Wakili Albert Msando amepotosha umma kwa kudai CAG hana kinga ya kutohojiwa na Kamati ya Bunge

Mtu akishakuwa ccm tayari anakuwa na low IQ..so msando kwa sasa sio wakili msomi bali wakili tumbo

MTATIRO naye kajichimbia kaburi..nyota yake kwa sasa ishafifia..toka ahamie ccm amekuwa kama kuku alinyolewa manyoa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanasheria wa Tanzania wengine ni kama wachekeshaji. Wanajidanganya wanachojua wao ndio sahihi kabisa eti kwa kusoma mstari mmoja wa sentensi
Hakuna mamlaka yasiyo na wajibu. CAG kwenda nje na kusema vile hata kama yuko sahihi, platform aliyotoa maneno yake sio sahihi.
Amekosea sana
 
Amani iwe kwenu Wadau.

Kwanza napenda kuwasalimu na kuwaomba radhi kwa kipindi chote ambacho sijaonekana katika jukwaa hili.

Nimekuwa kimya kwa kipindi nikifutilia mijadala mbalimbali kwenye jukwaa hili huku nikitafakari kwa kina ni kwa jinsi gani jukwaa hili linatoa mchango chanya katika ukuaji wa nchi yetu kwenye Nyanja zote.

Niliamua kuwa msomaji tu na sio mchangiaji ila hili alilolipost Wakili Msando leo limenifanya nirudi haraka na mie nitumie mchango wangu katika kuuelewesha umma wa watanzania katika mambo ya msingi ya kisheria kwa sababu nikikaa kimya umma wa watanzania utalishwa matango pori na watu wanajiita kuwa wanasheria ila wanapotosha kwa makusudi kwa sababu zao binafsi.

Albert Msando amepotosha umma kwa kiwango kikubwa sana kwa kusema kuwa CAG HANA kinga ya kutohojiwa na kamati ya Bunge kwa kauli inayosemekana ya kulidhalilisha Bunge. Napenda kusema kuwa Msando amekosea sana na anastahili kuiomba radhi tasnia ya sheria kwa upotoshaji huu uliotukuka.

Katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 kati ya nafasi ambazo zimelindwa na zimewekwa kuwa nyeti mojawapo ni nafasi za Jaji( Mahakama kuu na Mahakama ya rufaa) pamoja na CAG. Watu hawa wamewekewa utaratibu maalumu wa kuwawajibisha endapo watafanya makosa yeyote yale iwe wao kama wao au wao kama taasisi na Katiba ya Tanzania haikuacha mwanya wowote katika hayo.

CAG wa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 ibara za 143 na 144 ana njia mbili tu za kumuwajibisha nazo ni
  • MAHAKAMA
  • KAMATI/TUME MAALUM YA MAJAJI AMBAYO LAZIMA IJUMUISHE MAJAJI KUTOKA JUMUIYA YA MADOLA
Katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania haijasema popote pale kuwa kamati ya Bunge inaweza kumuhoji CAG kwa iyo jibu kama kamati ya Bunge ina mamlaka ni HAPANA HAINA MAMLAKA HAYO.

Mussa Assad alikuwa nchini Marekani kama CAG akiwakilisha Tanzania kama CAG ana hata pale alikuwa akihojiwa kama CAG wa Tanzania kuhusu utengaji wake wa kazi za U CAG wa Tanzania. Kama kuna kosa limefanywa pale taratibu za kumshughulikia ni za njia mbili tu yaaani ni kwa Mahakama au Tume maalumu ya Majaji ambayo lazima ijumuishe majaji/ jaji kutoka nchi za jumuiya ya Madola.

Naomba Msando usitumike katika kupotosha juu ya hili na napenda sote tukumbuke jambo hili linahusu katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo ndo inayotuongoza sote.

Ingawa Katiba ya Jamhuri ya muungazo ya 1977 ina mapungufu mengi na wengine kudai imepitwa na wakati lakini pia ina mambo mazuri mengi sana yakiwemo haya ya kulinda taasisi ya Mahakama/Majaji na taasisi/nafasi ya CAG.

Asanteni.

Huu Uzi wako ungekuwa mtamu zaidi kama ungekuja na ' Verified User Name ' yako kwani uliyemtuhumu wengi tunamjua ila Wewe hatukujui hivyo unakuwa humtendei haki.
 
Kinga alizo nazo CAG ni katika kutimiza majukum yake ya uCAG tu,Hakuna sehem speaker atamwita CAG kuhusiana na mambo ya Auditing kuwa yamekosewa, amechelewa kutoa au kashindwa kutimiza jambo lolote katika kazi yake. Hapa speaker hana Nguvu yyt ya kumhoji CAG. Mfano hata kwa Makonda speaker asingekuwa na mamlaka yyt ya kumwita makonda kwa makosa ya utekelezaji wa majukum yake ya uRC. Makonda hata awe anachelewa kuingia ofisini, anatukana watu au anafanya mambo yyt kinyume na maadili bado bunge halina haki ya kumhoji. Makonda na CAG waliitwa na Bunge kwa kosa moja tu,KUDHARAU BUNGE. Hapa huna cha nilikua kwenye majukum yangu au nilikua wapi,Swala ni umedharau Mhimili wa Bunge na Bunge haliwez kukupa adhabu yyt nje ya onyo na kama ni kutaka ufukuzwe kazi ni wao kuwasiliana na Mhimili uliokupa ajira ambao ni Serikali. Bunge likiona makosa yako ni makubwa na hayabebeki wao ni kutoa maazimio kwenda kwa serikali na Mwisho serikali itatakiwa kutoa uamuzi juu ya jambo hilo.CAG na ofisi yake sio muhimil unaojitegemea,Huu uko chini ya serikali na kinga alizo nazo ni ktk kutimiza majukum yake ya uCAG na sio nje ya Hapo.Kama kulidharrsha bunge ni sehemu ya kazi za CAG basi hakuna shida.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Unachokiandika hata wewe mwenye hukielewi.

CAG ameulizwa swali according to his findings, finding ambazo zimepatikana baada yakufanya kazi yake, kazi yake yenywe ni ya-U-CAG. Sasa unaweza kutofautisha vipi maoni ya CAG binafsi na maona ya CAG as CAG?? Shida ya Ma-CCM unyumbu unawasumbua, akili zote hazipo hata kwenye mambo yanayoitaji akili ya kawaida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unamaanisha anaitwa kama mtanzania wa kawaida alietoa maoni yabayodhaniwa kulidharau bunge,kwa hiyo wataitwa wangapi au hili ni mahsusi na halitatokea kwa mwingine
Kinga alizo nazo CAG ni katika kutimiza majukum yake ya uCAG tu,Hakuna sehem speaker atamwita CAG kuhusiana na mambo ya Auditing kuwa yamekosewa, amechelewa kutoa au kashindwa kutimiza jambo lolote katika kazi yake. Hapa speaker hana Nguvu yyt ya kumhoji CAG. Mfano hata kwa Makonda speaker asingekuwa na mamlaka yyt ya kumwita makonda kwa makosa ya utekelezaji wa majukum yake ya uRC. Makonda hata awe anachelewa kuingia ofisini, anatukana watu au anafanya mambo yyt kinyume na maadili bado bunge halina haki ya kumhoji. Makonda na CAG waliitwa na Bunge kwa kosa moja tu,KUDHARAU BUNGE. Hapa huna cha nilikua kwenye majukum yangu au nilikua wapi,Swala ni umedharau Mhimili wa Bunge na Bunge haliwez kukupa adhabu yyt nje ya onyo na kama ni kutaka ufukuzwe kazi ni wao kuwasiliana na Mhimili uliokupa ajira ambao ni Serikali. Bunge likiona makosa yako ni makubwa na hayabebeki wao ni kutoa maazimio kwenda kwa serikali na Mwisho serikali itatakiwa kutoa uamuzi juu ya jambo hilo.CAG na ofisi yake sio muhimil unaojitegemea,Huu uko chini ya serikali na kinga alizo nazo ni ktk kutimiza majukum yake ya uCAG na sio nje ya Hapo.Kama kulidharrsha bunge ni sehemu ya kazi za CAG basi hakuna shida.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
Majukumu ya CAG yanapatikana katika Ibara ya 143 (2) (3) , (4) ya katiba, pia kifungu cha 11 na 12 cha Public Audit Act, 2008 ;

Kutoa maoni ya Taasisi anazofanya nazo kazi sio sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake kwani majukumu yake ya msingi yamekwisha ainishwa hapo juu ambapo kitendo hicho hakifanyi sehemu ya majukumu hayo.

Kwa ujumla wake tungependa kuiona comment yake wazi wazi katika ripoti zake na sio katika vyombo vya habari vya nje.
Profesa amewavuruga na mmepata stroke kweli kweli...!!!
Msema Kweli ni Mupenzi wa Mungu, ila kuna watu wakiambiwa ukweli wana-jam mioyoni
 
Tatizo linakuja kwenye separation ya “majukumu ya CAG”. Wakati anajibu lile swali, alikuwa ameulizwa yeye kama CAG. Ni rahisi kusema alikuwa akifanya kazi yake. Tafsiri ya kusema maneno yale ni kulidhalilisha Bunge ni subjective na CAG anaweza kugoma kuitikia wito na kama vipi Speaker aende Mahakamani kupata tafsiri sahihi
 
Unamaanisha anaitwa kama mtanzania wa kawaida alietoa maoni yabayodhaniwa kulidharau bunge,kwa hiyo wataitwa wangapi au hili ni mahsusi na halitatokea kwa mwingine
Hapo sasa! Manake kwa hili ingebidi orodha ya wanaoitwa na bunge iwe ndefu sana, nafikiri hata nafasi ya kufanya kazi nyingine ingekosekana! Bila ya yeye kuwa CAG katu asingeitwa. Nashidwa kuelewa hawa wanaodai kaitwa kama yeye. Unaachanisha vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amani iwe kwenu Wadau.

Kwanza napenda kuwasalimu na kuwaomba radhi kwa kipindi chote ambacho sijaonekana katika jukwaa hili.

Nimekuwa kimya kwa kipindi nikifutilia mijadala mbalimbali kwenye jukwaa hili huku nikitafakari kwa kina ni kwa jinsi gani jukwaa hili linatoa mchango chanya katika ukuaji wa nchi yetu kwenye Nyanja zote.

Niliamua kuwa msomaji tu na sio mchangiaji ila hili alilolipost Wakili Msando leo limenifanya nirudi haraka na mie nitumie mchango wangu katika kuuelewesha umma wa watanzania katika mambo ya msingi ya kisheria kwa sababu nikikaa kimya umma wa watanzania utalishwa matango pori na watu wanajiita kuwa wanasheria ila wanapotosha kwa makusudi kwa sababu zao binafsi.

Albert Msando amepotosha umma kwa kiwango kikubwa sana kwa kusema kuwa CAG HANA kinga ya kutohojiwa na kamati ya Bunge kwa kauli inayosemekana ya kulidhalilisha Bunge. Napenda kusema kuwa Msando amekosea sana na anastahili kuiomba radhi tasnia ya sheria kwa upotoshaji huu uliotukuka.

Katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 kati ya nafasi ambazo zimelindwa na zimewekwa kuwa nyeti mojawapo ni nafasi za Jaji( Mahakama kuu na Mahakama ya rufaa) pamoja na CAG. Watu hawa wamewekewa utaratibu maalumu wa kuwawajibisha endapo watafanya makosa yeyote yale iwe wao kama wao au wao kama taasisi na Katiba ya Tanzania haikuacha mwanya wowote katika hayo.

CAG wa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 ibara za 143 na 144 ana njia mbili tu za kumuwajibisha nazo ni
  • MAHAKAMA
  • KAMATI/TUME MAALUM YA MAJAJI AMBAYO LAZIMA IJUMUISHE MAJAJI KUTOKA JUMUIYA YA MADOLA
Katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania haijasema popote pale kuwa kamati ya Bunge inaweza kumuhoji CAG kwa iyo jibu kama kamati ya Bunge ina mamlaka ni HAPANA HAINA MAMLAKA HAYO.

Mussa Assad alikuwa nchini Marekani kama CAG akiwakilisha Tanzania kama CAG ana hata pale alikuwa akihojiwa kama CAG wa Tanzania kuhusu utengaji wake wa kazi za U CAG wa Tanzania. Kama kuna kosa limefanywa pale taratibu za kumshughulikia ni za njia mbili tu yaaani ni kwa Mahakama au Tume maalumu ya Majaji ambayo lazima ijumuishe majaji/ jaji kutoka nchi za jumuiya ya Madola.

Naomba Msando usitumike katika kupotosha juu ya hili na napenda sote tukumbuke jambo hili linahusu katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo ndo inayotuongoza sote.

Ingawa Katiba ya Jamhuri ya muungazo ya 1977 ina mapungufu mengi na wengine kudai imepitwa na wakati lakini pia ina mambo mazuri mengi sana yakiwemo haya ya kulinda taasisi ya Mahakama/Majaji na taasisi/nafasi ya CAG.

Asanteni.
Wee, usipotoshe kabisa! Acha mtu atiwe adabu. Kinga aliyonayo ni ya kazi yake ya Auditing, Basi! Leo hii akinitukana, akibaka mwanao, akiiba pesa za jirani, nk. atatiwa adabu tu! Kinachotafutwa hapa siyo makosa ya kiuwajibikaji, ni makosa ya kibinadamu yaliyotoka nje ya kazi yake ya auditing. Bunge halimuiti kwa kutoa ripoti mbaya au nzuri au nini ndani ya kazi yake, linamuita kwa kuingilia utendaji wa Bunge, basi! Kinga ya nini??
 
Kama maelezo yote yale bado hujaelewa basi kuna walakini ktk uwezo wako wa kuchanganua Mambo. Hicho kifungu kiko wazi kabisa,kinaelezea majukum yake. Au hujui kusoma?Rais hakuna popote pale anaweza shtakiwa au hojiwa kwa jambo lolote lile analofanya hii ni katiba. Kasome vizur katiba uone kama kinga ya Rais na CAG ziko sawa.Pili umekuja na mfano mbovu kabisa wa kuita wanafunzi vilaza, Sasa wanafunzi ni wabunge au ni Bunge?Tuseme Rais asingekuwa na kinga ya kuhojiwa bado kuna tume ya utumishi wa umma inayosimamia maadili na huko ndio angepelekwa kuhojiwa na sio Bungeni. Hao wote wameitwa kuhojiwa kwa kosa la kudharau bunge sio kwa makosa ya utekelezaji wa majukum yao.CAG hana kinga yyt juu ya makosa nje ya kazi zake. CAG akipiga mtu lzm ashitakiwe, lkn Rais akipiga mtu hakuna popote pa kumshtaki. So kinga ya CAG msiikweze sana na amepewa hiyo kinga kutokana na unyeti wa kazi zake ambapo inahitaji umakini mkubwa sana bila kusumbuliwa na yyt.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
umeulizwa Rais kuita wale watoto wetu UDOM vilaza pia ni kazi ya rais??

Assad alikua USA km CAG wa 🇹🇿 Tanzania na alihojiwa km CAG, swali linakuja ni majibu gani akiyatoa anakua hajayatoa CAG, na yapi anakua anayajibu km CAG??
 
Amani iwe kwenu Wadau.

Kwanza napenda kuwasalimu na kuwaomba radhi kwa kipindi chote ambacho sijaonekana katika jukwaa hili.

Nimekuwa kimya kwa kipindi nikifutilia mijadala mbalimbali kwenye jukwaa hili huku nikitafakari kwa kina ni kwa jinsi gani jukwaa hili linatoa mchango chanya katika ukuaji wa nchi yetu kwenye Nyanja zote.

Niliamua kuwa msomaji tu na sio mchangiaji ila hili alilolipost Wakili Msando leo limenifanya nirudi haraka na mie nitumie mchango wangu katika kuuelewesha umma wa watanzania katika mambo ya msingi ya kisheria kwa sababu nikikaa kimya umma wa watanzania utalishwa matango pori na watu wanajiita kuwa wanasheria ila wanapotosha kwa makusudi kwa sababu zao binafsi.

Albert Msando amepotosha umma kwa kiwango kikubwa sana kwa kusema kuwa CAG HANA kinga ya kutohojiwa na kamati ya Bunge kwa kauli inayosemekana ya kulidhalilisha Bunge. Napenda kusema kuwa Msando amekosea sana na anastahili kuiomba radhi tasnia ya sheria kwa upotoshaji huu uliotukuka.

Katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 kati ya nafasi ambazo zimelindwa na zimewekwa kuwa nyeti mojawapo ni nafasi za Jaji( Mahakama kuu na Mahakama ya rufaa) pamoja na CAG. Watu hawa wamewekewa utaratibu maalumu wa kuwawajibisha endapo watafanya makosa yeyote yale iwe wao kama wao au wao kama taasisi na Katiba ya Tanzania haikuacha mwanya wowote katika hayo.

CAG wa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Tanzania ya mwaka 1977 ibara za 143 na 144 ana njia mbili tu za kumuwajibisha nazo ni
  • MAHAKAMA
  • KAMATI/TUME MAALUM YA MAJAJI AMBAYO LAZIMA IJUMUISHE MAJAJI KUTOKA JUMUIYA YA MADOLA
Katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania haijasema popote pale kuwa kamati ya Bunge inaweza kumuhoji CAG kwa iyo jibu kama kamati ya Bunge ina mamlaka ni HAPANA HAINA MAMLAKA HAYO.

Mussa Assad alikuwa nchini Marekani kama CAG akiwakilisha Tanzania kama CAG ana hata pale alikuwa akihojiwa kama CAG wa Tanzania kuhusu utengaji wake wa kazi za U CAG wa Tanzania. Kama kuna kosa limefanywa pale taratibu za kumshughulikia ni za njia mbili tu yaaani ni kwa Mahakama au Tume maalumu ya Majaji ambayo lazima ijumuishe majaji/ jaji kutoka nchi za jumuiya ya Madola.

Naomba Msando usitumike katika kupotosha juu ya hili na napenda sote tukumbuke jambo hili linahusu katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo ndo inayotuongoza sote.

Ingawa Katiba ya Jamhuri ya muungazo ya 1977 ina mapungufu mengi na wengine kudai imepitwa na wakati lakini pia ina mambo mazuri mengi sana yakiwemo haya ya kulinda taasisi ya Mahakama/Majaji na taasisi/nafasi ya CAG.

Asanteni.
Kiongozi labda hukumwelewa
 
Kinga alizo nazo CAG ni katika kutimiza majukum yake ya uCAG tu,Hakuna sehem speaker atamwita CAG kuhusiana na mambo ya Auditing kuwa yamekosewa, amechelewa kutoa au kashindwa kutimiza jambo lolote katika kazi yake. Hapa speaker hana Nguvu yyt ya kumhoji CAG. Mfano hata kwa Makonda speaker asingekuwa na mamlaka yyt ya kumwita makonda kwa makosa ya utekelezaji wa majukum yake ya uRC. Makonda hata awe anachelewa kuingia ofisini, anatukana watu au anafanya mambo yyt kinyume na maadili bado bunge halina haki ya kumhoji. Makonda na CAG waliitwa na Bunge kwa kosa moja tu,KUDHARAU BUNGE. Hapa huna cha nilikua kwenye majukum yangu au nilikua wapi,Swala ni umedharau Mhimili wa Bunge na Bunge haliwez kukupa adhabu yyt nje ya onyo na kama ni kutaka ufukuzwe kazi ni wao kuwasiliana na Mhimili uliokupa ajira ambao ni Serikali. Bunge likiona makosa yako ni makubwa na hayabebeki wao ni kutoa maazimio kwenda kwa serikali na Mwisho serikali itatakiwa kutoa uamuzi juu ya jambo hilo.CAG na ofisi yake sio muhimil unaojitegemea,Huu uko chini ya serikali na kinga alizo nazo ni ktk kutimiza majukum yake ya uCAG na sio nje ya Hapo.Kama kulidharrsha bunge ni sehemu ya kazi za CAG basi hakuna shida.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Mkuu, umetuelewesha vizuri sana.
 
Kasome Sheria za maadili ya viongoz. Sijui kazi unayofanya na elimu yako,lkn kwa Mimi niliyesoma ETHICS za Uongozi ni kosa kubwa sana kutaja UDHAIFU au kukashifu kiongoz mwenzio hadharani hata kama ni ukweli kias gani. Mkuu wa Shule Huwez simama assemble na kusema mwalimu flani hufundishi vizur na ndio maana watoto wanafeli. Unaweza kuwa sahihi kabisa kwa kauli yako lkn kimaadili ya utumishi wa umma ni kosa kubwa ambalo kama litafika sehem husika unaweza fukuzwa kazi. CAG ni mtumishi wa umma na kuna fomu ya maadili ya viongoz kajaza inasema nini kuhusu kuheshimu viongoz au taasisi unayoshirikiana nayo kufanya kazi?Na utaona kesi ya CAG haimamriwi na mahakama bali na kamati ya maadili. CAG akiiba kwanza anapelekwa kamati ya maadili na Mwisho mahakaman. Kusema Dhaifu sio kosa la jinai na ni kweli bunge ni dhaifu lkn ndio maadili ya viongoz au watumishi wa umma?

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Mkuu, Asante kwa nondo!
 
Manguli wa sheria mllioko kwenye hii siredi niwaulize hivi inawezekana kulidhalilisha Bunge ni kazi ya CAG kisheria? Maana watetezi wake wanasema alikuwa UNO kikazi na mahojiano aliyafanya kama sehemu ya majukumu yake ya kiofisi.
 
Back
Top Bottom