Wakili Mwale anena mazito juu ya kesi zinazomkabili

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
WASHITAKIWA kwenye shauri la utakasaji fedha linalomkabili wakili Maarufu jijini Arusha, Median Mwale na wenzake watatu wamesema wako ngangari kwa mapambano ya kisheria huku wakiwataka mawakili wa Serikali waache kukata rufaa kila wanapoona mambo hayaendi vizuri kwa upande wao.

Wamesema hayo leo mbele ya hakimu Mkazi Nestory Barro wa mahakama ya hakimu Mkazi Arusha baada ya wakili wa Serikali, Awamu Mbagwa kuiomba mahakama ihairishe shauri hilo mpaka kesho ili kutoa nafasi kwa ofisi ya msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kusajili maelezo ya kesi hiyo yatakayosomwa kwenye mahakama ya hiyo kabla ya shauri hilo kuhamia mahakama Kuu Kwa ajili ya kusikilizwa.

Wakili Mwale amesema mawakili wa Serikali wana tabia wakiona mambo yanaharibika wanakata rufaa jambo alilowataka waache kufanya hivyo ili kesi hiyo iiliyodumu kuanzia mwaka 2011 iweze kuendelea na kufikia mwisho.


"Tunaomba waharakishe, tuna kiu ya kupambana, tuko ngangari, tuko tayari wasicheleweshe. Mwale wametufundisha sheria sasa hivi tunajua sheria wasicheleweshe tuko tayari tumejiandaa na wao wajipange," alisema mshitakiwa Don Gichana.

Hakimu Barro aliwauliza washitakiwa hao kwa nini wanawahofia mawakili wa Serikali.

"Sisi hatuwahofii wao ndiyo wanatuhofia na tuko magereza tungekuwa uraiani sijui ingekuwaje, si wangepanda bombardier," alisema mshitakiwa Gichana huku wananchi na mawakili waliokuwa mahakamani hapo wakiangua vicheko.

Mawakili wa Serikali nhawakujibu chochote ambapo shauri hilo limeahirishwa mpaka kesho litakaporudi mahakamani hapo kwa washitakiwa kusomewa maelezo ya kesi.

Wakili Mwale, Gichana, Eliasi Ndejembi na Boniface Mwimbwa wanakabiiwa na mashitaka 42 tofauti ya kula njama, kutatisha fedha haramu, kugushi nyaraka na kukutwa na mali zilizopatikana kwa njia ya uhalifu.

Novemba mosi mwaka huu washitakiwa hao walisomewa mashitaka hayo ikiwa NI sijui moja baada ya kuachiwa na mahakama Kuu kutokana na upande wa jamhuri kuwasilisha hati ya Mkurugenzi wa mashitaka nchini, (DPP), ya kuliondoa shauri hilo kwani hana nia ya kuendelea nalo.

Mara baada ya kusomewa mashitaka hayo ambayo hawakutakiwa kuyakubali au kuyakana, Ndejembi alimuomba hakimu ampe ruhusa ya kusema jambo ambapo hakimu alimpa ruhusa.

"Mimi si mtaalam wa sheria lakini sarakasi zimeshaendelea mara nyingi ni bora waamue watufunge kuliko kuendelea kututesa magereza familia zetu zinateseka. Tuna taarifa umepandishwa cheo tunaomba utumie mamlaka yako kutufunga," alisisitiza mshitakiwa Ndejembi.

Wakili mwale aliunga mkono hoja ya mshitakiwa mwenzake huku akifananisha shauri hilo na timu za mpira za Simba na yanga huku alitokea mfano kuwa kila wanapoifunga yanga wanaibuka na sababu za kukataa ushindi wakitoa sababu zisizo na msingi kutaka mchezo uanze upya.

"Kesi imeanza mwaka 2011, kimsingi shitaka ni moja ila maelezo yanawekwa mengi, leo tunarudi kusomewa shitaka kwa mara ya nne, hata jana jaji, (David Mrango) wakati akitoa uamuzi wake aliwaambia kama mnafuta shitaka kuja kutunga ushahidi sitakubali lakini kama mnaifuta ili washitakiwa watoke gerezani nakubaliana na nyie washitakiwa wawe huru," alisema wakili Mwale.

Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa ni heri shauri hilo likasikilizwa kama wanafungwa ni sawa kuliko wanavyoendelea kusota magereza Kwa zaidi ya miaka sita sasa huku shauri likishindwa kumalizika huku akisisitiza kuwa haki inayocheleweshwa ni sawa na haki iliyopita.

Hata hivyo Wakili wa mkuu Serikali, Oswald Tibabyekomya, aliyekuwa mahakamani hapo siku hiyo akujibu hoja hizo.
 
WASHITAKIWA kwenye shauri la utakasaji fedha linalomkabili wakili Maarufu jijini Arusha, Median Mwale na wenzake watatu wamesema wako ngangari kwa mapambano ya kisheria huku wakiwataka mawakili wa Serikali waache kukata rufaa kila wanapoona mambo hayaendi vizuri kwa upande wao.

Wamesema hayo leo mbele ya hakimu Mkazi Nestory Barro wa mahakama ya hakimu Mkazi Arusha baada ya wakili wa Serikali, Awamu Mbagwa kuiomba mahakama ihairishe shauri hilo mpaka kesho ili kutoa nafasi kwa ofisi ya msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kusajili maelezo ya kesi hiyo yatakayosomwa kwenye mahakama ya hiyo kabla ya shauri hilo kuhamia mahakama Kuu Kwa ajili ya kusikilizwa.

Wakili Mwale amesema mawakili wa Serikali wana tabia wakiona mambo yanaharibika wanakata rufaa jambo alilowataka waache kufanya hivyo ili kesi hiyo iiliyodumu kuanzia mwaka 2011 iweze kuendelea na kufikia mwisho.


"Tunaomba waharakishe, tuna kiu ya kupambana, tuko ngangari, tuko tayari wasicheleweshe. Mwale wametufundisha sheria sasa hivi tunajua sheria wasicheleweshe tuko tayari tumejiandaa na wao wajipange," alisema mshitakiwa Don Gichana.

Hakimu Barro aliwauliza washitakiwa hao kwa nini wanawahofia mawakili wa Serikali.

"Sisi hatuwahofii wao ndiyo wanatuhofia na tuko magereza tungekuwa uraiani sijui ingekuwaje, si wangepanda bombardier," alisema mshitakiwa Gichana huku wananchi na mawakili waliokuwa mahakamani hapo wakiangua vicheko.

Mawakili wa Serikali nhawakujibu chochote ambapo shauri hilo limeahirishwa mpaka kesho litakaporudi mahakamani hapo kwa washitakiwa kusomewa maelezo ya kesi.

Wakili Mwale, Gichana, Eliasi Ndejembi na Boniface Mwimbwa wanakabiiwa na mashitaka 42 tofauti ya kula njama, kutatisha fedha haramu, kugushi nyaraka na kukutwa na mali zilizopatikana kwa njia ya uhalifu.

Novemba mosi mwaka huu washitakiwa hao walisomewa mashitaka hayo ikiwa NI sijui moja baada ya kuachiwa na mahakama Kuu kutokana na upande wa jamhuri kuwasilisha hati ya Mkurugenzi wa mashitaka nchini, (DPP), ya kuliondoa shauri hilo kwani hana nia ya kuendelea nalo.

Mara baada ya kusomewa mashitaka hayo ambayo hawakutakiwa kuyakubali au kuyakana, Ndejembi alimuomba hakimu ampe ruhusa ya kusema jambo ambapo hakimu alimpa ruhusa.

"Mimi si mtaalam wa sheria lakini sarakasi zimeshaendelea mara nyingi ni bora waamue watufunge kuliko kuendelea kututesa magereza familia zetu zinateseka. Tuna taarifa umepandishwa cheo tunaomba utumie mamlaka yako kutufunga," alisisitiza mshitakiwa Ndejembi.

Wakili mwale aliunga mkono hoja ya mshitakiwa mwenzake huku akifananisha shauri hilo na timu za mpira za Simba na yanga huku alitokea mfano kuwa kila wanapoifunga yanga wanaibuka na sababu za kukataa ushindi wakitoa sababu zisizo na msingi kutaka mchezo uanze upya.

"Kesi imeanza mwaka 2011, kimsingi shitaka ni moja ila maelezo yanawekwa mengi, leo tunarudi kusomewa shitaka kwa mara ya nne, hata jana jaji, (David Mrango) wakati akitoa uamuzi wake aliwaambia kama mnafuta shitaka kuja kutunga ushahidi sitakubali lakini kama mnaifuta ili washitakiwa watoke gerezani nakubaliana na nyie washitakiwa wawe huru," alisema wakili Mwale.

Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa ni heri shauri hilo likasikilizwa kama wanafungwa ni sawa kuliko wanavyoendelea kusota magereza Kwa zaidi ya miaka sita sasa huku shauri likishindwa kumalizika huku akisisitiza kuwa haki inayocheleweshwa ni sawa na haki iliyopita.

Hata hivyo Wakili wa mkuu Serikali, Oswald Tibabyekomya, aliyekuwa mahakamani hapo siku hiyo akujibu hoja hizo.
Vp mkuu lete updates basi
 
Back
Top Bottom