Wakili Jebra Kambole: Mtu Mzalendo ni yule anayependa Nchi yake na siyo Serikali yake

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899


Mtu ambaye ni mzalendo ni yule anayeipenda Nchi yake na sio serikali yake! Wakoloni walikuwa wanaserikali ulitaka wapendwe? Makaburu wa South Africa walikuwa wanaserikali ulitaka wapendwe, Mobutu, Idd Amin, Hitler wote walikuwa na serikali ulitaka wapendwe ?
 
Sasa ukienda huko duniani kushawishi waache kushirikiana na nchi unakomoa serikali?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani kasema wasishirikiane na nchi? Tunataka wasishirikiane na serikali dhalimu inayo tupia watu wanaoikosoa kwenye tundu la chatu. Hivi kijana wangu Wakudadavuwa unadhani kesho na kesho kutwa ukibadilika utawala basi ajaye akisema wale manaibu waziri wote tupia kwenye tundu la chatu au weka kwenye viroba na tupa baharini itakuwa ni sawa?
Hakika hiyo serikali hata Rais awe Mbowe, Lissu au Kadinali Pengo tutaipinga wote. Kwa nini nyie mnaunga mkono unyama huu?
 
Nani kasema wasishirikiane na nchi? Tunataka wasishirikiane na serikali dhalimu inayo tupia watu wanaoikosoa kwenye tundu la chatu. Hivi kijana wangu Wakudadavuwa unadhani kesho na kesho kutwa ukibadilika utawala basi ajaye akisema wale manaibu waziri wote tupia kwenye tundu la chatu au weka kwenye viroba na tupa baharini itakuwa ni sawa?
Hakika hiyo serikali hata Rais awe Mbowe, Lissu au Kadinali Pengo tutaipinga wote. Kwa nini nyie mnaunga mkono unyama huu?
Kama hataelewa atakua na ajenda yake nyingne

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi kulipenda Taifa lako bila kuipenda serikali yako,sababu Taifa ndio linakuwa limeichagua serikali iliyoko madarakani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kila serikali iliyoko madarakani imechaguliwa na wananchi. Kuna serikali zingine huchukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi. Serikali kama hiyo na zingine zenye kufanana na hiyo hazifai kupendwa kabisa.
 
Kwasasa hatuendi na Membe 2020,chadema raha sana. Ahahahaaaa. Sijui nani atafuata baada ya Lissu.

always positive
 
Huwezi kulipenda Taifa lako bila kuipenda serikali yako,sababu Taifa ndio linakuwa limeichagua serikali iliyoko madarakani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umesikia wapi ni halali serikali inaona fahari kuua watu wake holela kama kweli unamaanisha kwamba Taifa ndio watu wanaoichagua serikali hiyo? Akili yako ni mgoroko kweli. Majina huumba uhalisia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom