Jaguar: Wakenya kuwaondoa kwa kipigo Watanzania, Wachina, Waganda na Wapakistani nchini mwao

Wewe hapo kwa kuvimbiwa makande una ubavu gani wa kuvua uanachama wa Kenya kwenye huu muungano, ifahamike asilimia 40% ya uchumi wa EAC umemilikiwa na Kenya, hivyo nchi hii ndio baba ukanda huu, hamna anayeweza kumfukuza baba nyumbani.
Narudia tena, hizo ni kauli za mwanasiasa ambaye ameishiwa, anafahamu uchaguzi unakaribia, ndio anatafuta jinsi ya kutibua apate kiki, haya mataifa tunategemeana na hakuna mwenye ubavu wa kumfurusha mwenzie, rais wetu alishalitambua hilo na akaamrisha wana EAC wote waje na kujihisi Wakenya, wamiliki biashara na kila watakachoweza, hapa kwangu mtaani getini duka la kwanza ni la Mtanzania, familia yangu inategemea duka lake kwa bidhaa nyingi tu na haijawahi tokea sku hata moja tukawaza Utanzania wake, cha msingi ukiwa na hela, nenda dukani kwake, nunua ulichkifuata piga stori, sepa zako kafanye mengine.
Pembeni hapa kuna jengo lenye vyumba vya kupanga, yaani apartments, mali ya Mchagga fulani raia wa Tanzania, hapo amewekeza na anategemewa kwa njia moja au nyingine.

Hivyo muendelee kuropokwa na kutokwa povu ni ruksa, lakini mwisho wa siku kila mmoja wetu ataishia kitandani usiku na kukoroma, lakini uhusiano baina ya haya mataifa upo pale pale, raia tunahusiana na kufanya biashara.
boss bado unakaa mwiki au ulishahama?
 
Nimemsikia, lakini kama hakuna kiongozi yeyote was Kenya aliyekemea kauli hiyo basi tusishangae yale ya Afrika kusini kutokea hapo Kenya.
Ila yakitokea hayo hakuna wakupona maana nao wakenya wako huku kwa wingi sana
Siku moja moja kumbe huwa unaacha ukibendera wako
Leo umeongea
 
Ndio hawa Wamejazwa kwa magari ya council wanakuja
 

Attachments

  • YOUme2CWz5ssE5Q8XhQXe1WZUpcEmyhDjsLnVjUO1vvO2g8zG6cj_RJJSfhNW2j3kUMoDevDRjfAsW5A-udp0zyPG5nj1...jpeg
    YOUme2CWz5ssE5Q8XhQXe1WZUpcEmyhDjsLnVjUO1vvO2g8zG6cj_RJJSfhNW2j3kUMoDevDRjfAsW5A-udp0zyPG5nj1...jpeg
    13.8 KB · Views: 22
Hilo tamko,limetolewa na mbunge wao,na amelitoa kisiasa zaidi.
Watu wenye maisha magumu,siku zote huwa wanatafuta wa kumtwisha lawama kutokana na umaskini wao.
Sasa jiulize,mpakistan,aliyeingia Kenya,na mtaji wake wa mabilioni ya dola,akafungua show room,amesababisha vipi umaskini wa wananchi wa kawaida?hata akiondoka huo umaskini hauishi zaidi utaongezeka maana ajira alizokuwa anatoa,zitasitishwa.
Watakao umia ni wale wageni wanaomiriki biashara ndogo,kama za maduka,
MTz anayemiriki kampuni kama ya IT,tena imeajiri wakenya kibao,unaanzia wapi kumgusa?huyo anaweza kuguswa tu na sera za nchi kama zikibadirika

Kwa bahati mbaya sana historia inaendelea kudhihirisha ni namna gani wanasiasa wenye maono mafupi na uchu wa madaraka wametumia umasikini wa wananchi wao kuendeleza kujikweza na kuziba ombwe lao la "uongozi". Wamekuwa wakitafuta wakuwatupia lawama na kuchochea ubaguzi, ilhali ni uongozi wao duni ndio unaongeza matatizo kwa wananchi. Mwisho wa siku wanaongeza matatizo juu ya matatizo na kujakuondolewa kwa aibu na dhahma. Mwisho wake tutauona tu, time will tell.
Kina Mugabe, Mobutu, Idd Amin, nk. walijaribu huo mchezo, na mwisho wao tunaufahamu.
 
Kama nakumbuka vizuri baada ya Jiwe kuapishwa kama rais alianza kwa kuwafurusha wakenya huko Tz. Siungi mkono tamko la Jaguar, kwa maoni yangu, wale ambao sio waafrika ndio tunafaa kuwafurusha. Omba omba wa kitanzania wametapakaa kwenye miji ya Kenya. Machangudoa na wachuuzi pia kutoka Tz wapo wengi sana Kenya ila wakenya huwa hawana bifu nao.
Hao wanaomsupport jaguar na vigelegele sio wakenya hao, eti wakenya hawana bifu nao
 
Sijawahi kuona umuhimu wa hii jumuiya, bora tuunde jumuiya nyingine iwe na watu kama hawa wanatumia bandari yetu
-Uganda
-Congo
-Burundi
-Rwanda
-Zambia

Hili limetokea, aliyesema hivyo ni kiongozi - mbunge. Sijui kama kuna kauli yeyote imetolewa na viongozi wa nchi yetu kulaani hilo tamko, au wanasubiri hali iwe mbaya ndo wajitpkeze.
 
Wakuu nimeanzisha huu uzi kwa ajili ya kupinga ubaguzi wa wazi wazi aliounyesha Jaguar dhidi ya Wa Tanzania na Waganda waishio Kenya.Hivyo nawaomba tufute kabisa nyimbo za huyu jamaa kwenye simu, computer au tablet. Na pia tuviombe vyombo vyetu pendwa kutokupiga nyimbo zake.
NAOMBA KUWASILISHA
 
niliwahi kusema hapa nikaambulia matusi kwamba Kenya muda huu inawafukuza watanzania saa nyingine kuwachania permit na passport watanzania waishio Kenya,
Malalamiko haya niekuwa nayakuta ofisi mbali mbali na tuliahidi suala hili kulifanyia kazi
 
Yule mwehu '' Ana hamasisha chuki dhidi ya Mataifa hays mawili ambayo Yana muda mrefu sasa tangu yaamue kuwa na Ushirikiano kama ndugu ---

Yule ni moja ya viongozi wa ajabu kabisa ambao nimepata kuwashuhudia
 
Back
Top Bottom