Wake zetu na Ma-house girls, Kulikoni?

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Wana-jf sina uhakika kama hili lilishawahi kuzungumzwa hapa au la. Lakini nimeona si vibaya tukalijadili na kuchangia mawazo. Ndugu yangu mmoja hakumaliza wikiendi yake vizuri jana. Kisa ni kuwa mke wake amechachamaa anataka house girl aondoke haraka. Kwa maelezo ya huyo ndugu yangu ni kuwa jumamosi ya juzi binti wa kazi aliomba ruhusa kwa mother house kwenda kusuka nywele tangu alipoondoka saa 4 asubuhi akarudi saa 11 jioni. Mother house alipomuuliza binti kulikoni kachelewa vile akadai kuwa msusi alikuwa na kazi nyingi na wateja wa kusuka walikuwa wengi so alilazimika kusubiri. Mother house hataki anasema binti ameshakuwa na kiburi so akiondoka anarudi muda anaotaka. Jamaa amejaribu kumsihi mkewe amsamehe huyo binti kwa kuwa kwanza hana uhakika wa kupata h/girl mwingine kwa haraka na ukizingatia wana watoto wadogo wa kati ya miaka 5 na 2. Mother house amepamba moto kwa nini jamaa anapinga binti kuondolewa au yeye ndio anayempa kiburi may be kashamuonja so kanogewa hataki aondoke. Kwa kweli jamaa kila akifikiria busara ya kumfukuza binti ukizingatia yeye na mkewe wote ni wafanyakazi haelewei kilichompata mkewe. Na kibaya zaidi mother house kampigia simu mpaka mama yake mzazi ( mama wa mother house) kuwa yeye muda wowote atarudi kwao kwa kuwa jamaa anapinga binti wa kazi kuondolewa kwa kuwa eti huenda anampenda sana h/girl kuliko kusikiliza ushauri wa mkewe. Ndani ya nyumba hakuna amani kisa msichana wa kazi.. Jamani hii vipi? FL, Nyamayao, Pretty na wadada/wamama wengine ndivyo mlivyo au??
 
Mke asiyejiamini hawezi kumwamini mwenza wake. PERIOD!!! wasi wasi tuuuuuu!!! sukari itashuka bure kwa sababu ya upuuzi.
 
huyo mwanamke kwanza hajiamini, pili suala la kuchelewa kwa msusi hilo liko wazi kabisa, kama huna appointment lazima masaa si chini ya saba yakukute huko, na huyo mama lazima analijua hilo, hapo alikuwa anatafuta sababu ya kumfukuza dada wa watu
 
Nafikiria tofauti. Mkeo atakuamini iwapo wewe mwenyewe ni mwaminifu. Sasa jamani, housegirl ni msaidizi wa mama. baba, unapokataa asiondoke maana yake nini? mimi sihitaji permission ya mume ku-fire house girl(though wangu ana ruhusa ya kutoka every sunday, asije nchukulia l'azizi wangu eh!)
 
Nafikiria tofauti. Mkeo atakuamini iwapo wewe mwenyewe ni mwaminifu. Sasa jamani, housegirl ni msaidizi wa mama. baba, unapokataa asiondoke maana yake nini? mimi sihitaji permission ya mume ku-fire house girl(though wangu ana ruhusa ya kutoka every sunday, asije nchukulia l'azizi wangu eh!)
hahahahahaaaa!!
 
Nafikiria tofauti. Mkeo atakuamini iwapo wewe mwenyewe ni mwaminifu. Sasa jamani, housegirl ni msaidizi wa mama. baba, unapokataa asiondoke maana yake nini? mimi sihitaji permission ya mume ku-fire house girl(though wangu ana ruhusa ya kutoka every sunday, asije nchukulia l'azizi wangu eh!)
..Kwa hiyo wewe hakuna kushauriana na mumeo kuhusu kuleta au kumuondoa h/girl? Kutoka kila sunday ni nzuri najua ki-saikolojia binti inamuweka vizuri kama anakwenda kupata huduma za kawaida kama binadamu aliyekamilika. Ukizingatia anakula vizuri na kuchoka sana mwili unakusanya protini kweli kweli so lazima apate mahali pa kutolea...
 
Nafikiria tofauti. Mkeo atakuamini iwapo wewe mwenyewe ni mwaminifu. Sasa jamani, housegirl ni msaidizi wa mama. baba, unapokataa asiondoke maana yake nini? mimi sihitaji permission ya mume ku-fire house girl(though wangu ana ruhusa ya kutoka every sunday, asije nchukulia l'azizi wangu eh!)
what makes wives jump into conclusions that wame zao wanatembea na h/g? kwa sababu wamecoment kuhusu h/g? au sababu nini hasa?
Kama mmeo anaona unataka kufanya irrational decission, kitu ambacho anajua kitakuletea shida mbeleni, asikuwambie wala kuku-advisi?
 
ni kweli hizi ishu za wamama/hgal huwa ni nyingi tu, me naweza kusema kila upande una tatizo!...tukiangalia kama hili, kwani kama msusi ameona ana watu wengi c angepanga na msuc arudi baadae ili arudi home kusaidia kazi mbili/tatu? japo c ishu ya kumuondoa lakini pia ukizembea vitu vidogo vidogo kama hivi ndio wanakuja kukupanda kichwani, mie naonaga bora hboy kwa kweli, nipo nae miaka sasa tunaenda sawa, tatizo la hgal ukimchukua mbichi akushavunja ungo na kuanza kupendeza tu tabu inaanza...mama/hgal wote wanakuwaga na kasheshe zao.
 
Well, usigenerolaiz kiviiilee, ila bado kuna kitu ninakikosa, ni kuchelewa mara moja ndio kumezua kizazaa au imeshakuwa tabia? Na huyo faza house, utetezi mara moja ndio nao umezua utata au kila ikiibuliwa issue ya mdada wa kazi bendera ya utetezi inapandishwa?

Anywayz, issue za wadada vs mama wenye nyumba, naomba niiite binafsi kama ni a bit complex. Kwanini, yote kama ilivyo kati ya relationship yeyote, ni suala la kuchukuliana na kuvumiliana. Ni yapi mtu anajiandaa kwa kuyabeba kama yalivyo na ni yapi yanatosha kumfanya mtu aigeuze nyumba juu chini kwa kugomba! Kama ni one off case, bado kuna suala la kukumbushana na kuonyana kuonyesha ni tabia gani hazikubaliki ndani ya nyumba. Lakini kama masikio yanawekwa pamba, then hatua zaidi zitachukuliwa kutegemeana na tabia inayokatazwa. Huko makanisani/misikitini si bado tunakumbushwa mara kadhaa kuhusu kutenda mambo mema? Kuna siku viongozi wa ibada waliwahi kusema..'sasa kwenye issue ya dhambi nafikiri tumemaliza, kuanzia leo tutakuwa tunaongelea habari mpya ya kumpenda jirani!'?

Hapa linakuja suala la mtu na mtu sasa! Kuna mwingine ambaye kwake huna nafasi ya kufanya kosa, kosa lolote lile linamfungisha dada virago! Wakati wengine wana moyo wa subira, akiona havivumiliki ndio atamruhusu dada aende zake. Ila ambalo ninaweza kukuhakikishia ni kuwa, kama binadamu yoyote alivyoumbwa, bearing in mind kuwa wadada nao ni binadamu, kuna wadada wana jeuri, wala usitake kusikia.

Kama huyo dada mbona issue yake rahisi, kwani hajui mdada wake anasuka wapi? si angeweza kupata uhakika tika huko kabla ya kwenda mbali kiasi cha kutaka kumwingiza na faza hauz kwenye mkumbo huo? Manake saa nyingine huwa tukikaa individually, surely huwa tunajiuliza, hivi mimi ndiye niliyepayuka yote yale?
Ni mtazamo tu.
 
Well, usigenerolaiz kiviiilee, ila bado kuna kitu ninakikosa, ni kuchelewa mara moja ndio kumezua kizazaa au imeshakuwa tabia? Na huyo faza house, utetezi mara moja ndio nao umezua utata au kila ikiibuliwa issue ya mdada wa kazi bendera ya utetezi inapandishwa?

Anywayz, issue za wadada vs mama wenye nyumba, naomba niiite binafsi kama ni a bit complex. Kwanini, yote kama ilivyo kati ya relationship yeyote, ni suala la kuchukuliana na kuvumiliana. Ni yapi mtu anajiandaa kwa kuyabeba kama yalivyo na ni yapi yanatosha kumfanya mtu aigeuze nyumba juu chini kwa kugomba! Kama ni one off case, bado kuna suala la kukumbushana na kuonyana kuonyesha ni tabia gani hazikubaliki ndani ya nyumba. Lakini kama masikio yanawekwa pamba, then hatua zaidi zitachukuliwa kutegemeana na tabia inayokatazwa. Huko makanisani/misikitini si bado tunakumbushwa mara kadhaa kuhusu kutenda mambo mema? Kuna siku viongozi wa ibada waliwahi kusema..'sasa kwenye issue ya dhambi nafikiri tumemaliza, kuanzia leo tutakuwa tunaongelea habari mpya ya kumpenda jirani!'?

Hapa linakuja suala la mtu na mtu sasa! Kuna mwingine ambaye kwake huna nafasi ya kufanya kosa, kosa lolote lile linamfungisha dada virago! Wakati wengine wana moyo wa subira, akiona havivumiliki ndio atamruhusu dada aende zake. Ila ambalo ninaweza kukuhakikishia ni kuwa, kama binadamu yoyote alivyoumbwa, bearing in mind kuwa wadada nao ni binadamu, kuna wadada wana jeuri, wala usitake kusikia.

Kama huyo dada mbona issue yake rahisi, kwani hajui mdada wake anasuka wapi? si angeweza kupata uhakika tika huko kabla ya kwenda mbali kiasi cha kutaka kumwingiza na faza hauz kwenye mkumbo huo? Manake saa nyingine huwa tukikaa individually, surely huwa tunajiuliza, hivi mimi ndiye niliyepayuka yote yale?
Ni mtazamo tu.
 
haaa na sie kina mama jamani kuna vitu inabidi tuwe tunafikiria wakati mwingine . kama wewe unaweza kwenda saloon na kuchelewa kutoka vilevile kwani house gal yeye saloon ni yake ?
Pia labda kadada kamekuwa na hicho kijitabia mala nyingi na kinapata utetezi toka kwa faza hause tutajuaje ?
 
jamani wake zetu sometime mh! mi sikumoja nilikuwa na wife h-girl akapita nikatania tu wife huyu h-girl kanapendeza ckuizi. u cant believe kesho alisafirishwa kwao no comment nikijitetea ni utani tu my wife wangu jibu nilopewa nyie wanaume amna utani kwenye hilo. so jamaa kama wife ataki h-g mwache kuepuka lawama
 
..Kwa hiyo wewe hakuna kushauriana na mumeo kuhusu kuleta au kumuondoa h/girl? Kutoka kila sunday ni nzuri najua ki-saikolojia binti inamuweka vizuri kama anakwenda kupata huduma za kawaida kama binadamu aliyekamilika. Ukizingatia anakula vizuri na kuchoka sana mwili unakusanya protini kweli kweli so lazima apate mahali pa kutolea...

Naweza kudiscuss nae issue, atatoa opinions. But decisions zote about hgeli ni juu yangu. badala ya ku-discuss jinsi gani ya kuboresha penzi letu na kujiongezea maendeleo, we cant waste our precious time to discuss hgeli, mtu ambaye anaweza akakuamsha alfajiri kukuambia naondoka zangu! Hata talaka ina notice!
 
Nafikiria tofauti. Mkeo atakuamini iwapo wewe mwenyewe ni mwaminifu. Sasa jamani, housegirl ni msaidizi wa mama. baba, unapokataa asiondoke maana yake nini? mimi sihitaji permission ya mume ku-fire house girl(though wangu ana ruhusa ya kutoka every sunday, asije nchukulia l'azizi wangu eh!)

Hapo nakuunga mkono kwa asilimia mia moja. Jamani kina Baba tusiingilie mambo ya Mama na House-girl yatakukuta mabaya. Kwanza kabisa hata siku moja Baba huruhusiwi kutafuta house-girl na kumuajiri na sikuzote Mama ndiyo mwenye nyumba Baba utakapojifanya mjuaji ukiachiwa nyumba yatakushinda.
MAMA NDIE MWENYE MAMLAKA YA KUMUAJIRI NA KUMFUKUZA HOUSE-GIRL unaposikia kuna maamuzi magumu wakati mwingine ndio kama hayo ingekua House-boy Baba anamfukuza Mama hataki Baba angechukuliaje hali hiyo?
 
Naweza kudiscuss nae issue, atatoa opinions. But decisions zote about hgeli ni juu yangu. badala ya ku-discuss jinsi gani ya kuboresha penzi letu na kujiongezea maendeleo, we cant waste our precious time to discuss hgeli, mtu ambaye anaweza akakuamsha alfajiri kukuambia naondoka zangu! Hata talaka ina notice!

What if ni house boy?
 
Hapo nakuunga mkono kwa asilimia mia moja. Jamani kina Baba tusiingilie mambo ya Mama na House-girl yatakukuta mabaya. Kwanza kabisa hata siku moja Baba huruhusiwi kutafuta house-girl na kumuajiri na sikuzote Mama ndiyo mwenye nyumba Baba utakapojifanya mjuaji ukiachiwa nyumba yatakushinda.
MAMA NDIE MWENYE MAMLAKA YA KUMUAJIRI NA KUMFUKUZA HOUSE-GIRL unaposikia kuna maamuzi magumu wakati mwingine ndio kama hayo ingekua House-boy Baba anamfukuza Mama hataki Baba angechukuliaje hali hiyo?

Haya mimi binafsi yamenikuta! Wife anamtimua HG eti kisa umesifia chakula kizuri ama kunyoosha nguo vizuri!

Akishamtimua tatizo linakuwa kupata mwingine na may be kind na hardworking kama yule wa mwanzo! Matokeo yake mnakaa muda bila mfanyakazi na nyote mnafanya kazi, hamshindi nyumbani. what do you do kama mna mtoto? Wife aombe likizo kwa muda alee mtoto kisa kamtimua HG kwa kuhisi unakula mzigo?
 
ni kweli hizi ishu za wamama/hgal huwa ni nyingi tu, me naweza kusema kila upande una tatizo!...tukiangalia kama hili, kwani kama msusi ameona ana watu wengi c angepanga na msuc arudi baadae ili arudi home kusaidia kazi mbili/tatu? japo c ishu ya kumuondoa lakini pia ukizembea vitu vidogo vidogo kama hivi ndio wanakuja kukupanda kichwani, mie naonaga bora hboy kwa kweli, nipo nae miaka sasa tunaenda sawa, tatizo la hgal ukimchukua mbichi akushavunja ungo na kuanza kupendeza tu tabu inaanza...mama/hgal wote wanakuwaga na kasheshe zao.


Houseboys wanabaka watoto, watch out!!!
 
jamani wake zetu sometime mh! mi sikumoja nilikuwa na wife h-girl akapita nikatania tu wife huyu h-girl kanapendeza ckuizi. u cant believe kesho alisafirishwa kwao no comment nikijitetea ni utani tu my wife wangu jibu nilopewa nyie wanaume amna utani kwenye hilo. so jamaa kama wife ataki h-g mwache kuepuka lawama

Tehe tehe tehe nimeipenda hiyo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom