi kuliko fujo za Siasa ,kampeni,na vyama!
 
Binafsi uwa nasoma tu bila kuchangia...mana ngumi za siasani si mchezo...
 
Hahaha!!!

Zile fujo za kule ni wadada/wamama wachache wanaziweza aisee...

So far binti yangu sweetlady na mke wangu measkron ni kati ya wanawake wachache wanaoziweza zile mbilinge za kule...
 
Last edited by a moderator:
Hahaha!!!

Zile fujo za kule ni wadada/wamama wachache wanaziweza aisee...

So far binti yangu sweetlady na mke wangu measkron ni kati ya wanawake wachache wanaoziweza zile mbilinge za kule...

Pia kuna ban za kufa mtu, lakini ndiyo ulingo mwenyewe ni kupambana tu.
 
Last edited by a moderator:
Mie huwa nasoma mara kwa mara ila sina ushabiki wa kushobokea wanasiasa mpaka niwaseme vibaya walio na mawazo tofauti ambapo ndo kazi kubwa huko. Kwa hiyo huwa napita kimya kimya ya nini kutukanwa
 
Habari wanajamvi, Hii topic ilitakiwa iende kwenye Jukwaa la Siasa lakini kwa kuwa walengwa wakuu wako huku nimeona ni vema niitupe huku. Nimekuwa najiuliza swali, kwanini Wakinadada/mama wengi huwa wanatoa michango yao kwa wingi kwenye Jukwaa la MMU lakini kwenye majukwaa mengine hasa lile la Siasa hawaonekani kabisa tofauti na Wanaume/Vijana wa Kiume maana wengi wao wanacheza pande zote. Naomba walengwa waniambie, tatizo ni nii, je, ni waoga wa siasa? Na kama ni waoga wa Siasa je, hii Hamsini, Hamsini wanayoitaka kwenye Uongozi wataipata, au waendelee kupata upendeleo? Acha kunywa maziwa tu jaribuni na nyama ngumu. CC Faizafoxy a.k.a Mrembo. Mamdenyi na wengine wanaothubutu.
Kwa sababu hakuna jipya zaidi ya mambo ya usaliti wa ZZK.
 
Aisee kule acha tu paitwe sihasani afu kama vile pana wenyewe!

Yani unaweza ukajikuta umepewa likizo ya lazima (ban) usipokuwa makini

Kuna siku mtu alinipa jibu hilo heeh mpaka nikasahau mlango nilioingilia...!!siku hizi ni mpitaji tu
 
Problem is wanawake wengi wanakuwa easily influenced katika siasa
Ni wachache wanakuwa na misimamo huru na pia we tend to be too emotional
It takes balls biiiig balls kusema mawazo yako katika siasa na si mawazo pia kujibu kwa hoja pia
 
Back
Top Bottom