Wakenya tushukuru Mungu kwa demokrasia yetu, watani wetu wamebanwa hadi wanalia toshaaa, wanakiri kwamba nchi yao sasa imekuwa 'Police State'

pingli-nywee

JF-Expert Member
Sep 16, 2015
11,923
13,344
Hii nayo ni hatari, Civil Society Organisations Director's Forum ambayo ni mkusanyiko wa mashirika 65 ya kitanzania ya haki za kibinadamu na kidemokrasia limeamua kupaza sauti liwe liwalo. Wanalalamika na kulilia dunia kwa kile ambacho wanakiita 'Police State' ambayo mzee mtakatifu kule ikulu ameibuka nayo kwa kukandamiza kabisa upinzani, wanahabari na uhuru wa wananchi wake. Wanasema kwa mwendo huu wa kuminya demokrasia na uhuru wa wapinzani kuwa na vikao vyao, amani ya nchi inavurugwa huku katiba ikinajisiwa na viongozi wanaotawala. Matokeo yake ni wananchi wanaoishi kwa uoga na kujihisi kwamba hawapo huru kwenye nchi yao. Wameangazia sanasana kutupwa selo kwa miezi mitatu kwa kiongozi mmoja wa upinzani, Mr. Freeman Mbowe. Kunani watani wetu watanzania? Mnanikumbusha enzi za Nyayo Kenya. Mbona mmebadilika kiasi hiki? Tuliwajua kwa ustaarabu wenu ila sasa sivyo tena. https://www.africanews.com/2019/04/...n-groups-risks-undermining-peace-in-tanzania/
 
Kenya ni nchi ya familia mbili zinagombana na kupata Kenyatta family na Jaramogi Odinga Oginga. Wengine manyumbu tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Boss umebofya hiyo link hapo na ukasoma taarifa yenyewe? Au umetangulia tu kutupia comment ya kishabik? Hii ni sifa mbaya sana kwa nchi yenu. Wakenya tumeishi kwenye hali kama hiyo ya 'police state' chini ya utawala wa rais mstaafu Daniel Arap Moi, almaarufu Nyayo. Usitamani kuyaona yale ambayo sisi tuliyashuhudia. Wazazi wetu wakivamiwa usiku wa manane na kuzabwa makofi, huku wakinyanyuliwa juu kwa juu na kutupwa kwenye landcruiser na kutawacha tukijiuliza kama ndio itakuwa siku yetu ya mwisho ya kuwaona kwa macho yetu mawili.
 
instagram-media-bv_2wogjunt-jpg.1066195
 
Nani watani zenu? Kama ni sisi hatuna utani na taifa lisilojielewa, halina hata umoja wa kitaifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tuna matitizo yetu ila kwa miaka miwili sasa tumeona mambo yakibadilika na siasa za chuki zikitupiliwa mbali. Wapinzani na wenzao serikalini wanaonana macho kwa macho na kuketi kwenye vikao pamoja hata nje ya bunge. Ushabik wa vyama vya kisiasa nao, kwenye masuala muhimu ya nchi, haupo tena. Ustaarabu umeshamiri na ubaguzi wa aina yoyote ule umefifia.
 
Hii nayo ni hatari, Civil Society Organisations Director's Forum ambayo ni mkusanyiko wa mashirika 65 ya kitanzania ya haki za kibinadamu na kidemokrasia limeamua kupaza sauti liwe liwalo. Wanalalamika na kulilia dunia kwa kile ambacho wanakiita 'Police State' ambayo mzee mtakatifu kule ikulu ameibuka nayo kwa kukandamiza kabisa upinzani, wanahabari na uhuru wa wananchi wake. Wanasema kwa mwendo huu wa kuminya demokrasia na uhuru wa wapinzani kuwa na vikao vyao, amani ya nchi inavurugwa huku katiba ikinajisiwa na viongozi wanaotawala. Matokeo yake ni wananchi wanaoishi kwa uoga na kujihisi kwamba hawapo huru kwenye nchi yao. Wameangazia sanasana kutupwa selo kwa miezi mitatu kwa kiongozi mmoja wa upinzani, Mr. Freeman Mbowe. Kunani watani wetu watanzania? Mnanikumbusha enzi za Nyayo Kenya. Mbona mmebadilika kiasi hiki? Tuliwajua kwa ustaarabu wenu ila sasa sivyo tena. https://www.africanews.com/2019/04/...n-groups-risks-undermining-peace-in-tanzania/
Chalenge ya vyama ilishawashinda mkaamuua kuweka hand shake na now your are practically one part state lead by two dynastes
 
Hii nayo ni hatari, Civil Society Organisations Director's Forum ambayo ni mkusanyiko wa mashirika 65 ya kitanzania ya haki za kibinadamu na kidemokrasia limeamua kupaza sauti liwe liwalo. Wanalalamika na kulilia dunia kwa kile ambacho wanakiita 'Police State' ambayo mzee mtakatifu kule ikulu ameibuka nayo kwa kukandamiza kabisa upinzani, wanahabari na uhuru wa wananchi wake. Wanasema kwa mwendo huu wa kuminya demokrasia na uhuru wa wapinzani kuwa na vikao vyao, amani ya nchi inavurugwa huku katiba ikinajisiwa na viongozi wanaotawala. Matokeo yake ni wananchi wanaoishi kwa uoga na kujihisi kwamba hawapo huru kwenye nchi yao. Wameangazia sanasana kutupwa selo kwa miezi mitatu kwa kiongozi mmoja wa upinzani, Mr. Freeman Mbowe. Kunani watani wetu watanzania? Mnanikumbusha enzi za Nyayo Kenya. Mbona mmebadilika kiasi hiki? Tuliwajua kwa ustaarabu wenu ila sasa sivyo tena. https://www.africanews.com/2019/04/...n-groups-risks-undermining-peace-in-tanzania/
Nyie multiparties mmeshaiua boss kwani hujui!!!!!!!!!
 
Nyie mnademocrasia au mnavutwa na ukabila? Ukabila ndo unaoendesha Siasa za Kenya, mengine kelele tu
Kenya rais na viongozi wengine wanakashifiwa, wanakosolewa na hata wanatusiwa hadharani, na maisha yanaendelea tu. Sio kila siku kusifia na kuendeleza miungu watu. Hilo ni jambo hatari sana kwenye utawala wowote ule ambao hauheshimu katiba walioapa kuilinda.
 
Nyie multiparties mmeshaiua boss kwani hujui!!!!!!!!!
Chalenge ya vyama ilishawashinda mkaamuua kuweka hand shake na now your are practically one part state lead by two dynastes
Itakuwa labda hujui chochote kuhusu siasa za Kenya. Kuna hadi wapinzani ndani ya chama tawala, ambao hawakomi kumkashifu rais kwa lolote afanyalo na wala hawatishiki. Tena kwenye upinzani, ambao ulikuwa ni muungano wa vyama, kuna vyama ambavyo havikumfata Raila na ile handshake yake na rais U.K. Watu kama Musalia Mudavadi na Moses Wetangula. Upinzani Kenya bado upo imara na zaidi ya yote hawakandamizwi na yeyote yule.
 
Acha wabanwe kabisa si wanapenda kulala fofofo

Huwa siwaonei huruma, wanafaa kubanwa ipasavyo had watie akili, yaani kwao chama kinataka kufutwa kisa baadhi ya wafuasi waliitika neno 'takbir', halafu spika anamvuruga CAG kisa CAG amesema udhaifu wa bunge, yaani kule spika huwa na uwezo wa kuagiza polisi wamkamate yeyote, polisi kwao huchezewa chezewa kfuata maagizo na amri ya kila mkulu, iwe mkuu wa wilaya, waziri, mkuu wa mkoa kila mmoja wao anaamrisha amrisha polisi wamkamate nani na akae lockup siku ngapi.
 
Boss umebofya hiyo link hapo na ukasoma taarifa yenyewe? Au umetangulia tu kutupia comment ya kishabik? Hii ni sifa mbaya sana kwa nchi yenu. Wakenya tumeishi kwenye hali kama hiyo ya 'police state' chini ya utawala wa rais mstaafu Daniel Arap Moi, almaarufu Nyayo. Usitamani kuyaona yale ambayo sisi tuliyashuhudia. Wazazi wetu wakivamiwa usiku wa manane na kuzabwa makofi, huku wakinyanyuliwa juu kwa juu na kutupwa kwenye landcruiser na kutawacha tukijiuliza kama ndio itakuwa siku yetu ya mwisho ya kuwaona kwa macho yetu mawili.
Wapinzani Tz ni chini ya alfu tano..Wote waliompigia kura lowassa wapo sasa Sisiemu..Unawao waongelea ni wadau wa mitandao kama mange kimambi na miguna miguna..Takataka tuu
 
Wapinzani Tz ni chini ya alfu tano..Wote waliompigia kura lowassa wapo sasa Sisiemu..Unawao waongelea ni wadau wa mitandao kama mange kimambi na miguna miguna..Takataka tuu
Sawa, umetia saini kwenye register na maoni yako tumeyasikia. Hebu sasa wapishe wenye nchi, wanaojielewa, nao watoe maoni yao pia.
 
Nchi haiwezi endeshwa kwa masilahi ya watu chini ya alfu tano eti sababu wanapiga kelele sana kwa mitandao..kelele lazima wapige na kazi lazima pia iendelee
Bofya kwenye hiyo link hapo juu kwanza, kisha soma taarifa kwa umakini. Alafu ndio urejee upya, naona ni kama unaongea kuhusu masuala tofauti na yanayojadiliwa hapa.
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom