Chamoto
JF-Expert Member
- Dec 7, 2007
- 8,319
- 17,473
Leo nikiwa nimepumzika nikaamua kuingia JF kusoma mada mbalimbali na moja ya mada zilizonishangaza ni ile ya ujenzi wa bwawa la umeme mto mara. Nimeshangaa jinsi Wakenya wanavyo jitutumua kwa nini wajenge bwawa huku wakitulalamikia sisi kutotaka wao kujenga. Moja ya hoja ya msingi iliyoelezwa na wadau ni ile ya kuharibu mazingira, kutokana na ecosystem ya Serengeti kutegemea mto mara.
Tukirudi nyuma, miaka michache iliyopita watu wa mkoa wa mara walitaka kujengewa barabara kuelekea Musoma kupitia mbuga ya Serengeti, kupunguza umbali wa safari ukilinganisha na huu ya sasa. Wakenya walipiga kelele sana, wakizunguka dunia nzima kupinga hiyo barabara isijengwe kwasababu za kimazingira ikiwa ni pamoja na kusumbua wanyama ambao huenda hadi Kenya.
>>> Wakenya waanza kulialia baada ya tanzania kuthibitisha kuanza ujenzi wa barabara kupitia serengeti
>>> Nyie kenya ujenzi wa barabara mbuga ya serengeti nini tatizo
Cha kushangaza leo wameanzisha mpango wa kujenga bwawa la kuzalisha umeme mto Mara na Tanzania imekuwa ikipinga kuwa bwawa hilo litaharibu ecosystem ya serengeti. Sasa kama mlipinga barabara yetu kujengwa kwasababu ya mazingira inakuwaje leo msiwe rafiki wa hayo mazingira kwa kujenga bwawa mbugani?
Tukirudi nyuma, miaka michache iliyopita watu wa mkoa wa mara walitaka kujengewa barabara kuelekea Musoma kupitia mbuga ya Serengeti, kupunguza umbali wa safari ukilinganisha na huu ya sasa. Wakenya walipiga kelele sana, wakizunguka dunia nzima kupinga hiyo barabara isijengwe kwasababu za kimazingira ikiwa ni pamoja na kusumbua wanyama ambao huenda hadi Kenya.
>>> Wakenya waanza kulialia baada ya tanzania kuthibitisha kuanza ujenzi wa barabara kupitia serengeti
>>> Nyie kenya ujenzi wa barabara mbuga ya serengeti nini tatizo
Cha kushangaza leo wameanzisha mpango wa kujenga bwawa la kuzalisha umeme mto Mara na Tanzania imekuwa ikipinga kuwa bwawa hilo litaharibu ecosystem ya serengeti. Sasa kama mlipinga barabara yetu kujengwa kwasababu ya mazingira inakuwaje leo msiwe rafiki wa hayo mazingira kwa kujenga bwawa mbugani?