Wakili afungua kesi kupinga polisi kuajiri wachina kwenye jeshi la polisi

moyafricatz

JF-Expert Member
Nov 27, 2015
2,900
4,865
Wakili mmoja nchini Zambia Bw.Dickson Jere amefungua kesi ya kikatiba kwenye mahakama kuu ya nchi hiyo, kupinga polisi nchini humo kuajiri raia wa Kichina katika jeshi hilo.

Hivi karibuni jeshi la polisi nchini Zambia limeajiri raia nane (8) wa Kichina na kuteua wawili kati yao kushika vyeo vya juu, ambao ni Mkuu wa Kamandi ya Polisi wa akiba, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP.Zhang Ming, na Msaidizi wake, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP.Wu Ming.

Maofisa hao wapya 8 waliapishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini humo, Inspekta Jenerali Kakoma Kanganji, ambapo pia alipokea magari 10 yaliyotolewa na serikali ya China kama msaada kwa jeshi hilo.

Wakili Jere amesema kitendo kilichofanywa na jeshi la polisi nchini Zambia ni cha aibu na ni kinyume na katiba. IGP Kanganji alijitetea kuwa maofisa wote 8 walioajiriwa ni raia wa Zambia pia kwa sababu wana uraia pacha (wa Zambia na China).
_
Hata hivyo Wakili Jere ametaja ibara ya 194 (a) ya Katiba ya nchi hiyo kuwa hairuhusu raia yeyote wa Zambia mwenye uraia wa nchi nyingine (uraia pacha) kuajiriwa katika nafasi yeyote kwenye majeshi. "Mtu mwenye uraia pacha anaweza kuajiriwa katika idara nyingine za serikali lakini si kwenye majeshi. Polisi wamevunja katiba" amesema Jere.

Hivi karibuni serikali ya China ilitangaza kuutaifisha uwanja wa ndege wa Keneth Kaunda mjini Lusaka, siku chache zilizopita, ili kufidia deni ambalo Zambia imeshindwa kulilipa kwa muda mrefu.

Nchini Afrika Kusini raia wa kichina Bi.Jianling Wu aligombea udiwani katika kata namba 118 jijini Johannesburg, kupitia chama cha ANC.

Wimbi la raia wa Kichina kuingia katika nchi za Afrika na kupewa nafasi vyeo mbalimbali limeibua wasiwasi kwa baadhi ya wananchi wakidai China ndiye mkoloni mpya barani Afrika, kutokana na nchi nyingi za Kiafrika kudaiwa madeni makubwa na China yasiyolipika.

Nini maoni yako?
IMG_20180920_112032.jpeg
 
baada ya kupata Uhuru nchi nying za Africa zilikuwa znatawaliwa na ukoloni mamboleo lakin sasa ni Kama ukoloni rasmi umeingia China analitawala bara LA Africa directly
 
Dooh afadhali wakili...apambane kuondoa hiyo aibu.....rais wa Zambia sijui analichukuliaje hili swala.....lkn pia natambua toka soko la shaba liyumbe duniani..... Zambia wapo taabani sana kifedha.....maana wao ndio walikuwa wauzaji wakubwa wa shaba kwenye soko la dunia.....
 
baada ya kupata Uhuru nchi nying za Africa zilikuwa znatawaliwa na ukoloni mamboleo lakin sasa ni Kama ukoloni rasmi umeingia China analitawala bara LA Africa directly
Nafikiri zianzishwe sera za kupinga ....aina mpya ya ukoloni ambayo china anataka kuifanyia Africa kupitia mikopo yake ya ajabu kabla haijawa too late....kama viongozi wetu hawataweza...basi wananchi wenyewe waanzishe...hizo movement
 
Nafikiri zianzishwe sera za kupinga ....aina mpya ya ukoloni ambayo china anataka kuifanyia Africa kupitia mikopo yake ya ajabu kabla haijawa too late....kama viongozi wetu hawataweza...basi wananchi wenyewe waanzishe...hizo movement
China yuko kimaslahi hilo linajulikana lakin bara LA Africa sjui tulirogwaje yan china anacheza na akili zetu tumetulia tu
 
Zambia imeshatekwa na Wachina. Hii ya kupenda misaada bwerere matokeo yake ndo hayo
 
Hapana Hawa wachina n Kama cancer Kwa bara LA Africa wanatutafuna taratibu hadi watumalize
Mkuu asa tufanyeje Tilampu badala yakusaidia Africa akasema "Shithole Africa" Europe nao wapobize kuimalisha jesh la mipakan kutuzuia tusiingie....ukisema tubak Africa Watukufu ndo kwanza wanatuminya kimbilio lililo baki ni mchina ""An Afrika mbombo ngafu
 
wachina wanatutafuna taratibu hadi watumalize tubaki mifupa tu
Hhhhhh!!! hio tunaita fall of USA colonization in Africa anda rise of Chinese colonization....tena USA kapoteza mpira(Afrika) umempata adui mchina....na mchina akicheza vibaya mjapan atauchukua mpira(Africa)... Europe kw sasa ni mashabik kwan walshatolewaga kweny hatua za makundi....Afrika tnatabu sana tukubal tukatae kutawaliw is an inevitable
 
"Kiujumla kujitawal wenyew tumeshndwa...wametuacha tujitawale ila Watakatifu wetu wamejipeleka wenyew kuomba kutawaliwa"
 
Tumelaaniwa saana Ngozi nyeusi
;) Saa zngine naungana na Eurocentric views kuwa Afrika haikua na maendeleo kabla ya ukolono""uthibitisho Wahadzabe+Bushmen's ad leo they done Nuttin which is refers as development kaz ni kuwinda na kutafuta matunda+miziz cku imeenda...
 
Back
Top Bottom