Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,745
- 11,872
Kesi namba 456 (Jamhuri v Maxence Melo na mwenzake Micke William) ambapo Kampuni ya Oilcom iliandikwa katika mtandao wa JamiiForums ikidaiwa kukwepa kodi na kuchakachua mafuta bandarini Dar, imekwama tena kuendelea na utetezi, Septemba 24, 2019
Sababu iliyokwamisha kesi kuendelea ni kutokana na Wakili wa upande wa Jamhuri aliyekabidhiwa shauri hilo kushindwa kufika Mahakamani kutokana na kupata udhuru
Hakimu ameomba taratibu zote kukamilishwa ili mpaka Oktoba 15 kesi iwe imekwisha kwasababu imeshaenda kwa muda mrefu. Baada ya kusema hayo aliahirishwa kesi mpaka Oktoba 7
Kesi hii inasikilizwa chini ya Hakimu, Thomas Simba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Wakili Candid Nasua na upande wa utetezi uliwakilishwa na Wakili Peter Kibatala
Aidha, katika shauri hilo Washtakiwa wanatuhumiwa kutotoa ushirikiano kwa Polisi walipotakiwa kutoa taarifa za aliyeandika taarifa kuhusu Oilcom
zaidi, soma;
Sababu iliyokwamisha kesi kuendelea ni kutokana na Wakili wa upande wa Jamhuri aliyekabidhiwa shauri hilo kushindwa kufika Mahakamani kutokana na kupata udhuru
Hakimu ameomba taratibu zote kukamilishwa ili mpaka Oktoba 15 kesi iwe imekwisha kwasababu imeshaenda kwa muda mrefu. Baada ya kusema hayo aliahirishwa kesi mpaka Oktoba 7
Kesi hii inasikilizwa chini ya Hakimu, Thomas Simba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Wakili Candid Nasua na upande wa utetezi uliwakilishwa na Wakili Peter Kibatala
Aidha, katika shauri hilo Washtakiwa wanatuhumiwa kutotoa ushirikiano kwa Polisi walipotakiwa kutoa taarifa za aliyeandika taarifa kuhusu Oilcom
zaidi, soma;
Kesi namba 456: Jamhuri vs JamiiForums juu ya Oilcom na Uchakachuaji mafuta bandarini kufanyiwa marekebisho tena!
KISUTU, DAR: Kesi dhidi ya JamiiForums inayohusiana na Kampuni ya Oilcom na Uchakachuaji Mafuta imesogezwa mbele kupisha Jamhuri kufanya marekebisho ya Mashtaka kwa mara nyingine. Kesi hiyo sasa itatajwa tena Septemba 26, 2017. Ieleweke, hii itakuwa ni mara ya 3 kwa kesi hii kufanyiwa...
www.jamiiforums.com