Wakili Peter Madeleka: Mimi na mke wangu tulikamatwa na kushtakiwa kwa uhujumu uchumi, nitawashtaki

Hivi hawa watu wanaowakamata wenzao tena wazazi wote wawili wenye watoto wadogo Kwa kesi za kupikwa, ingekuwa wao wangejisikiaje?? Watoto wanateseka Kwa kukosa malezi bora kisa binadamu wenzako?? Huku watoto wao wakifurahia maisha. Kwanini watoto hao wasijekuwa kina Hamza baadae??? Nchi hii imejaa watu wabaya Sana. Mungu atawaadhibu Kwa kadri awezavyo.
Hao ni mashetani katika maumbile ya wanadamu. Hawana tafakari kama hiyo ya kwako juu watoto na haki za hao wanaowaonea. Hao kwa tafsiri sahihi ndiyo magaidi, maana dhamaira yao ni kuleta terror ili maovu yao yasihojiwe na yeyote.
 
Huyu wakili kufanya KAZI polisi na mke wake pia kua afisa wa uhamiaji lazima kuna mgongano wa kimaslahi maana chocho zote za kuwatetea wahamiaji haramu wanajua.

Kuna kitu kaficha
Hakuna cha kuficha. Kama angekuwa ametenda uovu, wasingemwachia.
 
fasiliteta
Umesema ukweli kabisa, inawezekana kuna kitu kaficha, wanasheria na wengi na mawakili wengi ujanjajanja ni mwingi sana!
Nilivyomsikia anasema kuna sehemu kuna mapungufu kwenye sheria, hivyo anatumia mapungufu hayo kuwatetea waalifu/wahamiaji haramu!
Umesoma lakini inaonekana umetoka zero.

Yeye ameishtaki Serikali kwa kumweka mahabusu bila hatia. Lakini ili atoke ilimlazimu akiri kosa na alipe milioni 2.

Kwa hiyo serikali ushahidi itakaoutumia dhidi yake ni kukiri kosa. Upenyo alionao ni kukiri kwake kosa kufutwe kwa sababu hakukufuata utaratibu. Kukiri kwake kosa kusipotambulika kwa vile hakukufuata utaratibu, basi sasa atakuwa na haki ya kulalamikia tendo la yeye kuwekwa mahabusu bila hatia, na baadaye kufutiwa mashtaka kwa kukosa ushahidi.
 
Nilikuwa namchukia magufuli tangu akiwa waziri nilikuwa haamini hakuwa kiongozi Bora.nilishangaa siku anateuliwa kuwa mgombea uraisi. Nilijua wengi wangehangaika na kutaabika sana kwakuwa chini yake
POLE SANA KAKA PETER MADELEKA.
HATA MM NILIAMUA KUACHA KAZI KWENYE UTUMISHI WA UMMA KWA SABABU YA MAGUFULI
Inaonekana watu mbalimbali walikuwa mahabusu kwa uonevu kutokana na Magufuli. Yeye tu kufariki tarehe 17 Machi, tarehe 30 Machi hiyo hiyo, akaachiwa.

Mwanadamu hufurahii kifo cha binadamu mwenzako, lakini kifo cha Magufuli kimewaokoa wengi kutoka kwenye mateso na dhuluma mbalimbali.
 
Nilikuwa namchukia magufuli tangu akiwa waziri nilikuwa haamini hakuwa kiongozi Bora.nilishangaa siku anateuliwa kuwa mgombea uraisi. Nilijua wengi wangehangaika na kutaabika sana kwakuwa chini yake
POLE SANA KAKA PETER MADELEKA.
HATA MM NILIAMUA KUACHA KAZI KWENYE UTUMISHI WA UMMA KWA SABABU YA MAGUFULI
Wewe ulikua mtumishi hewa ulifoji cheti huna lolote
 
Umesoma lakini inaonekana umetoka zero.

Yeye ameishtaki Serikali kwa kumweka mahabusu bila hatia. Lakini ili atoke ilimlazimu akiri kosa na alipe milioni 2.

Kwa hiyo serikali ushahidi itakaoutumia dhidi yake ni kukiri kosa. Upenyo alionao ni kukiri kwake kosa kufutwe kwa sababu hakukufuata utaratibu. Kukiri kwake kosa kusipotambulika kwa vile hakukufuata utaratibu, basi sasa atakuwa na haki ya kulalamikia tendo la yeye kuwekwa mahabusu bila hatia, na baadaye kufutiwa mashtaka kwa kukosa ushahidi.
Nashukuru kwa sifa uliyonipatia, ila uelewe hawa mawakili ni wajanjawajanja sana, kwani si amesema mwenyewe alikuwa anawatetea hata waharifu?
 
Kila mtu anamambo yake ambayo asingependa yajulikane, changamoto inakuja unafanya maovu ila unajificha kwenye mgongo wa siasa mwisho wa siku ukikamatwa unawapa wafuasi wako mwanya waitengeneze hiyo issue kuwa yakisiasa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwan wapi imesemwa ni issue ya kisiasa? Huyo kagusa maslahi ya watu wazito hasa huko uhamiaji.
 
Angenyamaza tuu.. ...

Watamuondoa ... ...

Haya sasa.. ...
Huyu jamaa anaongea sana na ukifuatilia sana utakuta kuna baadhi ya mambo anaforce sana.

Angepiga kimya tu. Kuna kitu alikua anakitafuta na kakipata.
 
21 April 2022

WAKILI WA PETER MADELEKA AIBUA MAZITO KINACHOENDELEA BAADA YA KUKAMATWA KWA WAKILI PETER MADELEKA



Source : Mubashara Studio
 
Back
Top Bottom