Wakili Mediam Mwale adaiwa kukutwa na TZS 18 bilioni haramu

Dr wa ukweli

JF-Expert Member
Feb 28, 2011
900
264
WAKILI maarufu nchini, Mediam Mwale aliyekuwa akishikiliwa na polisi tangu Agosti 2, mwaka huu, jana alifikishwa mahakamani akidaiwa kukutwa na fedha haramu zaidi ya Sh18 bilioni.

Mwale alifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Arusha, Charles Magesa ambaye hata hivyo, alikataa kupokea hati ya mashtaka baada ya kugundua makosa ya kisheria.

Wakili huyo anakabiliwa na mashtaka 13 ambayo Hakimu Magesa alisema shtaka la tatu hadi 13 hayaonyeshi ushiriki wa moja kwa moja iwapo mshtakiwa alilipwa au alipata fedha kupitia kampuni, taasisi au shirika kutokana na hati hiyo kutofafanua jambo hilo.

Mashtaka dhidi ya wakili huyo yalisomwa na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Velitasi Mlau aliyedai kuwa hati hiyo imekamilika na inajitosheleza ndiyo maana imewasilishwa mbele ya mahakama.

Wakili wa utetezi, Loomu Ojare alipinga hoja ya wakili huyo wa Serikali akitaka upande wa mashtaka kujipanga upya na kueleza tuhuma zinazomkabili mteja wake, idadi yake na aina ya tukio badala ya kuwasilisha mashtaka ya jumla yasiyojitosheleza kisheria.

Hakimu Magesa alikubaliana na kosa la kwanza hadi la tatu na aliahirisha kesi hiyo kwa kuuagiza upande wa mashtaka kurekebisha hati hiyo na kuirejesha mahakamani ikionyesha kwa usahihi kampuni iliyompa fedha wakili huyo.

Kutokana na uamuzi huo, Wakili Mwale alirejeshwa mikononi mwa jeshi la polisi wakati upande wa mashtaka wakitekeleza amri ya kurekebisha hati ya mashtaka kabla ya kuirejesha upya mahakamani.


Chanzo: Mwananchi
 
Habari ndio hiyo mkuu,....nchi imewekwa mikononi mwa wachache
 
Wana JF,

Nimepata Tetesi kuwa Issue kubwa kuhusi hizo Billion zilizo kutwa kwa Account ya Adv. Mwale ilikuwa ni Issue ya Kuuuza Aridhi na zilitumwa na wateje kutoka huko USA na Muhusika mkuu alikuwa ni Adv. Nyaga Paul Mawalla, Inavyosemekana baada ya Mwale na mawalla kupokea hiyo Deal wakajiuliza nani asimamie show basi Mwale akajitosa kusimamia show huku na kule pesa zika tumwa zikaja kama kawaida CRDB Bank yetu inayo husika na shutuma nyingi za kupitisha pesa kimya kimya kwa mafungu makubwa ilihusika na ndipo hapo zilipo kuja kubumburuka Nyaga Paul Mawalla aka kaa mbali na kukana kabisa kuwa hausiki na kuuza viwanja wakati swala liko wazi kuwa Adv. Nyaga Mawalla moja kwa moja hujihusisha na uuzaji wa aridhi na anamaeneo mengi sana mfano pale Arusha Burka, Dar-goba,Meatu, nakadharika.

Katika sakata hilo la Billion za Mwale limepelekea hadi Baadhi ya wafanya kazi wa CRDB Bank kuiitwa na kuhojiwa kituo cha Police.

My Take:

Wanasheria wengi wao esp Huko Arusha nadhani hiizi deal za viwanja wana husika sana, TAKUKURU iwachunguze na Halimashauri za Miji zitupe details za ukweli wakina nani wana Hold maeneo makubwa na esp kwa Wanasheria Tu ndio Mtajua wanasheria wetu kwa kiasi gani wanatuhujumu nchi yetu.

Hii sasa naanza kuamini kuwa Nchi yetu na serikali yetu ndio imeifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 7 Africa kwa serikali kuwa corrupt kwa kuuza Aridhi kwa wageni esp wazungu kutoka USA.
 
Kama ni pesa halali, then haina shaka... tatizo ni kama pesa za wizi
 
Kama ni pesa halali, then haina shaka... tatizo ni kama pesa za wizi

pesa halali tzs 18 bil....oooh no no no,....haiwezekani hata kidogo,kazi ya uwakili sidhani kama inalipa kiasi cha kuwa na hela hizo kwenye akaunti moja,....kumbuka hapa hatuzungumzii asset za mwale ni pesa alizonazo kwenye akaunti
 
Nazidi kuuliza, CRDB wanatumia sheria gani hasa inayowapa mamlaka ya kufanya money laundering? Karibu hela zote kubwa haramu zinaonekana kupitia mikononi mwa hii Bank tukianza na EPA!
 
Nazidi kuuliza, CRDB wanatumia sheria gani hasa inayowapa mamlaka ya kufanya money laundering? Karibu hela zote kubwa haramu zinaonekana kupitia mikononi mwa hii Bank tukianza na EPA!
CRDB Tumeibaini, kilichobaki ni kubaini aliye nyuma ya mchezo huu mchafu. Kwa maana nyingine anayeamuru sheria na kanuni za kibenki zivunjwe. Ni wazi hapo kuna mtu au kundi fulani lina nguvu kiasi cha kufanya CRDB iwe kama kibubu (wale wa uswazi wenzangu tunajua kibubu) binafsi cha kuweka na kuchukua tena bila kufuata taratibu. Kwani ni muda sasa tangu hizi tuhuma dhidi ya CRDB jamani.
 
Wito: wanataaluma wenzetu kwenye tasnia ya sheria mnatakaiwa kukaa na kutafakari mchango wenu kwenye haya matukio. Nafikiri mnahitaji pia kupitia mtaala wenu na mtusaidie kujenga uzalendo baina ya yenu na wateja mnaowahudumia. Binafsi nasikitika mnaposhutumiwa kwa mikataba mibovu na sasa kula njama za kuuza nchi kinyemela. inasikitisha jamani. hebu wakongwe tutafakari hili
 
pesa halali tzs 18 bil....oooh no no no,....haiwezekani hata kidogo,kazi ya uwakili sidhani kama inalipa kiasi cha kuwa na hela hizo kwenye akaunti moja,....kumbuka hapa hatuzungumzii asset za mwale ni pesa alizonazo kwenye akaunti
<br />
<br />
UKIWA WAKILI WA MAFISADI HIZO NI KIDOGO SANA ALAAA
 
19 Apr 2011 – WAKILI Median Mwale anayemtetea Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Anna Mwahalende
Kenyan robbery suspects shifted to Arusha
by Staff Reporter
10 Kenyan nationals who were in custody in Moshi for suspected robbery of the National Bank of Commerce (NBC) and stealing Tsh.5.3 billion were last week transferred to Arusha Regional Prison to ease hearing of the government’s appeal against their application of filing an abduction case against Tanzania and Mozambique authorities.
In its appeal the government is praying the court of appeal to quash the trial court decision to allow the application by the suspects through their lawyers.
Median Mwale, one of the suspects’ advocates confirmed the transfer of his clients to Arusha ready for hearing of the government appeal from 15[SUP]th[/SUP] October before three high court judges.

On June 5, 2006 High Court Judge John Mkwawa had set aside the government objection against the suspects application for hearing of their abduction case.
The suspects applied for hearing of their application for abduction by Tanzania and Mozambique state authorities claiming that the action is contrary to international law.
In the trial court ruling the suspects’ lawyers Median Mwale and Loomu Ojare were allowed to file formal application for hearing, with amendments, of abduction case of their clients which the government of Tanzania is now appealing against.
In the original case of robbery the Kenyans were booked for stealing of Tsh.5.3 billion from NBC branch in Moshi the case which Judge Mkwawa has agreed to postpone awaiting the ruling on the suspects abduction case applicatio

7 Apr 2011 – ... (47) are among those still on the hook for the conspiracy and robbery charge, and are being represented by Arusha advocate Median Mwale. ...

--------



REPORT BY A MEMBER OF THE TANGANYIKA LAW SOCIETY IN THE ADVOCATES COMMITTEE TO THE HALF ANNUAL GENERAL MEETING TO BE HELD ON THE 13[SUP]th [/SUP]AUGUST 2010 AT DODOMA

1. Application No. 12 of 2010: Abdallah Hassan versus Median Mwale, Advocate
The Complainant alleges that he had handed a Title Deed over to Advocates Median Mwale and Ruwaichi John for conveyance of the subject farm to ERBS Smarty Hardy Co. Ltd. Instead the Advocate went behind him and purported to sell the property to another entity, namely, the Registered Trustees of Congregation of Sisters of Notre Dame, from whom they received some money without the Complainant’s knowledge. He further alleges that the Advocates have refused to return to him the Title Deed aforesaid. Pleadings are not complete. The matter is scheduled for mention on 29[SUP]th[/SUP] September 2010

ANATISHA HUYU WAKILI KWA VIJISENTI NA KUHONGA MAHAKAmA PALE ARUSHA...
 
<br />
<br />
bilioni 18 zitumwe toka u.s.a kwa ajili ya viwanja it doesnt make sense hapa kuna issue hatuijui ila ukweli utajulikana

REPORT BY A MEMBER OF THE TANGANYIKA LAW SOCIETY IN THE ADVOCATES COMMITTEE TO THE HALF ANNUAL GENERAL MEETING TO BE HELD ON THE 13[SUP]th [/SUP]AUGUST 2010 AT DODOMA
1. Application No. 12 of 2010: Abdallah Hassan versus Median Mwale, Advocate
The Complainant alleges that he had handed a Title Deed over to Advocates Median Mwale and Ruwaichi John for conveyance of the subject farm to ERBS Smarty Hardy Co. Ltd. Instead the Advocate went behind him and purported to sell the property to another entity, namely, the Registered Trustees of Congregation of Sisters of Notre Dame, from whom they received some money without the Complainant's knowledge. He further alleges that the Advocates have refused to return to him the Title Deed aforesaid. Pleadings are not complete. The matter is scheduled for mention on 29[SUP]th[/SUP] September 2010


Nadhani hiki kipande hapo mkuu kitakusaidia pia ujue kuwa issue ni Land pia kama ulivyo sema ngoja tungojee na issue zingine kama zipo
 
kweli kila jambo litasemwa humu ndani, but sijapata kuona watu wajinga kama wanaopoteza muda kuongea vitu vya uongo, hivi nyinyi wtu huu umbea wote mnao uandika huku ndani mnajua ukweli wake? acheni unafiki
 
kweli kila jambo litasemwa humu ndani, but sijapata kuona watu wajinga kama wanaopoteza muda kuongea vitu vya uongo, hivi nyinyi wtu huu umbea wote mnao uandika huku ndani mnajua ukweli wake? acheni unafiki

nikikutusi ntakuwa nimekuonea?hivyo vya ukweli mbona hujaviongea?
 
Mkuu Jethro thanx for the info! Namuonea huruma Medium lakini hizi hela ni nyingi mno. He should have known better. I hope haya yataisha salama maana machache nnayoyajua kuhusu yeye ni mema for the most part.
 
...habari yenyewe ilivyoripotiwa na Mwananchi haijakaa sawa.wameandika kuwa hakimu kakubaliana na mashtaka matatu ya kwanza na kukataa kuanzia shtaka la tatu,bila kutuambia ni mashtaka gani hayo.kwa hiyo kwa hiyo just kwa logic sidhani kama naweza kusema chochote,maana itakuwa kulongalonga,kama sijui ni mashtaka gani hasa ambayo huyu jamaa anatuhumiwa....hii inadhihirisha udhaifu wa waandishi wetu wa habri,kuandika habari nusunusu,maana kama unaacha kiini hasa cha habari basi unakuwa huripoti kitu bali ni ushabiki tu.
Anasema katika ripoti kuwa kashtakiwa kwa kuwa kakutwa na bilioni 18.sasa je ukiwa na bilioni pekee ndo chanzo cha kushtakiwa,na kama unashindwa kuripoti kuhusu ni sheria gani hasa zimevunjwa kutokana na hati ya mashtaka basi hakuna kitu cha kujadili hapa,maana tunajadili kitu tusichokijua.
 
...habari yenyewe ilivyoripotiwa na Mwananchi haijakaa sawa.wameandika kuwa hakimu kakubaliana na mashtaka matatu ya kwanza na kukataa kuanzia shtaka la tatu,bila kutuambia ni mashtaka gani hayo.kwa hiyo kwa hiyo just kwa logic sidhani kama naweza kusema chochote,maana itakuwa kulongalonga,kama sijui ni mashtaka gani hasa ambayo huyu jamaa anatuhumiwa....hii inadhihirisha udhaifu wa waandishi wetu wa habri,kuandika habari nusunusu,maana kama unaacha kiini hasa cha habari basi unakuwa huripoti kitu bali ni ushabiki tu.
Anasema katika ripoti kuwa kashtakiwa kwa kuwa kakutwa na bilioni 18.sasa je ukiwa na bilioni pekee ndo chanzo cha kushtakiwa,na kama unashindwa kuripoti kuhusu ni sheria gani hasa zimevunjwa kutokana na hati ya mashtaka basi hakuna kitu cha kujadili hapa,maana tunajadili kitu tusichokijua.
Tuache kujadili mada kutokana na ushabiki wa kijiweni,bali kutokana na facts,na kwa jinsi hii habari ilivyoripotiwa,basi hatuna facts zozote,unless kama kuna miongoni mwetu walioona hiyo hati ya mashtaka.Na sidhani kwa Tanzania huyu bwana ni wa kwanza kuwa na kiasi hiki cha pesa.
 
Back
Top Bottom