TAMU YA LEO
Member
- Mar 26, 2020
- 8
- 3
Same
Wakazi wa kata ya Chome wanaoishi nje ya kata hiyo wameunga mkono jitihada za serikali kuboresha miundombinu ya barabara yenye urefu wa kilomita 15 baada ya serikali kutengeneza barabara ya Sanga Chome Kakoa kilomita 9 kati ya 24.
Hamad Waziri Hamad mkazi wa Chome alisema kuwa kutokana na barabara hiyo kutopitika kutokana na ubovu hususan kipindi cha mvua kumepelekea shughuli nyingi za kimaendeleo kukwama.
Alisema serikali ya awamu ya tano imekuwa na nia njema ya kuwajengea barabara kwa kilomita 9 kati ya 24 na hivyo wameona ni vyema kushiriki kwa kuongeza nguvu ili kuweza kuondoa changamoto hiyo.
''Wakazi waliopo nje ya hapa watachangia fedha na sisi tutajitoa kwa nguvu kazi lengo ni kuhakikisha tunaunga mkono jitihada za serikali kutuboreshea barabara yetu''alisema
Kwa upande wake Mhandisi Joseph Kakore ambaye ni mwakilishi wa wakazi wa Chome wanaoishi nje ya eneo hilo ambapo alisema umoja wao unaunga mkono jitihada za serikali kutatua kero hiyo kwani barabara hiyo ni muhimu kwa ustawi wa kata hiyo sanjari na kuchochea ukuaji wa kiuchumi.
Alisema barabara hiyo matengenezo ambayo yatahitajika ni pamoja na umwagaji wa vifusi vya moramu ujengaji wa mitaro na njia zakuchesha maji ambapo kazi zote zitaenda kwa ubia kati ya wakazi wanaoishi Chome na wale waliopo nje ya kata hiyo.
Napendael Mlay mtendaji kata ya Chome alisema kuna baadhi ya maeneo korofi likiwemo kituo cha afya Shengena hadi soko la kata na kuwa barabara hiyo ina mchango mkubwa hususan kufikisha huduma kwa wakazi wa kata hiyo.
Kwa mujibu wa mtendaji huyo barabara hiyo ambayo licha ya kufikakatika hifadhi ya taifa ya msitu wa Shengena vile vile ni kiungo muhimu kwa ustawi wa wakazi wa kata hiyo yenye wakazi zaidi ya 5000 ambapo kukamilika kwa barabara kutawezesha kurahisisha usafirishaji.
Meneja wa wakala wa barabara za mjini na vijijini (TARURA)wilaya ya Same mhandisi Felician Msangi alisema tayari ofisi yake itashirikiana na wadau hao kuhakikisha lengo lao linatimia na kuwa tayari upembuzi yakinifu ulishafanyika kwa ajili ya ujenzi katika kiwango cha changarawe.
Mwisho.
Wakazi wa kata ya Chome wanaoishi nje ya kata hiyo wameunga mkono jitihada za serikali kuboresha miundombinu ya barabara yenye urefu wa kilomita 15 baada ya serikali kutengeneza barabara ya Sanga Chome Kakoa kilomita 9 kati ya 24.
Hamad Waziri Hamad mkazi wa Chome alisema kuwa kutokana na barabara hiyo kutopitika kutokana na ubovu hususan kipindi cha mvua kumepelekea shughuli nyingi za kimaendeleo kukwama.
Alisema serikali ya awamu ya tano imekuwa na nia njema ya kuwajengea barabara kwa kilomita 9 kati ya 24 na hivyo wameona ni vyema kushiriki kwa kuongeza nguvu ili kuweza kuondoa changamoto hiyo.
''Wakazi waliopo nje ya hapa watachangia fedha na sisi tutajitoa kwa nguvu kazi lengo ni kuhakikisha tunaunga mkono jitihada za serikali kutuboreshea barabara yetu''alisema
Kwa upande wake Mhandisi Joseph Kakore ambaye ni mwakilishi wa wakazi wa Chome wanaoishi nje ya eneo hilo ambapo alisema umoja wao unaunga mkono jitihada za serikali kutatua kero hiyo kwani barabara hiyo ni muhimu kwa ustawi wa kata hiyo sanjari na kuchochea ukuaji wa kiuchumi.
Alisema barabara hiyo matengenezo ambayo yatahitajika ni pamoja na umwagaji wa vifusi vya moramu ujengaji wa mitaro na njia zakuchesha maji ambapo kazi zote zitaenda kwa ubia kati ya wakazi wanaoishi Chome na wale waliopo nje ya kata hiyo.
Napendael Mlay mtendaji kata ya Chome alisema kuna baadhi ya maeneo korofi likiwemo kituo cha afya Shengena hadi soko la kata na kuwa barabara hiyo ina mchango mkubwa hususan kufikisha huduma kwa wakazi wa kata hiyo.
Kwa mujibu wa mtendaji huyo barabara hiyo ambayo licha ya kufikakatika hifadhi ya taifa ya msitu wa Shengena vile vile ni kiungo muhimu kwa ustawi wa wakazi wa kata hiyo yenye wakazi zaidi ya 5000 ambapo kukamilika kwa barabara kutawezesha kurahisisha usafirishaji.
Meneja wa wakala wa barabara za mjini na vijijini (TARURA)wilaya ya Same mhandisi Felician Msangi alisema tayari ofisi yake itashirikiana na wadau hao kuhakikisha lengo lao linatimia na kuwa tayari upembuzi yakinifu ulishafanyika kwa ajili ya ujenzi katika kiwango cha changarawe.
Mwisho.