Wakazi wa Ubungo wampongeza Rais Kikwete kujenga barabara maeneo yao

Kwa nini apongezwe wakati ametekeleza majukumu yake kama rais na ahadi alizotoa?
 
Wanabodi,

Wakazi wa Ubungo pamoja na wakazi wa Jiji la Dar es Salam wamempongeza Rais Kikwete kwa kitendo chake kujenga barabara za Ubungo kupambana kupunguza foleni.

Serikali imetenga Sh10.5 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizo ili kupunguza msongamano wa magari barabara hizo ni pamoja na Mbezi Luis kupitia Goba mpaka Tanki Bovu, Mbezi kwa Yusuph, Msakuzi-Mpiji Magohe, Tegeta Bunju.

Nyingine ni Mbezi Malambamawili-Kinyerezi, Kimara-Mavurunza, Bonyokwa, Ubungo Maziwa-External, Kimara-Kilungule, Makoka, Makaburini, Kimara-Matosa, Mbezi, Ubungo-Msewe, Chuo Kikuu.

Wakazi hao wanasubiri usafari wa treni yenye uwezo wa kubeba abiria walioketi na kusimama wasiopungua 1,000 kila safari, hizo treni zitakuwa na vituo sita Buguruni, Tabata, Matumbi, Mabibo, Ubungo Maziwa.


Wana Ubungo wamempongeza Kikwete kwa kujenga Barabara...mara Serikali imetenga shilingi 10b kwa ujenzi wa Barabara hizo...

Hebu nyoosha Kiswahili, Barabara hizo ziko tayari au ni mwendelezo wa ahadi?
 
Ritz,

..Raisi anatakiwa asifiwe kwa mambo makubwa.

..hizo barabara za sh 10.5 billion waachiwe wabunge wa take credit.

..In this case tumpongeze John Mnyika ambaye mradi huo umewezekana akiwa mbunge.
 
Last edited by a moderator:
Naona upo katika harakati za kuganga njaa mkuu,,mh!chunga usichinje nyau maana hiyo njaa uliyo nayo balaa tupu!
 
Ritz,

Hivi Miradi hiyo ni kwa pesa ya nani hasa? za JK au wananchi? nataka tu kujua.

Mara nyingine kwa kudhani unamsaidia mtu kumbe unamsababishia matatizo, kwa zredi kama hii huyu mkaazi wa Ikulu atazidi kudharaulika na kuchukiwa. Don't ask me why.
 
Wamempongeza;
1.wapi (Kwani Mh. Rais wetu ametingwa na ratiba ya mikutano na safari za nje)?
2.lini?
3.kwa njia ipi(barua,televisheni/luninga,mihadhara) n.k?
4.Kwa mfano kama akipongezwa..haikupaswa kuwa majukumu yake?..nadhani hata kama ingekuwa ni pongezi zingekwenda kwa Mh. Mbunge wa Jimbo na Mh. Waziri husika!!!
 
Usiulize sana mkuu wangu. Hali ya maisha ya wananchi imeboreka. Hivi sasa wananchi wa kawaida wamejitahidi mpaka wameweza kujijengea majumba ya ghorofa. Maisha bora kwa kila Mtanzania. Kwanini wasimpongeze Rais wao?

Canon+4+WJC+107.jpg

hahahahahaha!!
Kikwete hoyeeee!!!

Barabara za Ubungo zinajengwa, pongezi kwa kikwete na shukrani nyingi.
Barabara za Kawe hazijengi, lawama ziende kwa mbunge wao. . .

Huo ndio ukenge wa mleta mada. Nafikiri mmenielewa.
 
Back
Top Bottom