Wakenya waishambulia Serikali Loliondo, mwana mama jasusi la kimataifa susana norduland agawa simu za kupigia picha

msuyaeric

JF-Expert Member
Dec 18, 2014
838
1,167
Imeelezwa kuwa wakati serikali ikiendesha zoezi la kuweka mipaka katika Pori tengefu la Loliondo, makundi ya wananchi kutoka Kenya wamewavamia askari na kuwashambulia kwa silaha za jadi ikiwemo, Mishale, Mkuki na Marungu, watu hao ambao wamejiweka kama wananchi wa kijiji cha Ololosokwani wametokea Kenya maeneo ya mpakani na kuingia kwaajili ya kuzuia uwekaji wa mpaka wa Pori tengefu la Loliondo kwa kuwa ndipo yalipo malisho ya Mifugo yao,

Katika vurugu hizo wamewajeruhi askari kadhaa waliokuwa wakifanya doria katika maeneo hilo, ambapo walijeruhiwa wakati wakijaribu kuwatuliza watu hao wasifanye fujo, baada ya Askari kujeruhiwa iliwalazimu kutumia nguvu kidogo ili kutuliza fujo hizo ambapo baadhi watu hao walijeruhiwa, ambapo imeelezwa kwamba majeruhi hao wamepelekwa katika Hospitali za Kenya za Posmoru na Lalemtya Wilaya ya Narok

Vurugu hizo zinatokana na hamasa iliyofanywa na baadhi ya Viongozi wakenya ambao wametajwa kuwa na Mifugo yao katika eneo akiwemo Seneta wa Count ya Narok Bw. Oledema na Chief wa Posmoru na matajiri wengine wa Kenya

Baadhi ya wananchi ambao ni Watanzania wamekiri kwamba ipo nguvu kutoka Kenya ambapo wamesema lengo la wakenya hao ni kuhakikisha kwamba serikali ya Tanzania inashindwa kulihifahi eneo hilo kwa kuwa ndilo wanalotegemea kwa malisho ya Mifugo yao na kufanya ujangili wa kuwinda wanyama pori ikiwemo Tembo, wananchi hao wamesema wao wamefurahishwa na kitendo cha serikali kulihifadhi eneo hilo kwakuwa litasaidia sana kuhifadhi malisho ya Mifugo yao kwakuwa Mifugo ya wakenya itaondoka

Wananchi hao wa Tanzania wanasema "sisi tupo tayari kuungana na serikali kwa kuwa tunaamini eneo linalotengwa nikwa manufaa yetu na Mifugo wetu itapata malisho ya kutosha baada ya wakenya kuondoka" alisema mwananchi mmoja kutoka katika kijiji cha Ololosokwani, ambaye jina lake limehifadhiwa

Wananchi hao wamesema zoezi la uwekaji wa bicons za mpaka wa Pori tengefu la Loliondo linaendele vizuri na hakuna fujo kati ya wananchi Watanzania na serikali yao, ambapo wameonya juu ya watu na mitandao inaopotosha kwamba wananchi wa Tarafa ya Loliondo wamepanga kupambana na serikali katika zoezi hilo, wamesema picha zinazosambaa katika mitandao ya kijamii sio za Watanzania na kwamba hakuna Mtanzania yeyote aliyepatwa na tatizo kutokana na vurugu hizo

Wakati huo huo imeelezwa kuwa Mwana mama ambaye ni Jasusi la kimataifa raia wa Sweden bi. Susan Norduland ametuma simu nyingi za smart phone ambazo zimegawiwa kwa baadhi vijana wa Tarafa ya Loliondo katika vijiji vya Ololosokwani, Soitisambu, Kirtalo, Oloipiri, Losoito, Olorieni, Mbukeni Arashi, Piyaya na Malambo, ambapo chanzo cha habari kimesema kuwa simu hizo ziliinginzwa kutoka Kenya na Diwani wa Ololosokwani Mheshimiwa Moloimet Sain'geu ambapo alizipokea kutoka kwa Jasusi hilo pamoja na Seneta Oledama, ambapo simu hizo zitatumika kupiga picha katika matukio mbalimbali yanayohusu Uhifadhi na kumtumia Jasusi huyo mwenyewe na kusambaza katika mitandao ya kijamii, ili kuonyesha kuwa wananchi wa Tarafa ya Loliondo wananyanyasika katika zoezi hilo la uwekaji bicons na matukio mengine

Susana Norduland alipigwa maarufu kuingia Tanzania mwaka 2014 ambapo alipewa PI akitumia hati ya kusafiria ya Marekani na kurudi tena mwaka 2016 akitumia hati ya kusafiria ya Sweden ambapo pia alikamatwa na kufukuzwa tena kwa PI mwaka huo, hata hivyo amekuwa akiingia Tanzania kupitia njia za panya akitokea Kenya kwa msaada wa baadhi ya watu na Viongozi wa Kenya

Kufukuzwa kwa mwanamke huyo ni kutokana na vitendo vyake vya kichochezi ambapo amekuwa akichochea vurugu za kijamii katika Tarafa ya Loliondo tangu mwaka 2001, ambapo alianza na uchochezi wa vita vya kikabila kati ya Wamasai wa Loita na Batemi, ambapo alikuwa mnunuzi mkubwa wa Silaha za kupigania zilizokuwa zikiingizwa kwa njia za haramu, baadae kuanzisha mtandao wa uwindaji haramu wa Tembo, ambapo alikuwa mfadhili wa wawindaji haramu na mnunuzi mkubwa wa meno ya Tembo na kuendeleza uchochezi wa migogoro kati ya Hifadhi na vijiji kwa mwamvuli wa kujifanya mtetezi wa haki za wananchi wa Tarafa ya Loliondo

Sent from my SM-A325F using JamiiForums mobile app
 
Samia aliomba msamaha tena ndani ya Ikulu yetu takatifu kwa Wakenya, alijishusha mwenyewe akifikiri kwamba they care about her, sasa bili inakuja, Mungu hamfichi mnafiki, walifikiri kwa kumponda Magu(RIP) wangeheshimika kumbe ndo kwanza wanawadharau na bado Mzungu wa USA hajawageuka bado!
 
Samia aliomba msamaha tena ndani ya Ikulu yetu kwa Wakenya, alijishusha mwenyewe akifikiri they care about her, sasa bili inakuja, Allah hamfichi mnafiki, walifikiri kwa kumponda Magu(RIP) wangeheshimika, Uhuru Kenyata akaalikwa mgeni rasmi mpaka Jeshi letu likampa heshima kujipendekeza kote kumbe ndo kwanza wanawadharau na kuwaona low na bado Mzungu wa USA hajawageuka bado.

Labda Uhuru Kenyata atamuomba Samia msamaha pia, ngoja tuone!
 
Hili suala la wakenya kuingia Tanzania naona linatumiwa kipropaganda, ikumbukwe Kenya napo wapo wamasai, na hiki ndicho chanzo cha serikali ya Tanzania kutumia njia hiyo ili kuzima kile kinachoendelea Ngorongoro.

Msipokuwa waangalifu naona mnaenda kuleta mgogoro wa kidiplomasia na serikali ya Kenya, nyie endeleeni kuropoka tu. Pale mtakapoambiwa mthibitishe madai yenu sijui mtatoa ushahidi wa sura za wamasai, au yale mashuka yao.

Halafu kama wakenya wanaingia Tanzania bila kibali kwanini hawazuiwi mpakani? au mnakiri kwamba mpaka wetu na Kenya hauna ulinzi, au ulinzi uliopo ni dhaifu?

Zaidi naona mnadhalilisha jeshi letu bila nyie kujua, mnalionesha lilivyo dhaifu kwenye kulinda mipaka yetu wakati kila siku huwa wanatuaminisha mipaka yetu iko salama, dawa ya tatizo sio kulikimbia, ni kukulitatua.
 
Imeelezwa kuwa wakati serikali ikiendesha zoezi la kuweka mipaka katika Pori tengefu la Loliondo, makundi ya wananchi kutoka Kenya wamewavamia askari na kuwashambulia kwa silaha za jadi ikiwemo, Mishale, Mkuki na Marungu, watu hao ambao wamejiweka kama wananchi wa kijiji cha Ololosokwani wametokea Kenya maeneo ya mpakani na kuingia kwaajili ya kuzuia uwekaji wa mpaka wa Pori tengefu la Loliondo kwa kuwa ndipo yalipo malisho ya Mifugo yao,

Katika vurugu hizo wamewajeruhi askari kadhaa waliokuwa wakifanya doria katika maeneo hilo, ambapo walijeruhiwa wakati wakijaribu kuwatuliza watu hao wasifanye fujo, baada ya Askari kujeruhiwa iliwalazimu kutumia nguvu kidogo ili kutuliza fujo hizo ambapo baadhi watu hao walijeruhiwa, ambapo imeelezwa kwamba majeruhi hao wamepelekwa katika Hospitali za Kenya za Posmoru na Lalemtya Wilaya ya Narok

Vurugu hizo zinatokana na hamasa iliyofanywa na baadhi ya Viongozi wakenya ambao wametajwa kuwa na Mifugo yao katika eneo akiwemo Seneta wa Count ya Narok Bw. Oledema na Chief wa Posmoru na matajiri wengine wa Kenya

Baadhi ya wananchi ambao ni Watanzania wamekiri kwamba ipo nguvu kutoka Kenya ambapo wamesema lengo la wakenya hao ni kuhakikisha kwamba serikali ya Tanzania inashindwa kulihifahi eneo hilo kwa kuwa ndilo wanalotegemea kwa malisho ya Mifugo yao na kufanya ujangili wa kuwinda wanyama pori ikiwemo Tembo, wananchi hao wamesema wao wamefurahishwa na kitendo cha serikali kulihifadhi eneo hilo kwakuwa litasaidia sana kuhifadhi malisho ya Mifugo yao kwakuwa Mifugo ya wakenya itaondoka

Wananchi hao wa Tanzania wanasema "sisi tupo tayari kuungana na serikali kwa kuwa tunaamini eneo linalotengwa nikwa manufaa yetu na Mifugo wetu itapata malisho ya kutosha baada ya wakenya kuondoka" alisema mwananchi mmoja kutoka katika kijiji cha Ololosokwani, ambaye jina lake limehifadhiwa

Wananchi hao wamesema zoezi la uwekaji wa bicons za mpaka wa Pori tengefu la Loliondo linaendele vizuri na hakuna fujo kati ya wananchi Watanzania na serikali yao, ambapo wameonya juu ya watu na mitandao inaopotosha kwamba wananchi wa Tarafa ya Loliondo wamepanga kupambana na serikali katika zoezi hilo, wamesema picha zinazosambaa katika mitandao ya kijamii sio za Watanzania na kwamba hakuna Mtanzania yeyote aliyepatwa na tatizo kutokana na vurugu hizo

Wakati huo huo imeelezwa kuwa Mwana mama ambaye ni Jasusi la kimataifa raia wa Sweden bi. Susan Norduland ametuma simu nyingi za smart phone ambazo zimegawiwa kwa baadhi vijana wa Tarafa ya Loliondo katika vijiji vya Ololosokwani, Soitisambu, Kirtalo, Oloipiri, Losoito, Olorieni, Mbukeni Arashi, Piyaya na Malambo, ambapo chanzo cha habari kimesema kuwa simu hizo ziliinginzwa kutoka Kenya na Diwani wa Ololosokwani Mheshimiwa Moloimet Sain'geu ambapo alizipokea kutoka kwa Jasusi hilo pamoja na Seneta Oledama, ambapo simu hizo zitatumika kupiga picha katika matukio mbalimbali yanayohusu Uhifadhi na kumtumia Jasusi huyo mwenyewe na kusambaza katika mitandao ya kijamii, ili kuonyesha kuwa wananchi wa Tarafa ya Loliondo wananyanyasika katika zoezi hilo la uwekaji bicons na matukio mengine

Susana Norduland alipigwa maarufu kuingia Tanzania mwaka 2014 ambapo alipewa PI akitumia hati ya kusafiria ya Marekani na kurudi tena mwaka 2016 akitumia hati ya kusafiria ya Sweden ambapo pia alikamatwa na kufukuzwa tena kwa PI mwaka huo, hata hivyo amekuwa akiingia Tanzania kupitia njia za panya akitokea Kenya kwa msaada wa baadhi ya watu na Viongozi wa Kenya

Kufukuzwa kwa mwanamke huyo ni kutokana na vitendo vyake vya kichochezi ambapo amekuwa akichochea vurugu za kijamii katika Tarafa ya Loliondo tangu mwaka 2001, ambapo alianza na uchochezi wa vita vya kikabila kati ya Wamasai wa Loita na Batemi, ambapo alikuwa mnunuzi mkubwa wa Silaha za kupigania zilizokuwa zikiingizwa kwa njia za haramu, baadae kuanzisha mtandao wa uwindaji haramu wa Tembo, ambapo alikuwa mfadhili wa wawindaji haramu na mnunuzi mkubwa wa meno ya Tembo na kuendeleza uchochezi wa migogoro kati ya Hifadhi na vijiji kwa mwamvuli wa kujifanya mtetezi wa haki za wananchi wa Tarafa ya Loliondo

Sent from my SM-A325F using JamiiForums mobile app
nonsense, usianzishe mgogoro wa kidiplomasia hapa, hili swala linajulikana ni la ndani tu
 
Kama serikali inashindwa kuwatambua raia zake kwenye eneo husika, nani alaumiwe kama siyo serikali yenyewe?

Andiko hili, pamoja na pengine kuwemo na ukweli kuhusu hao watu kutoka Kenya, lakini linaonekana kama propaganda nyingine ya kuendelea kuwakandamiza wananchi wa Loliondo.

Raia toka nchi jirani waje wapambane na jeshi letu halafu warudi kwao salama, na wala hakuna aliyekamatwa kuonyesha ushahidi?

Serikali hii imekuwa na uongo mwingi.
 
Wakenya tena...!?

Au mnalahirisha namna ya kuongeza kichapo mkidai wa Masai wa Tanganyika hawana tabu Ila ndio hao mnawatandika kwa mgongo wa wakenya..?

Fanyeni namna ya kuzungumza nao na sio kutimia nguvu
 
Samia aliomba msamaha tena ndani ya Ikulu yetu takatifu kwa Wakenya, alijishusha mwenyewe akifikiri kwamba they care about her, sasa bili inakuja, Mungu hamfichi mnafiki, walifikiri kwa kumponda Magu(RIP) wangeheshimika kumbe ndo kwanza wanawadharau kama takataka na bado Mzungu wa USA hajawageuka bado!
Kwamba "tunaomba radhi kwa kuchoma vifaranga vya kuku vilivyoingizwa nchini bila kufuata utaratibu" Hangaya apewe kumi akimaliza kipindi hiki cha mpito!
 
Hili suala la wakenya kuingia Tanzania naona linatumiwa kipropaganda, ikumbukwe Kenya napo wapo wamasai, na hiki ndicho chanzo cha serikali ya Tanzania kutumia njia hiyo ili kuzima kile kinachoendelea Ngorongoro.

Msipokuwa waangalifu naona mnaenda kuleta mgogoro wa kidiplomasia na serikali ya Kenya, nyie endeleeni kuropoka tu. Pale mtakapoambiwa mthibitishe madai yenu sijui mtatoa ushahidi wa sura za wamasai, au yale mashuka yao.

Halafu kama wakenya wanaingia Tanzania bila kibali kwanini hawazuiwi mpakani? au mnakiri kwamba mpaka wetu na Kenya hauna ulinzi, au ulinzi uliopo ni dhaifu?

Zaidi naona mnadhalilisha jeshi letu bila nyie kujua, mnalionesha lilivyo dhaifu kwenye kulinda mipaka yetu wakati kila siku huwa wanatuaminisha mipaka yetu iko salama, dawa ya tatizo sio kulikimbia, ni kukulitatua.
Point! Kama Wamasai wa Kenya wanaweza kuja kufanya vurugu mpaka kuwajeruhi Polisi wa Tanzania basi huo utakuwa ni udhaifu mkubwa kwa upande weru. Jeshi letu ndilo linalinda mipaka yetu. Je, limeshindwa kuilinda?
 

Olekaturi Kurambe Olekaturi

dsnpooSret5 91ovhi77ee8,rfNh1g4020 4611854fmmb0 ·

Nimepokea taarifa kwamba huko Mambarashani OBC wameanza makazi (kuandaa kambi kwa mgeni) na watu machungani wameanza kupigwapigwa makofi.
Watu kadhaa wamesema hiyo ni kweli!
Mahakama ya Afrika Mashariki imetoa zuio dogo dhidi ya unyanyasaji.
Sasa kuna vitu viwili vya kufanya:
1 Kupata taarifa kamili.
2 Kuripoti kwa mahakama.
Do something now!
Copy & paste
Kutoka kwa Susanna Norduland.
👆🏻
👆🏻
👆🏻
👆🏻
👆🏻
👆🏻
👆🏻
👆🏻

_________________________
Watanzania wenzangu hapa lengo ni kumjibu huyu Mbwa Koko, asiye na kwao ambaye anaishi akijua Tanzania ni nyumbani kwa bibi yake.

Naomba ifahamike kwamba huyu Mwanamke Mpumbavu anayeishi kama mtu asiye na kwao ndo yule aliyesaidiana na Taasisi moja ya Jijini Nairobi kuifungulia kesi Serikali ya Tanzania katika Mahakama ya EAC kupinga kutengenezwa kwa Barabara ya MTOWAMBU - LOLIONDO kwa sasa LOLIONDO - MTOWAMBU lakini Serikali yetu ilikomaa na sasa Barabara ya kiwango cha Lami inatengenezwa na Mkandarasi CHINA WU, YI, CO. LTD yupo site na anaendelea na kazi, huyu ndio mtoa habari kwa vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa visivyojua nini kinachoendela Loliondo na kutangazia Ulimwengu kwamba wananchi Watanzania wa Loliondo wilayani Ngorongoro wananyanyaswa na kuonewa na Serikali yao, Huyu mwanamama ndio mwandishi wa ripoti za kizushi za Orkland akisaidiana na baadhi ya watu wetu anaowalipa kwa kipato kisichojulikana, ninataka kuuambia Ulimwengu na Watanzania kwamba Mwanamke huyu ambaye zamani aliishi Tanzania kama Mwalimu wa KiHispaniola ni Mtu hatari kwa Usalama wa Mataifa ya Africa Mashariki, amekuwa akiwarubuni wananchi wa Loliondo Tanzania kwamba wanaonewa na kuwatafutia fedha za kuendesha kesi na Serikali yao na kupinga shughuli mbalimbali za Maendeleo zinazofanywa na Serikali hapa Loliondo, lakini nitumie nafasi hii kuwaambia Wananchi wala msidanganiyike, Pamoja na Serikali kusitakiwa mahakama ya EAC kupinga Barabara yetu lakini Serikali haikuondoa nia na sasa imetimiza, sasa siamini kama Serikali hii hii inaweza kuondoa nia yake ya kuhifadhi Loliondo kwaajili ya Jibwa Jike la Kiswidishi, wawekezaji waliopo na wanaokuja Loliondo kila Mara ni mkakati wa Serikali yetu kuwekeza na kukuza uchumi wa Taifa letu na sio kumsikiliza Mbwa Jike la Kizungu kama Susanna na kama ana ubavu aache kupiga tararira akiwa Ulaya aje Tz japo kwa dakika 10 tu alafu atasimulia Uhuru na Utawala wa kizalendo uliopo hapa Tanzania.

Ni rai yangu kwetu sisi Watanzania tuachane na kupandikizwa chuki ya kuichukia nchi yetu na wazungu wasio na Mwelekeo kama Susanna, badala yake tujikite kushauriana na Serikali yetu katika mambo ya msingi tunayotaka Serikali yetu itufanyie, mapambano na nguvu kubwa ya kudai madai yetu hayawezi kuwa na tija, Serikali yetu ni sikifu na inajali hoja za Watanzania na sisi ndo Watanzania wenyewe. Pengine tu tunaweza kutofautiana lugha lakini malengo yetu ni mamoja tusikubali kutumika kwa vyovyote vile

Paul Dudui.
 
Haya ndiyo matumizi mabaya ya mtandao. Hiyo habari unaweza kuithibitisha iwapo itahitajika hivyo
 
Hizo quotations zinaonyesha una video au sauti zao, tunaomba utuwekee hapa where we dare to talk
 
Imeelezwa kuwa wakati serikali ikiendesha zoezi la kuweka mipaka katika Pori tengefu la Loliondo, makundi ya wananchi kutoka Kenya wamewavamia askari na kuwashambulia kwa silaha za jadi ikiwemo, Mishale, Mkuki na Marungu, watu hao ambao wamejiweka kama wananchi wa kijiji cha Ololosokwani wametokea Kenya maeneo ya mpakani na kuingia kwaajili ya kuzuia uwekaji wa mpaka wa Pori tengefu la Loliondo kwa kuwa ndipo yalipo malisho ya Mifugo yao,

Katika vurugu hizo wamewajeruhi askari kadhaa waliokuwa wakifanya doria katika maeneo hilo, ambapo walijeruhiwa wakati wakijaribu kuwatuliza watu hao wasifanye fujo, baada ya Askari kujeruhiwa iliwalazimu kutumia nguvu kidogo ili kutuliza fujo hizo ambapo baadhi watu hao walijeruhiwa, ambapo imeelezwa kwamba majeruhi hao wamepelekwa katika Hospitali za Kenya za Posmoru na Lalemtya Wilaya ya Narok

Vurugu hizo zinatokana na hamasa iliyofanywa na baadhi ya Viongozi wakenya ambao wametajwa kuwa na Mifugo yao katika eneo akiwemo Seneta wa Count ya Narok Bw. Oledema na Chief wa Posmoru na matajiri wengine wa Kenya

Baadhi ya wananchi ambao ni Watanzania wamekiri kwamba ipo nguvu kutoka Kenya ambapo wamesema lengo la wakenya hao ni kuhakikisha kwamba serikali ya Tanzania inashindwa kulihifahi eneo hilo kwa kuwa ndilo wanalotegemea kwa malisho ya Mifugo yao na kufanya ujangili wa kuwinda wanyama pori ikiwemo Tembo, wananchi hao wamesema wao wamefurahishwa na kitendo cha serikali kulihifadhi eneo hilo kwakuwa litasaidia sana kuhifadhi malisho ya Mifugo yao kwakuwa Mifugo ya wakenya itaondoka

Wananchi hao wa Tanzania wanasema "sisi tupo tayari kuungana na serikali kwa kuwa tunaamini eneo linalotengwa nikwa manufaa yetu na Mifugo wetu itapata malisho ya kutosha baada ya wakenya kuondoka" alisema mwananchi mmoja kutoka katika kijiji cha Ololosokwani, ambaye jina lake limehifadhiwa

Wananchi hao wamesema zoezi la uwekaji wa bicons za mpaka wa Pori tengefu la Loliondo linaendele vizuri na hakuna fujo kati ya wananchi Watanzania na serikali yao, ambapo wameonya juu ya watu na mitandao inaopotosha kwamba wananchi wa Tarafa ya Loliondo wamepanga kupambana na serikali katika zoezi hilo, wamesema picha zinazosambaa katika mitandao ya kijamii sio za Watanzania na kwamba hakuna Mtanzania yeyote aliyepatwa na tatizo kutokana na vurugu hizo

Wakati huo huo imeelezwa kuwa Mwana mama ambaye ni Jasusi la kimataifa raia wa Sweden bi. Susan Norduland ametuma simu nyingi za smart phone ambazo zimegawiwa kwa baadhi vijana wa Tarafa ya Loliondo katika vijiji vya Ololosokwani, Soitisambu, Kirtalo, Oloipiri, Losoito, Olorieni, Mbukeni Arashi, Piyaya na Malambo, ambapo chanzo cha habari kimesema kuwa simu hizo ziliinginzwa kutoka Kenya na Diwani wa Ololosokwani Mheshimiwa Moloimet Sain'geu ambapo alizipokea kutoka kwa Jasusi hilo pamoja na Seneta Oledama, ambapo simu hizo zitatumika kupiga picha katika matukio mbalimbali yanayohusu Uhifadhi na kumtumia Jasusi huyo mwenyewe na kusambaza katika mitandao ya kijamii, ili kuonyesha kuwa wananchi wa Tarafa ya Loliondo wananyanyasika katika zoezi hilo la uwekaji bicons na matukio mengine

Susana Norduland alipigwa maarufu kuingia Tanzania mwaka 2014 ambapo alipewa PI akitumia hati ya kusafiria ya Marekani na kurudi tena mwaka 2016 akitumia hati ya kusafiria ya Sweden ambapo pia alikamatwa na kufukuzwa tena kwa PI mwaka huo, hata hivyo amekuwa akiingia Tanzania kupitia njia za panya akitokea Kenya kwa msaada wa baadhi ya watu na Viongozi wa Kenya

Kufukuzwa kwa mwanamke huyo ni kutokana na vitendo vyake vya kichochezi ambapo amekuwa akichochea vurugu za kijamii katika Tarafa ya Loliondo tangu mwaka 2001, ambapo alianza na uchochezi wa vita vya kikabila kati ya Wamasai wa Loita na Batemi, ambapo alikuwa mnunuzi mkubwa wa Silaha za kupigania zilizokuwa zikiingizwa kwa njia za haramu, baadae kuanzisha mtandao wa uwindaji haramu wa Tembo, ambapo alikuwa mfadhili wa wawindaji haramu na mnunuzi mkubwa wa meno ya Tembo na kuendeleza uchochezi wa migogoro kati ya Hifadhi na vijiji kwa mwamvuli wa kujifanya mtetezi wa haki za wananchi wa Tarafa ya Loliondo

Sent from my SM-A325F using JamiiForums mobile app
mkuu wamekutuma kuja kupima upepo ?
 

Atuzwa kwa kuisumbua Serikali (1)​

Jamhuri June 15, 2016

maanda.jpg

Ngoitiko ambaye ni kiongozi wa asasi ya Pastoral Women Council (PWC), wakati wowote wiki hii atapewa tuzo ya Front Line Defenders Award for Human Rights inayotolewa na Shirika la The International Foundation For the Protection of Human Rights Defenders at Risk mjini Dublin, Ireland.

Mimi William Mosongo Alais – Diwani wa Kata ya Oloipiri na Ndugu Gabriel Kamomon Olle Killel – Mkurugenzi wa Shirika la KIDUPO Integrated Development Peoples’ Organization, tunakosoa utoaji wa tuzo hii kwa Maanda.

Hii tuzo haina ukweli wowote na faida kwa wafugaji wa Kimaasai. Amebebwa kupata tuzo hiyo na Susanna Nordlung, raia wa Sweden ambaye ni mmoja wa wavurugaji wakuu wa amani katika Loliondo, wakisaidiwa na kampuni ya Ndorobo Safaris.

Maanda ametumiwa na wajanja hao kupata tuzo kwa ajili ya maslahi binafsi ya hao waliopo nyuma ya pazia ambao ni DoroboSafaris na Susanna Nordlund. Hawa wanakusanya mamilioni ya fedha duniani kote na kuyafaidi kwa mgongo wa Wamaasai. Hii tuzo ni kama asante yao kwa Maanda kwa juhudi zake za kuifanya Loliondo isitawalike.

Kwa masikitiko makubwa, Maanda Ngoitiko amepata tuzo hiyo kwa njia ya kutuhumu Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mashirika yake ya umma kama vile TANAPA na Ngorongoro (NCAA), Thomson Safari, Ortello Busines Corporation, KIDUPO na Diwani wa Kata ya Oloipiri dhidi uporaji wa ardhi ya Wamaasai kama sehemu ya kupata pesa kutoka mashirika mbalimbali ya wafadhili na wahisani bila kusaidia jamii kwa pesa zilizopatikana.

Kwa mfano mwaka 2011 shirika la Pastoral Women Council of Tanzania (PWC) chini ya uongozi wa Maanda Ngoitiko alipata Sh 885,242,212 na mwaka 2012 alipata dola 717,521 za Marekani (Sh 1,112,158,137) bila kufanya miradi yoyote yenye tija ndani ya vijiji alivyoombea pesa hizo. Tunajiuliza, je utetezi huu wa Maanda ni wa dhati au ni wa kunufaika na migogoro anayoanzisha katika Tarafa ya Loliondo? Tunajiuliza tena kama Maanda anapigania kweli ardhi ya vijiji kama anavyodai kwenye tuzo, ni kwa nini anahamasisha na kushinikiza wahamiaji kutoka Kenya na kutoka vijiji ndani ya Tarafa ya Loliondo alivyopora ardhi yao yeye mwenyewe kuhamia maeneo katika vijiji vingine visivyo vyao bila kufuata utaratibu?

Maanda Ngoitiko amepata tuzo hii kwa hujuma na sisi tunaamini kwamba bado ana ajenda ya siri. Sisi tunataka kusema yafuatayo juu ya Maanda Ngoitiko na tuzo yake:

Mimi diwani wa Kata ya Oloipiri napenda kukanusha maneno ya uongo yaliyosemwa na Mheshimiwa Maanda Ngoitiko ili kuhalalisha kustahili kupewa tuzo kama ifuatavyo:

(1) Ninakanusha kuwa Mheshimiwa Maanda hakuzaliwa katika Kata ya Oloipiri, Kijiji cha Sukenya na wala baba yake hakuzaliwa wala hakuzikwa katika Kijiji cha Sukenya. Kiukweli ni kwamba Maanda Ngoitiko amezaliwa katika Kijiji cha Kirtalo, Kitongoji cha Olosirua katika Kata ya Soit-Sambu na pia baba yake amezikwa katika Kijiji cha Kirtalo.

(2) Kuhusiana na tuzo: Sisi tunasema kwamba Maanda Ngoitiko si mtetezi mkweli wa ardhi kwa jamii ya Wamaasai kama inavyosemekana katika tuzo, bali ni mporaji wa ardhi ya Waamasai. Kwa mfano, amejikatia eneo la karibu ekari 3,000 na kuweka uzio katika eneo la Irmasilig, Kata ya Soit- sambu katika Kijiji cha Mundorosi ambako kulikuwa maeneo ya malisho kwa wananchi wa Kijiji cha Mundorosi na Engusero-sambu na hivyo kusababisha mgogoro mkubwa wa ardhi uliosababisha mauaji ya ndugu yake.

Pili, uporaji wa ekari zaidi ya 3,000 uliyofanywa na Maanda ulisababisha kukosekana kwa maeneo ya malisho hivyo kusababisha migogoro ya malisho katika vijiji vingine vilivyotenga maeneo maalumu kwa ajili ya malisho ya mifugo yao. Mfano ni katika Kijiji cha Oloipiri.

(3) Sisi tunasema Maanda Ngoitiko si mtetezi (activist) wa ardhi ya Wamaasai kama tuzo inavyodai, bali amekuwa chanzo cha migogoro ya ardhi kati ya vijiji na vijiji, kwa mfano, Kijiji cha Sukenya na Mundorosi na pia kati ya Kijiji cha Kirtalo na Kijiji cha Oloipiri.

Maanda amekuwa mchochezi kati ya koo za Kimaasai. Kwa mfano, koo za Laitayok na koo ya Purko; na pia kati ya koo za Loita na Loitayok katika Kijiji cha Sukenya.

Amekuwa akiibua migogoro baina ya wawekezaji na wananchi. Kwa mfano, vijiji vilivyo karibu na shamba la TCL na vijiji vilivyo karibu na kitalu cha uwindaji cha OBC.

Maanda Ngoitiko amekuwa mchonganishi na mchochezi baina ya serikali na wananchi, kwa mfano, amekuwa akichochea maandamano ya vikundi vya wanawake dhidi Serikali juu ya masuala ya ardhi.
Maanda Ngoitiko si mtetezi wa Wamasai kuhusu masuala ya ardhi, bali ni mfanyabiashara anayetegeneza migogoro ya ardhi ili kunufaika yeye binafsi na migogoro hiyo, shirika lake pamoja na wadau wa mtandao wa shirika lake wamefanikisha, kwa mfano, ufunguzi wa kesi ya Sukenya dhidi Tanzania Conservation Limited na Kijiji Cha Sukenya.

Sisi tunaamini kwamba Maanda Ngoitiko anayo ajenda ya siri kuhusu OBC na Thomson ambao anawaita “land grabbers” yaani wapora ardhi ya Wamaasai na daima kuwaandika kwenye mitando ya jamii na kwenye tovuti mbalimbali za dunia wakati yeye mwenyewe amepora ekari nyingi za jamii bila kupewa na vilevile kuwa na wawekezaji wengine wengi ambao hawatajwi wala kuandikwa mitandaoni na wamewekeza kwenye vijiji vingine. Kwa mfano, wawekezaji wa Kijiji cha Ololosokwan, Clens Camp na End Beyond na wengine wanaomiliki maeneo makubwa yaliyokuwa ya malisho kama vile Ndorobo Safaris kule Ilmasilig.

Je, tatizo la Thomson na OBC kutetwa mno na Maanda Ngoitiko ni kwa sababu hafaidiki binafsi na miradi kutoka kwenye kampuni hizo?

Maanda Ngoitiko amekuwa mchochezi dhidi ya vijiji na OBC. Kwa mfano, amewahamasisha Wamasai kulima, kuweka maboma, kuweka soko la Karkarmoru na kujaza ng’ombe katika kitalu cha OBC ili washindwe kutimiza majukumu yao na hatimaye wakate tamaa waondoke.

Kitalu cha uwindaji cha OBC kimekuwa na ongezeko kubwa la mifugo kutoka Kenya, kata za Engusero-Sambu na Orgosorok na hivyo kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira, vyanzo vya maji na kusababisha kushuka kwa hadhi ya kitalu na kuwa chanzo cha wafugaji kuingiza ng’ombe kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kinyume cha sheria za nchi.

Kwa uchochezi Wamaasai wameaminishwa kwamba kitalu cha uwindaji cha OBC ni eneo la jumla la malisho ya mifugo kwa Maasai wote wakati wa masika na wa kiangazi pia.

Upotoshaji na uchochezi wa Maanda Ngoitiko umesababisha Wamaasai kuamini kuwa kuingiza mifugo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuweka maboma ni haki yao ya asili kinyume cha sheria za nchi juu Hifadhi hii ya Taifa.

Sisi tunasema Maanda Ngoitiko na shirika lake la Pastoral Women Council ni hatari kwa usalama wa Taifa kwa sababu wanashirikiana na wageni kuhujumu na kuharibu sifa nzuri ya nchi yetu.

Anashirikiana na baadhi ya watu waliopigwa marufuku kuingia hapa nchini, akiwamo Susanna Norduland ambaye alikuwa international volunteer wa shirika la Maanda la PWC na kuendelea kuwa msemaji wake wakati amepigwa marufuku na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Kwa makusudi Susanna kafungua tovuti lukuki kwa ajili tu ya kuvuruga amani ya Loliondo akishirikiana na Maanda Ngoitiko.

Sisi tunasema kwamba tuzo aliyopewa Maanda Ngoitiko si ya kweli na ya haki kwa sababu amepata kwa kudanganya dunia kwa kutoa taarifa za upotoshaji kuhusu wawekezaji, Serikali na wadau wengine wanaotetea haki za jamii ya Loliondo, kama Kidupo na Kata ya Oloipiri.

Sehemu ya pili ya waraka huu tutatoa mapendekezo yetu ya nini kifanyike ili kurejesha na kuimarisha hali ya amani ya utulivu katika Tarafa ya Loliondo na Wilaya ya Ngorongoro kwa jumla.
 

Atuzwa kwa kuisumbua Serikali (2)​

Jamhuri June 22, 2016
Sehemu iliyopita, viongozi wawili katika Tarafa ya Loliondo waliandika waraka kupinga hatua ya Maanda Ngoitiko ambaye ni kiongozi wa asasi ya Pastoral Women Council (PWC), kupewa tuzo ya Front Line Defenders Award for Human Rights inayotolewa na Shirika la The International Foundation For the Protection of Human Rights Defenders at Risk mjini Dublin, Ireland.

Wanapinga kwa maelezo kuwa Maanda amekuwa sehemu ya migogoro inayoendelea Loliondo kutokana na kupinga mambo mengi yanayofanywa na Serikali. Sehemu hii ya pili wanatoa mapendekezo wanayoamini yatasaidia kurejesha hali ya amani, utulivu na utangamano Loliondo.

Mapendekezo yetu
Ili kukabiliana na tatizo la mifugo mingi kuzidi uwezo wa ardhi (carrying capacity), vijiji vya kata ya Oloipiri vinaiomba Serikali ichukue jukumu la kuhakiki mipaka ya vijii ili tuweze kutengeneza mipango ya matumizi bora ya ardhi na pia kupata vyeti vya vijiji na hatimaye kudhibiti uhamiaji haramu kutoka nchi jirani ya Kenya na vijiji vya kata zinazotuzunguka.

Ipo haja kwa Serikali kuangalia upya migongano ya sheria kuhusu ardhi na kurejea Sheria ya Wanyamapori, lakini vijiji vilazimishwe kufanya mipango ya matumizi bora ya ardhi ili kulinda na kuendeleza uhifadhi wa mazingira kwa manufaa ya vizazi vya leo na vijavyo.

Kwa muda mrefu sasa Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imekuwa ikizuia wafugaji kupeleka mifugo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Ingawa tunakuabiliana na uzuizi huo kwa madhumuni ya kulinda mazingira na kuzuia ujangili, bado tunashauri wizara kujaribu kuruhusu wafugaji kuchunga katika eneo hilo katika kile kipindi cha kiangazi ambacho hakuna watalii wengi wanaotembelea hifadhi na wanyama wamehama katika mbuga hiyo, na wamehamia maeneo ya Hifadhi ya Maasai Mara na badala ya kutumia utaratibu wa kuchoma nyasi mbugani (controlled burning), wawaruhusu kwa utaratibu maalumu wafugaji wa vijiji vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kufanya malisho.
Kwa kufanya hivi kutapunguza malalamiko kutoka kwa wafugaji na pia mifugo inaweza kabisa kuchangia pato la taifa kwa kiwango kikubwa kama mifugo itauzwa wakati muafaka, kama vile nchi za Botswana, Kenya na nchi nyingi za Afrika zinavyofaidika kutokana na mazao yatokanayo na mifugo kama nyama, ngozi na maziwa.

Serikali ichukue jukumu la kutoa onyo na hata adhabu kali pale inapostahili kwa viongozi wa mashirika haya yasiyo ya kiserikali ambayo yamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha hakuna uhusiano chanya kati ya jamii na wawekezaji kwa manufaa yao binafsi.

Tunapendekeza kata na vijiji vyetu kufanya kazi na wawekezaji waliopo katika kata zetu na hata wale watakaojitokeza kutaka kuwekeza katika maeneo yetu yenye rasilimali zinazoweza kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa wananchi wetu.

Tunaomba Serikali itusaidie kuwadhibiti wale wote watakao kuwa na madhumuni ya kuchafua kata zetu, kuwachafua wawekezaji wetu kupitia vyombo vya habari, mitandao na tovuti maana NGOs wamekuwa wakituharibia uhusiano wetu na wawekezaji.

Kwa ufupi, tunakubali na kutambua uwepo wa wawekezaji na tunaomba Serikali iwalinde wawekezaji wazuri waliopo katika kata na vijiji kwa ajili ya kuwaletea maendeleo jamii za kifugaji ndani ya maeneo ya uwekezaji.

Tunaishauri Seriali kupitia vyombo vyake, kufanya uchunguzi wa kina kukagua (audit) haya mashirika (NGOs) kwa kufuatilia miradi waliyoombea pesa na kulinganisha kama miradi hiyo inaendana na pesa walizopata kutoka kwa wafadhili kama njia mojawapo ya kuwadhibiti na kuhakikisha fedha wazipatazo kutoka kwa wafadhili zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Faida kutoka kwa Wawekezaji
Ni dhahri kuwa picha ambayo dunia imekuwa nayo juu ya Loliondo ni ile ambayo imewekwa na wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo kwa kweli huweka sura hasi juu ya Tarafa ya Loliondo, kata na vijiji vyetu, lakini pia nchi kwa jumla.

Pia huu upotoshaji huenda kinyume cha jitihada za serikali za kukaribisha wawekezaji wenye tija kwa jamii kutoka pande mbalimbali za dunia.

Pia inaonesha dunia kuwa Loliondo ni eneo la hatari kwa wawekezaji na kwa sababu hii wawekezaji wengi wameamua kutoka katika maeneo yetu, kwa mfano, Nomads, Hoopoe, Buffalo n.k.

Kwa kuwa mashirika haya yamekuwa na nguvu sana na kusababisha kutujengea jina baya kwa tarafa yetu ya Loliondo na miradi mingi ya maendeleo imekuwa ikitoweka kwa ajili ya malumbano yanayosababishwa na Maanda Ngoitiko wa PWC na washirika wake, kwa mfano, mwaka 2010 Balozi wa Marekani alifanya ziara kwa mwekezaji wa Kimarekani kupitia TCL na alikuwa ametoa ahadi ya kuangalia ni jinsi gani kwa kushirikiana na wawekezaji wanaweza kusaidia kuwekeza kwenye ufugaji, lakini kwa kuwa shirika hili la PWC nia yake ni kuendeleza maslahi binafsi, walimwandika vibaya Balozi wa Marekani katika mitandao ya kijamii na kusababisha balozi huyo kujitoa katika mchakato huo.

Tungependa kueleza baadhi ya miradi iliyotekelezwa na wawekezaji katika maeneo yetu. Kwa mfano, kampuni ya OBC: Wamejenga Shule ya Sekondari Loliondo, upanuzi wa Hospitali ya Wasso na misaada ya vitanda, magodoro, blanketi, shuka, uchimbaji visima vya maji, ujenzi wa daraja la Mto Pololeti, ajira kwa vijana, ujenzi ofisi za vijiji vya Kirtallo, Soit-Sambu na uchangiaji wa madawati 200 katika shule za msingi wilayani Ngorongoro; na kadhalika.

Thomson Safaris: Wamejenga madarasa kwa shule za misingi, nyumba za walimu, mabweni kwa wavulana na wasichana katika Sekondari ya Soit-Sambu, ujenzi wa nyumba ya walimu wa Sekondari ya Soit-Sambu, ujenzi wa zahanati ya Sukenya, nyumba za watumishi wa zahanati, uchimbaji wa visima vya maji kwa ajili ya zahanati na miradi ya vikundi vya maendeleo ya akina mama (COCOBA) na kadhalika.

KIDUPO NGO: Ufadhili wa wanafunzi wa shule za msingi, sekondari; na wa vyuo na ujenzi wa shule za misingi ya Orkuyane na Mama Sara Lopolun.

Tunasisitiza kuwa matatizo yatakapojitokeza ni sharti yatatuliwe na wananchi kwenye vijiji na kata husika, na siyo Maanda Ngoitiko na shirika lake kuyasemea au kujaribu kuyatatua kwa maslahi yao binafsi.

Tunasisitiza kuwa hatupo tayari tena kutengenezewa migogoro na Maanda Ngoitiko na shirika lake la PWC dhidi ya Serikali na wananchi, dhidi ya wawekezaji na wananchi, dhidi ya koo na koo, dhidi ya kijiji na kijiji na pia dhidi ya NGO na NGO.

Hivyo, tunawaomba viongozi wetu wa Serikali kuhakikisha kwamba tunalindwa katika jitihada zetu za kupata amani na kutafuta maendeleo endelevu kwa manufaa ya wananchi wetu.

Imeandaliwa na:
Diwani wa Kata ya Oloipiri, Wilaya ya Ngorongoro
Mheshimiwa William M. Alais na
Mkurugenzi wa Shirika la KIDUPO (Integrated Development Peoples’ Organization) – Ndugu Gabriel K. Olle Killel.
 
Back
Top Bottom