Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Kwa sasa hakuna mwanasiasa anaeogopwa na watu wa chama cha kijani kama kamanda wetu ambae ni kiboko ya bwana yule na hivyo sitashangaa zikafanyika fitina za kisiasa za kuhakikish hashiriki hata kampeni za uchaguzi mwakani ikiwa watafanikiwa kumkosesha sifa za kuwa mgombea wa nafasi yoyote ya kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao.
Wakifanikiwa kumkosesha sifa za kugombea nafasi yoyote katika uchaguzi wa mwakani,bado wanaweza kuona haitoshi kutokana na kuhofia ushiriki wake katika kampeni za kuwanadi wagombea wengine hivyo kwa hofu na woga, wanaweza kumuundia zengwe lingine ikiwa ni pamoja na kumuweka kolokoloni kipindi chote cha kampeni kuhakikisha hapandi majukwaani kumnadi mgombea yoyote yule hasa wa ile nafasi nyeti kuliko zote.
Kama nilivyowahi kusema,japo hawategemea sanduku la kura kushinda,ila bado wangetamani sana washinde kupitia sanduku la kura ili ushindi unoge hivyo ni lazima wapambane kujaribu kushinda kupitia sanduku la kura kabla ya kufikiria njia nyingine kama ile ya kufanikisha ushindi kwa njia ya "bao la mkono".
Binafsi sina imani na hawa watu kabisa na kwakweli wanaweza fanya lolote bila hata aibu kama ambavyo teyari wameshafanya mpaka sasa.
Wakifanikiwa kumkosesha sifa za kugombea nafasi yoyote katika uchaguzi wa mwakani,bado wanaweza kuona haitoshi kutokana na kuhofia ushiriki wake katika kampeni za kuwanadi wagombea wengine hivyo kwa hofu na woga, wanaweza kumuundia zengwe lingine ikiwa ni pamoja na kumuweka kolokoloni kipindi chote cha kampeni kuhakikisha hapandi majukwaani kumnadi mgombea yoyote yule hasa wa ile nafasi nyeti kuliko zote.
Kama nilivyowahi kusema,japo hawategemea sanduku la kura kushinda,ila bado wangetamani sana washinde kupitia sanduku la kura ili ushindi unoge hivyo ni lazima wapambane kujaribu kushinda kupitia sanduku la kura kabla ya kufikiria njia nyingine kama ile ya kufanikisha ushindi kwa njia ya "bao la mkono".
Binafsi sina imani na hawa watu kabisa na kwakweli wanaweza fanya lolote bila hata aibu kama ambavyo teyari wameshafanya mpaka sasa.