Wakina-Baba na Mama Mlio Viongozi Mafisadi Mnaaibisha Familia na Jamii Zenu Daima..

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
....Mnasahau kuwa yote mtendayo katika karne hiii yanaandikika

....Mnasahu kuwa katika jamii zetu majina ya ukoo ni utamaduni mkubwa na wa kuendelezwa kizazi hadi kizazi

.....Mnasahau kuwa tukio kubwa moja miongoni mwa wanafamilia ndiyo mwangwi na taswira wa familia hiyo machoni pa wanajamii

.....Mnasahau viapo mlivyo kula mbele ya wananchi kuwa mtalitumikia taifa letu na wananchi wake kadri ya uwezo wenu kimawazo na kivitendo

......Kifupi, mnaacha aibu kubwa katika familia zenu. Pamoja na kuwa kila mmoja anahukumiwa kwa vitendo vyake, msishangae kuona familia nzima zinahukumiwa kutokana na tamaa na ubinafsi wenu kizazi hiki na kijacho. Mnatia madoa majina masafi ya familia. Na kwa vile jamii nzima imezingirwa na matendo ya rushwa na ufisadi wa kila aina; makalipio, lawama, mafunzo, ushauri na yote yanayoweza kuwasaidia kuachana na vitendo hivyo hayafanikiwi wala kuwafikia. Pia kwa vile familia na jamii kwa kujali tamaduni zetu zinajikuta zikikaa kimya kuwasuta kwani bado mnategemewa kifamilia; basi uhalalisho wa vitendo vyenu vya utomvu umekuwa ukipata msukumo usiokusudiwa na usio pingamizi.


SteveD.
 
SteveD, You said it right. Nina rafiki zangu ambao wazazi wao ni baadhi wa mafisadi maarufu. Yaani ninapoongea nao inabidi nichague maneno ninayoongea kwa makini.. Maana ninafikiri hata wao hawajisikii vizuri kuona nchi nzima inavyoupigia kelele ufisadi wa wazazi wao. I don't know wanajisikiaje wanapoingia kwenye nyumba za Mungu kuhudhuria ibada, maana I guess lazima nadhiri zao huwa zinawashitaki mioyoni mwao. Huwezi kukaa nyumbani mwa Mungu ukiwa umejikunyata ukisali wakati the next person pembeni mwako ana data zote za ufisadi wa familia yenu. I can't imagine myself being in that situation.. It is tough..

Yes, Mafisadi wameiba pesa nyingi mno, lakini sidhani kama wanazifurahia hizo pesa kwenye era hii ambayo kila mtu ana data zote kuhusiana na jinsi wao walivyotuhujumu uchumi wetu.

Kitu kingine; Hata level ya interaction kati yetu na hao watoto wa mafisadi imepungua, maana they know their parents looted our economy, na sisi tunafahamu the formula they used to steal our money. Sasa hivi nafikiri watakuwa wana-interact kivyao-kivyao tu, yaani between watoto wa mafisadi na watoto wengine wa mafisadi. Hii ni dhambi kubwa sana kwa wazazi. Watoto wenu hawaku-deserve all this kama nyie msingetuhujumu uchumi wetu. Watoto wenu wanalipa humu humu duniani madhambi mliyoyafanya nyie wazazi mafisadi. This is very unfair to your children. If your children were given a chance to choose parents, I don't think they'd have chosen you!!!!!
 
Mpaka kieleweke safari hii, PIGA, UA,GARAGAZA ukweli utaanikwa juani mchana kweupe! KIla jambo lina wakati wake na wakati uliokubalika TZ ndio huu, tuvute buti wataumbuliwa mmoja baada ya mwingine! Ushauri wa bure kwa mafisadi, ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji!Kaeni mkao wa kuliwa, sisi tukikaa mkao wa kula.
VIVA TANZANIA....
 
Ila ni vyema tumewajua na historia ijue kuwa fisadi families ni izi so that in future none of them shuold dare becomming a leader
 
SteveD, You said it right. Nina rafiki zangu ambao wazazi wao ni baadhi wa mafisadi maarufu. Yaani ninapoongea nao inabidi nichague maneno ninayoongea kwa makini.. Maana ninafikiri hata wao hawajisikii vizuri kuona nchi nzima inavyoupigia kelele ufisadi wa wazazi wao. I don't know wanajisikiaje wanapoingia kwenye nyumba za Mungu kuhudhuria ibada, maana I guess lazima nadhiri zao huwa zinawashitaki mioyoni mwao. Huwezi kukaa nyumbani mwa Mungu ukiwa umejikunyata ukisali wakati the next person pembeni mwako ana data zote za ufisadi wa familia yenu. I can't imagine myself being in that situation.. It is tough..

Yes, Mafisadi wameiba pesa nyingi mno, lakini sidhani kama wanazifurahia hizo pesa kwenye era hii ambayo kila mtu ana data zote kuhusiana na jinsi wao walivyotuhujumu uchumi wetu.

Kitu kingine; Hata level ya interaction kati yetu na hao watoto wa mafisadi imepungua, maana they know their parents looted our economy, na sisi tunafahamu the formula they used to steal our money. Sasa hivi nafikiri watakuwa wana-interact kivyao-kivyao tu, yaani between watoto wa mafisadi na watoto wengine wa mafisadi. Hii ni dhambi kubwa sana kwa wazazi. Watoto wenu hawaku-deserve all this kama nyie msingetuhujumu uchumi wetu. Watoto wenu wanalipa humu humu duniani madhambi mliyoyafanya nyie wazazi mafisadi. This is very unfair to your children. If your children were given a chance to choose parents, I don't think they'd have chosen you!!!!!

Mkubwa hii ni kweli kabisa, yani nina jamaa yangu siku hizi hata kunipigia simu imekuwa ngumu. Maana anafahamu kwamba ile janja yake ya kwenda college full time bila kubeba box nimeshaigundua si bure bali ni Ufisadi.

Mafisadi watu wabaya sana, hawa jamaa wamenunulia watoto wao nyumba kwenye best neigborhood. Lakini sasa tumeshajua kwamba sio bure bali ni pesa zetu wavuja jasho.
 
Hao nin wachache tu lakini CCM hawana mshipa wa Noma .Wataiba nakujengea hoja .Muoneni Makamba kwa mfano ndipo mjue .Lakini we utu inakuwa kazi .Makelele yanamfanya hata Mkapa sasa hawezi kutembea kifua mbele anakimbia wananchi wenzake .Ndiyo tukaze buti hadi kieleweke .
 
SteveD, You said it right. Nina rafiki zangu ambao wazazi wao ni baadhi wa mafisadi maarufu. Yaani ninapoongea nao inabidi nichague maneno ninayoongea kwa makini.. Maana ninafikiri hata wao hawajisikii vizuri kuona nchi nzima inavyoupigia kelele ufisadi wa wazazi wao. I don't know wanajisikiaje wanapoingia kwenye nyumba za Mungu kuhudhuria ibada, maana I guess lazima nadhiri zao huwa zinawashitaki mioyoni mwao. Huwezi kukaa nyumbani mwa Mungu ukiwa umejikunyata ukisali wakati the next person pembeni mwako ana data zote za ufisadi wa familia yenu. I can't imagine myself being in that situation.. It is tough..

Yes, Mafisadi wameiba pesa nyingi mno, lakini sidhani kama wanazifurahia hizo pesa kwenye era hii ambayo kila mtu ana data zote kuhusiana na jinsi wao walivyotuhujumu uchumi wetu.

Kitu kingine; Hata level ya interaction kati yetu na hao watoto wa mafisadi imepungua, maana they know their parents looted our economy, na sisi tunafahamu the formula they used to steal our money. Sasa hivi nafikiri watakuwa wana-interact kivyao-kivyao tu, yaani between watoto wa mafisadi na watoto wengine wa mafisadi. Hii ni dhambi kubwa sana kwa wazazi. Watoto wenu hawaku-deserve all this kama nyie msingetuhujumu uchumi wetu. Watoto wenu wanalipa humu humu duniani madhambi mliyoyafanya nyie wazazi mafisadi. This is very unfair to your children. If your children were given a chance to choose parents, I don't think they'd have chosen you!!!!!
Nikifufuka, umesema mengi kweli ndugu na ni ukweli mtupu!! Ina huzunisha.

Yaani nina baadhi ya rafiki walio watoto wa viongozi, hata kunipigia simu siku hizi imekuwa kasheshe, maana wanajua niko hapa JF naongelea jinsi ya kutokomeza ufisadi na jinsi ya kulinusuru Taifa letu. Katika kujadiliana najikuta nikitaja majina ya wazazi wao bila kupenda na kwa heshima ya marafiki zangu, inabidi kuminya kuongea mambo mengine kwani nitawakwaza kinamna.

Si hivyo tu, hata wao wangelipenda sana kujiunga na JF na kuonesha ujuzi wao katika majadiliano mbalimbali, lakini wanashindwa kutokana na kuwa, kila siku, kila kona na karibia kila thread wazazi wao wanabondewa, wanarushiwa maneno makali na kufunuliwa siri zao za ndani... kwa sababu tu mmoja wao katika familia (haswa mzazi) amejihusisha katika vitendo vya kifisadi akiwa kiongozi Serikalini au katika shirika la umma. Wamezihukumu Familia Zao.

SteveD.
 
Mpaka kieleweke safari hii, PIGA, UA,GARAGAZA ukweli utaanikwa juani mchana kweupe! KIla jambo lina wakati wake na wakati uliokubalika TZ ndio huu, tuvute buti wataumbuliwa mmoja baada ya mwingine! Ushauri wa bure kwa mafisadi, ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji!Kaeni mkao wa kuliwa, sisi tukikaa mkao wa kula.
VIVA TANZANIA....
Mashoo, hakika mkuu, kila jambo lina wakati wake.... huu ni wakati ambao wazazi walio viongozi au kupatakuwa viongozi na kujihusisha na ufisadi watasutika. Ni wakati ambao wanaangalia nyuma na kuona kinyaa walichokisababisha na kile ambacho wanalazimika kuishi nacho. Ni wakati ambao unaogopeka maana mtu hawezi kujua nini kitaandikwa kuhusiana na maovu ambayo alipata kuyafanya gizani na kutegemea kuwa hayatajulikana kamwe. Ni Wakati Mbaya Kwa Waliojihusisha, Tatizo Kubwa ni kuwa sisi sote ni wanajamii... makosa ya mmoja huathiri jamii yote, hivyo bila makusudio, wanajamii wanajikuta wakiwalaumu wanafamilia maana ndiyo beneficiary wakubwa wa ufisadi wa huyo kiongozi.

SteveD.
 
waswahili wanasema "aliyeshiba hamjui mwenye njaa" so hata tupige kelele vipi hawawezi kubadilika wala kuona haya kwa sababu wenyewe walioshiba wanasapotiana...dawa ni kupanga upya mashambulizi
 
Ila ni vyema tumewajua na historia ijue kuwa fisadi families ni izi so that in future none of them shuold dare becomming a leader

Njowepo, ndiyo hapa naweza kurudia kusema kuwa, viongozi mafisadi wanasahau kabisa kuwa hukumu ya vitendo walivyofanya kama wanafikiswa mahakamani si kwenda jela tu, bali jamii zina hukumu zake ambazo wala haziandikiki na wala hazina majaji... hukumu hizi zinawalenga wanafamilia zaidi..... Wanafanya yote haya wakisahau hili swala. Mwanafamilia hata kama atakuwa na uwezo wa kufanya kazi, hata kama atakuwa msafi namna gani..... hukumu ya jamii itamwandama tu, hazikwepeki kutokana na jinsi jamiii zetu zilivyo. Hukumu za jamii ni sawa na zile hukumu za jadi ambapo, ukoo mzima unao share surname fulani unajikuta ukiwekwa kizingiti hata baada ya kupigwa fine ya ng'ombe/mbuzi kadhaa na majunia ya mchele!!!


Mkubwa hii ni kweli kabisa, yani nina jamaa yangu siku hizi hata kunipigia simu imekuwa ngumu. Maana anafahamu kwamba ile janja yake ya kwenda college full time bila kubeba box nimeshaigundua si bure bali ni Ufisadi.

Mafisadi watu wabaya sana, hawa jamaa wamenunulia watoto wao nyumba kwenye best neigborhood. Lakini sasa tumeshajua kwamba sio bure bali ni pesa zetu wavuja jasho.
Mtanganyika... hilo la nyumba ndiyo usiseme, hata kama mtoto huyo atakuwa amefanya kazi na kuweza kupata nyumba hiyo kwa bidii zake.... Ni vigumu mno kwa wanajamii kuamini kuwa hiyo nyumba ni yake kwa nguvu zake.... sasa hili doa la nini jamani kwa wanafamilia wenu kwa nyie wazazi mlio mafisadi?! Clearly, they seem to overlook this kind of honorary punishment in society...


ule msemo kil mtu atabeba msalaba wake mnautafsiri vipi?

Mtu wa Pwani, mimi nadhani msemo huo unalenga zaidi katika hukumu za mahakama na hukumu za kiimani, yaani hukumu mbele ya Muumba wetu.

Kwenye mahakama, ni kuwa mtu hawezi kujitolea kufungwa on behalf ya mwingine kwa makubaliano na mahakama. Na vivyo hivo, mbele ya Muumba, mtu atabeba msalaba wake mwenyewe maana atahukumiwa yeye kutokana na matendo yake na si mwingine.

Hukumu niiongeleayo mimi ni hukumu inayotolewa na watu watuzungukao....ni hukumu ya jamii unayoishi. Hukumu hii haiandikiki na adhabu zake wala hazina mipaka...... kuanzia kuangaliwa kwa jicho baya, kufyonywa, mate kutemwa, kuzomewa, jina lako kuangazwa kwenye form zozote zile....n.k. Mambo kama haya yanaonekana madogo madogo na mtu unaweza ku-live with, but to tell the truth, ni hindrance kubwa sana kwa morale ya mtu hence his/her performance in daily activities, pale ambapo anaona anaonekana kero kwa wanajamii kwa kosa ambalo hajalifanya mwenyewe.

Mfano mkubwa: Ona jinsi Mugabe anavyo washutumu wazungu nchini mwake kwa makosa ya babu zao waliokuwa wakoloni..... je, unafikiri haya mambo yataishia kwa wazungu tu?! Je, unafikiri sheria za nchi zetu kuhusiana na mali zenye thamani kubwa ambazo ziko linked kwenye majina makubwa yaliyojihusisha na ufisadi zitaendelea kuwa hivi hivi hata baada ya miaka 25?.... hatujui mambo yatakuwaje huko mbeleni, ila kimoja kikubwa mtu unaweza kujua ni kuwa, kama hujihusishi na matendo ya kifisadi, huna cha kuogopa, kuanzia kwenye mali zako hadi kwenye usalama wa familia yako sasa na mbeleni...

Hao nin wachache tu lakini CCM hawana mshipa wa Noma .Wataiba nakujengea hoja .Muoneni Makamba kwa mfano ndipo mjue .Lakini we utu inakuwa kazi .Makelele yanamfanya hata Mkapa sasa hawezi kutembea kifua mbele anakimbia wananchi wenzake .Ndiyo tukaze buti hadi kieleweke .

Angalia sasa..... Mtu unafanya kazi kwa bidii kwa kipindi kikubwa cha maisha yako, halafu ghafla unajitokomeza kwenye vitendo vya kifisadi ambavyo vinakuchafulia historia yako yote na taswira nzima ya familia yako.... .what for?! Angalia Ndugu Balali..... mtu na phd yake, sasa hivi kokote aliko hawezi kwenda pahala kushiriki bila kusontwa..... uhuru gani huu jama? Couldn't they just retire and gather fruits of their hard labor?

Sasa hivi hata kuandika autobiograph ni vigumu kwao.... tamaa gani hizi zisizokipimo na zinazoonekana watu kama hawajasoma vile?! Ina kera..... Mbona akina Salim Ahamed Salim, Ustadhi Mwinyi na wachache wengineo bado wanapeta na kuheshimika sana katika jamii..... wanafikiri tutawasahau kama hawana pesa? NOoo! jamii itakujaji kutokana na matendo yako na siyo pesa zako? Hebu fikiria.... mtu unakuwa waziri mkuu au rais lakini bado unakuwa na tamaa.... ruzuku kibao ungepata baada ya kusitaaf, hekima za watu kutokana na uliyofanya kwa wananchi wako ni thawabu kubwa hapa duniani- kwako na kwa familia yako..... why tarnish it?!

SteveD.
 
Ok. jamani sasa ebu jiweweke, uvae viatu yaani uwe wewe ndo mtoto wa hao mafisadi. Je? Ungejitenga? Au ndo ungekuwa karibu na marafiki, hili usikie vizuri kinachoongelewa, hili ukamshauri mzazi wako.Japokuwa mzazi nae anweza kuwa mkali kwako. Kifupi kama mimi ningekuwa ni mmoja wa watoto wa mafisadi ningeumia sana, lakini nisingejitenga na marafiki zangu kwani, nikijitenga na marafiki halafu home unakuta kimya kama kuna msiba sasa ningekuwa mtu wa namna gani?
 
....., hili ukamshauri mzazi wako.Japokuwa mzazi nae anweza kuwa mkali kwako....

Imagine baba yako ni Mkapa, unafikiri atakusikiliza ukijaribu kumpa ushauri wowote? Hata kama ni simple logic ama common sense.... He'll just tell you LEAVE ME ALONE, I'M A RETIREE!!!!
 
SteveD na Nikifufuka. Natamani maneno yenu mazuri yaandikiwe makala nzuri na kuchapishwa kwenye gazeti kama Tanzania Daima au mwanahalisi au mwananchi ili wadau wengi zaidi waweze kuifaidi(hasa wasioweza tumia internet)
 
Hawa mafisadi wanafanya money laundering kwa kusomesha watoto wao jne ya Tanzania, unaweza kushangaa mkuu wam kijiji anamosomesha mtoto wake Marekani kwa mshahara huo huo anaopata, bila hata kuwa na biashara!!
 
Jamani hivi vituko vinatoka wapi, nchi yetu kama imeingiliwa na majinamizi vile, safari hii tena imekuwa Mh. Mkapa..... naye kashangiliwa na wananchi kijijini kwake katika harakati za kujiosha madhambi... hali sehemu ambapo anatumia muda mwingi kuendeshea shughuli zake na kuishi kila mmoja anamzomea au kumwangalia kwa jicho baya...

Je hili ni wimbi jipya la kurubuni wanavijiji wasamalia baada ya kujiharibia mambo mijini?!
 
Jamani hivi vituko vinatoka wapi, nchi yetu kama imeingiliwa na majinamizi vile, safari hii tena imekuwa Mh. Mkapa..... naye kashangiliwa na wananchi kijijini kwake katika harakati za kujiosha madhambi... hali sehemu ambapo anatumia muda mwingi kuendeshea shughuli zake na kuishi kila mmoja anamzomea au kumwangalia kwa jicho baya...

Je hili ni wimbi jipya la kurubuni wanavijiji wasamalia baada ya kujiharibia mambo mijini?!

Steve D washangaa?

Je ulikuwa hujui kuwa jamii nyingi za Kitanzania ambazo viongozi wetu na waliopata kuwa viongozi, wametokea huko, bado zinaamini katika mambo kama vile ya kupiga ramli, kuosha nyota au hata kufanya jambo baada ya kupata maelekezo ya wataalam a.k.a waganga.

Ukiangalia mwenendo mzima wa waliokumbwa na kashfa za ufisadi unaweza kukubaliana nami kuwa baada ya kukumbwa na kashfa huwa hawazijibu mpaka waende makwao ndipo wajibu.

Huko, licha ya kuwa ni remote, lakini hupata fursa nzuri ya kufanya matambiko kwa ajili ya kuuwa soo na wakisema watu wasicomment chochote.

Alianza Karamagi, akafanya ya kwake huko kwao, karudi roho ikiwa kwatuu!!

Kafuatia Fisadi EL, yeye nasikia kabla ya kwenda, alitanguliza timu ya wataalamu iliyokuwa na kazi ya kusafisha barabara kwa kufaya vituuuuzi. Akaongeza na media coverage ya nguvu. Naye alitoka huko akiwa roho kwatuuu!!!

Fisadi Vijisenti, ndiye aliyevunja record kwani kuanzia Mwanza airport mambo yalifanyika hadharani na ndani ya msafara wake, walikuwapo wataalam achilia mbali waliokuwa wakipika nyama ya ng'ombe waliolishwa wanavijiji.
 
Kama yote yaliyotokea Bungeni hivi karibuni yakimhusisha Ndugu Chenge na mambo ya kuonekana kwenye kamera ni ya kweli, basi nadhani aibu itakayo kuwa imejengeka kwa wanaukoo wote ni ya kiwango cha juu...unless, unless.... haya yote yawe si ya kweli.
 
Kama yote yaliyotokea Bungeni hivi karibuni yakimhusisha Ndugu Chenge na mambo ya kuonekana kwenye kamera ni ya kweli, basi nadhani aibu itakayo kuwa imejengeka kwa wanaukoo wote ni ya kiwango cha juu...unless, unless.... haya yote yawe si ya kweli.

You are very Right but that is life!In life there is also a hardtime.
 
Back
Top Bottom