Wakikutana hawanyimani!?

Baba Erick

JF-Expert Member
Aug 24, 2011
483
75
Habari za uzima wana JF,

Kuna jambo linanitatiza sana pale unaposhuhudia mke/girlfriend au mme/boyfriend wa mtu anaendeleza uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wake wa zamani au mpenzi wake waliocheza "kibaba baba" au "kimama mama" na ninaposikia watu wakisema kuwa msichana ulimtoa usichana/bikr* ni vigumu kukusahau na hata ukikutana naye baada ya kuolewa kwake hakunyimi.

INANIPA SHIDA SANA UKIZINGATIE WENGI WETU TUNAOANA TAYARI TUMESHAINGIA KWENYE MAHUSIANO MENGINE. Jamani naombeni mawazo yenu kwani nahofia kuoa tena.
 
Inategemea na beki za huyo msichana mwenyewe...kama beki hazikabi then atatoa kwa wengi ikiwemo na kwa huyo aliemwanzisha kikosi cha kwanza.
 
mkuu hii issue ni tabia ya mtu tu.. sio wote wanafanya hivyo, hata ufanyaje kama mtu ni kicheche atabaki kua hivyo
 
wapi wadada wa jf,..leteni ukweli mlionao moyoni mwenu kuhusu hili jaman
 
Huo ni utumwa kabisa,mtu ulishaachana nae unakutana nae eti mnakumbushiana ili iweje sasa?kwanini mlishindwa kuwa pamoja basi kwenye maisha kama mliona kila mmoja hawezi kumsahau mwenzie?
 
hapo sijui kwakweli ila huo utakua mchezo wa kuigiza na sio tabia ya watu wenye akili timamu
 
Back
Top Bottom