Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,909
- 32,335
Wanabodi..
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ambaye ni kada wa chama cha mapinduzi CCM ameombwa na wakazi Musoma Mjini kugombea ubunge jimboni humo mwaka 2015.
Profesa Sospeter Muhongo, ni msomi na mzaliwa wa Musoma Mjini wakazi wa mkoa Mara wanasema wakati umefika wa kumpa ubunge Profesa Muhongo, kutokana na elimu yake pamoja na uzoefu wake ili hawatumikie wananchi wa Mkoa wa Mara.
Jimbo la Musoma Mjini kwa sasa linaongozwa na chama cha Chadema kupitia mbunge wake Vicent Nyerere.
Wakazi wengi wa Musoma Mjini wanaoneka kumkubali zaidi Prof Muhongo, kutoka utendaji wake wake katika Wizara ya Nishati na Madini..