Wakazi wa DAR, tumelogwa na CCM? Kulikoni?

hiki kitu mkuu mshika chuma nimekuwa najiuliza kila siku! yani dar ambako wanajiita wameelimika ndowanatuangusha!
njoo arusha mkuu uwambie machalii ishu kuhusu ccm wanaweza kukupiga kabisa! juzi nilikuwa pale benki vijana wote wanaongea kuhusu kuipoteza ccm
lakini nyie bado mnakomaa nao nenda hata mwanza hadi watoto wa shule za msingi hawataki ccm! ila nyie ambao kuna vyuo vingi shule nyingi media nyingi bado mnakomaa na ccm tu! vijana wa dar wengi kazi kujisifu tu wakija mikoani! hawana lolote!

Unafikiri kujifagalia basi, sema tu tukitimba huko wenyewe tu wa mkoa huwa wanamwaga full fagio!!! totoz za arusha zenyewe; ndo kabisaa.....manake ukimwambia weekend njoo dar basi yupo tayari hata kutoroka kwa wazazi aje kuona bahari!!!!!
 
dar hamnazo,mgao wa umeme upo zaidi dar,makahaba na vibaka dar wapo dar umasikini mkubwa upo dar,wasomi,media na vyuo vipo dar lakini cha kushangaza mambumbumbu ndo wengi wasio elewa hata sera ni nini.poleni sana njooni mjifunze Arusha tunavyofanya.na kwa taarifa tu cdm haiko town tu but majimbo yote arusha na nakuhakikishia 2015 magamba hawapati hata jimbo moja chuga
 
Mkuu mimi nipo jimbo la kawe...sehemu niliyopo iko pouwa kiaina..maji yanatoka hayakatikikatiki ovyo...miundo mbinu kama barabara zinapanuliwa kwa kasi na mambo mengine.....

Lakini hata leo hii ukifanyika uchaguzi wa ubunge CCM haiambulii kitu hapa..sanasana kura zake zitapungua zaidi ya uchaguzi uliopita.....! Mimi nadhani sehemu zenye " Uswahili Uswahili mwingi" CCM huwa na mtaji mkubwa sana hata kama hao watu wa maeneo hayo hawapati huduma nzuri za jamii kama maji nk!

Huko kwenye uswahili uswahili ndo wapi mkuu? ndo matatizo yenu hayo; wasiokubaliana na nyinyi lazima mtawadhalilisha kwa kuwaita majina yasiyopendeza!!!! Ina maana huko kawe uswahili uswahili umetoka sasa? Mbona tangu zama hizo walikuwa wanachagua CCM?! Na lazima mkubali; yule mama wa CCM alikuwa dhaifu sana ukimlinganisha na Halima Mdee; hivyo kilichoisaidia CDM ni CCM kuweka mgombea dhaifu kama ilivyotokea kwa ubungo!
 
dar hamnazo,mgao wa umeme upo zaidi dar,makahaba na vibaka dar wapo dar umasikini mkubwa upo dar,wasomi,media na vyuo vipo dar lakini cha kushangaza mambumbumbu ndo wengi wasio elewa hata sera ni nini.poleni sana njooni mjifunze Arusha tunavyofanya.na kwa taarifa tu cdm haiko town tu but majimbo yote arusha na nakuhakikishia 2015 magamba hawapati hata jimbo moja chuga

hakuna cha kujifunza arusha; baadhi ya majimbo dar yalianza kuuchagua upinzani hata kabla ya hiyo arusha yako!!! na baadhi ya hayo majimbo yalipokea upinzani hata kabala ya majimbo mengi ambayo ndo yameamka hivi sasa.....na wao watakuja kushituka tu, unless magwanda muache siasa zenye na tija kwa wapenda shari.
 
Tatizo watu wa dar wanajifanya wako bize sana eti hawana muda na siasa ,mi wananiniboa sana.Lakini sehemu za Uswazi ndo zinaturudisha nyuma kwa hapa Dar maana ndo sehemu CCm wanaposhinda sana.

Hivi dar unaijua au unaisikia tu?! tatizo wengi wanajifanya wanaijua dar wakati hawaijui....wakifika kariakoo na posta mpya, ndio wanazani wameshaimaliza dar yote!!!! sasa kwa taarifa yako; heri huko uswazi wanaweza kudanganyika kuliko sehemu zingine ingawaje reference yenu kwa kila ki2 na kawe!!!! Hivi una habari 80% ya ubungo ni uswazi? tatizo mnazani uswazi ni temeke pekee; tunaoifahamu dar tunajua over 90% ya hili jiji ni uswazi including na hiyo kawe!
 
Mkuu wewe ni mtu kama wa kumi hivi kwenye post unaongea the same thing kuwa mtaji wa ccm hapa Dar ni watu wa uswahilini.
Lakini inakuwaje watu kama hao na maisha yao ni magumu sana wanaichagua ccm tena? tatizo ni nini hapo?

Usizani kila anaekaa uswahilini ana maisha magumu broda....wengine huko uswahilini ndiko kwenye makazi yao ya enzi na enzi na unakuta good lyf kuliko nyie mnaojifanya watoto wa kishua wakati hamna lolote!!!! baba zenu wakistaafu wote mnakuja huku huku......watu wanapiga deal za kila aina, halali na kafiri; hawasubirii pocket money; au mkwanja wa Grade D ya serikali.....na hata waki-make vipi bado hawahami huku!!!
 
Nimewasoma wengi na kubaini siku zote Chadema ni chama chenye malengo ya juu sana ya kutaka kuchukua madaraka kuiongoza tanzania bila kuwa na mipango na maandalizi mazuri katika mikakati yao.

Wengi wa wana Chadema ni mashabiki wanaoburuzwa pasi na kujua njia sahihi iwapi na kwa mtazamo huo wanafikiri kila mtu ni mtu wa kuburuzwa pasi na kutaka kujua.

Mimi ninavyojua watu wa Dar es salaam ni werevu sana na mara zote si watu wa kukurupuka pasi na kufanya udadisi wa kujua mazuri na mabaya.

Hakika Chadema ni chama kwa mtazamo wowote ule na mwenye akili timamu atagundua kina ajenda iliyofichika na ni wachache sana wanalijua hilo. Hata kwa mfano mdogo tu wa Dar. Sehemu walizoshinda katika wilaya za hapo Dar ni zile zenye bar nyingi nyingi ambazo ni Ubungo na Mbezi ambako kuna watu wengi wa kaskazini na hata wabunge wenyewe ni wa kutoka kaskazini.

Mimi nawashauri si vizuri kudandia chama pasi na kujua sera, malengo na mwerekeo wake bali kufuata mkumbo. nawapa pole sana kwa mawazo yenu mgando

Mkuu uliyosema ndio hasa yanayo-reflect dar!!! hapa huwezi kuwaburuza watu hovyo hovyo......kama vile Lema kajipeleka mahabusu halafu useme tuandamane na wakakusikiliza....yaani waache wakapige mzigo waende wakampiganie mtu mmoja!!!!! hapa hakuna kula kwa mjomba wala shangazi hivyo mtu hawezi kushabikia siasa ambazo hazina maslahi kwake!!! long time Rv. Mtikila alikuja na dizaini za wanazotumia hivi sasa CDM; watu wakaona anawazingua; wakamshiti!!
 
Mkuu umenena vema,ni kweli watu wa DAR ni wanafiki wenye kuendekeza njaa,lakini wanagubikwa na majigambo kwamba wao wako jijini na wanadhani ni wajanja sana.hapa DAR palitkiwa pawe ndo chacu ya mabadiliko na chachu ya ukombozi wa taifa hili,lakini mijitu inaendekeza njaa na kupiga hadthi kwenye kahawa tu.Nina ushahidi jinsi baadhi ya wananchi DAR wanavyoomba hela kwa wabunge.
Angalia ni majimbo mawili tu la Kawe na Ubungo lakini Kigamboni,Temeke,Ilala na Kinondoni yote yako chini ya ccm,najiuliza hapa DAR uchafu wote mkubwa unatokea hapa na wanauona lakini kipindi cha kura ni CCM.aibu sana.
kuna haja ya kufikiri upya
 
Haiwezekani hata siku moja watu wote wakawa na mawazo yanayofanana, wewe unaona CCM haifai lakini watu kibao wanaipenda.
 
mkuu nakuunga mkono kabisa kwamba sehemu zenye uswahili uswahili huwa ndo mtaji mkubwa wa ccm. angaalia mikoa ya tanga, kilwa, lindi temeke dar ambako uswahili umesheheni huko ndo wanachagua ccm. huwa nashindwa kufanya link kati ya uswahili na ccm. mikoa kama arusha, kilimanjaro, mwanza, mbeya.....nk mikoa hii hawajui uswahili ndo maana hawaitaki ccm. sasa sijui ccm inauswahili ndani yake sielewi!!

Mimi naamini kwamba magwanda wengi walidandia treni ya siasa za tz kwa mbele....kwa maana wengi hawaijui siasa na kilichopo kwao ni ushabiki usio na kichwa wala miguu unaodhihirisha hawajui wanachokiongea!!!! wao, upinzani ni CDM na wengine wote....sio wapinzani!!! mkuu tedo, wewe ndo unaonekana wala siasa yenyewe huijui mbali na ushabiki. Umeitaja Lindi na Kilwa; inaelekea wala hujui kwamba Mbunge wa Lindi Mjini anatokea CUF hali kadhalika na yule wa kilwa (if am not mistaken ni kilwa north). Au ulitaka hadi waichague CDM? Umeitaja TMK; kwa hapa Dar, Temeke ndio wilaya pekee ambayo kwa nyakati tofauti imewahi kuchukuliwa na wapinzani (jimbo la TMK-NCCR na jimbo la Kigamboni-CUF). Kwavile hawakuichagua CDM ?! Haya, nenda hata huko Arusha....au arusha ni arusha mjini na karatu peke yake?! hizo wilaya zingine nazo zina waswahili? mbali na arusha mjini na karatu, jimbo gani lingine lilichagua upinzani( hususani chadema) kwenye matokeo ya ubunge na urais?! Wanaofahamu siasa za tz; wanafahamu fika ni bifu kati ya Broda Masha na Diallo ndizo zilizochangia kuipa CDM ushindi na ndio maana hata kwenye matokeo ya urais, jimbo la nyamagana lilimchagua JK badala ya Slaa. The same applied pale Iringa; pamoja na ubunge kuipa CDM, bado JK aliongoza kwa mbali sana kwenye kura za urais. Hiyo pia ilitokea Maswa (east na west) pamoja bukombe ingawaje kila cku mtakimbilia kwenye hoja dhaifu zisizo na mashiko kwamba CCM waliiba kura!!!! je, huko nako kuna waswahili?! Hii tabia ya kudharau watu wa maeneo fulani ndio inayonifanya kuichukia CDM maradufu!!!Yaani kwa wanamgwanda; watu wa pwani hawajui lolote wakati hata weneyewe hamna tofauti yoyote na watu wa pwani!!! Ajabu, mkija dar mnataka mkaoneshwe meli!!!! wengine; wanataka wakaoneshwe bahari....lol!
 
Mkuu umenena vema,ni kweli watu wa DAR ni wanafiki wenye kuendekeza njaa,lakini wanagubikwa na majigambo kwamba wao wako jijini na wanadhani ni wajanja sana.hapa DAR palitkiwa pawe ndo chacu ya mabadiliko na chachu ya ukombozi wa taifa hili,lakini mijitu inaendekeza njaa na kupiga hadthi kwenye kahawa tu.Nina ushahidi jinsi baadhi ya wananchi DAR wanavyoomba hela kwa wabunge.
Angalia ni majimbo mawili tu la Kawe na Ubungo lakini Kigamboni,Temeke,Ilala na Kinondoni yote yako chini ya ccm,najiuliza hapa DAR uchafu wote mkubwa unatokea hapa na wanauona lakini kipindi cha kura ni CCM.aibu sana.
kuna haja ya kufikiri upya

Nitajie jimbo lingine lililochagua upinzani Arusha, tukiacha Arusha mjini na karatu!!!
 
Wakazi wa Ushwahilini dar wanashangaa kila duka la mchaga kuna bendera ya Chadema! Hilo bado lina wapa utata kujua Chadema ni chama cha aina gani! Hawakifahamu vizuri wanaona kama Chadema ni kikundi cha Watokao Kasikazini hasa akina Masawe,Mbowe,Mtei,Mushi,Lema.........ndesamburo!
 
Sometime huwanawaza kwanini wakazi wa Dar-es-salaam tusiwe chachu ya mabadiliko tunayoyataka? Maana utakuta tunapiga
keleleweeee lakini mwisho wa siku tunaichagua ccm! Hasa wakazi wa ILALA na KINONDONI' kwanini jamani? Tumelogwa? Hakika
haiingii akilini tunazidiwa na hata watu wa mikoani na vijijini?

Tena huko watu ndiyo wamelala na hawana mwamko au mtazamo kama sisi wakazi wa Dar....iweje watu wanaokaa nje kidogo tu ya jiji letu kama Kawe, Ubungo na hata Tabata Segerea hawataki kusikia kitu kinachoitwa CCM, sasa inakuwaje sisi wakazi tunaoishi majimbo ya katikati ya mji (Ilala na Kinondoni) tumeichagua CCM kwenye ucha guzi uliyopita?

Yaani nadiliki kusema hata kesho itokee uchaguzi wa ghafla Kinondoni au Ilala kama ilivyotokea Igunga basi utaona watu wanaichagua
ccm kwa kura za kishindo!. jamani tatizo ni nini? tumelogwa na ccm hii iliyotunyonya kwa miaka 50 na kutulaza na giza kila siku?

Hebu tazama wakazi wa Mwanza,Mbeya,Arusha,Shinyanga mjini,Iringa, Lindi mjini,Moshi mjini na vijijini,Singida vijijini,Mbozi nk huko
kote hawataki tena kusikia kitu kinachoitwa ccm. Sasa iweje sisi tunaojiita wajanja wa mjini (wabongo) kila uchaguzi tunaichagua ccm?

Makao makuu ya Chadema yako jimbo la kinondoni lakini cha ajabu ccm ndiyo inatawala hapo. Makao makuu ya NCCR yapo Ilala lakini
cha ajabu ccm ndiyo inatawala hapo. Makao makuu ya CUF yapo Buguruni lakini cha ajabu ccm ndiyo inatawala hapo. Jamani kulikoni?

Yaani makao makuu ya vyama vyetu yapo milangoni kwetu na tunaona kabisa hawa viongozi wetu wa vyama vya upinzani jinsi wana
vyopambana na kutuelimisha....lakini bado mwisho wa siku tunaichagua ccm. Jamani wabongo tuna nini kwenye vichwa vyetu?

Mageuzi ya kuindoa KANU yalianzia Nairobi, mageuzi ya kumuondoa Keneth Kaunda na sasa Rupia Banda yalianzia Lusaka, mageuzi ya
kumuondoa Ghabo wa Ivory coast yalianzia Abdijani, mageuzi ya kumuondoa rais wa Tunisia yalianzia Tunisia, mageuzi ya kumuondoa
Mubarak wa Egypti yalianzia Cairo na mageuzi ya kumuondoa Gaddafi wa Libya yalianzia Tripoli na baadae Beghazi.

So kuna waliotoka kwa sanduku la kura na kunawaliotoka kwa kufukuzwa na wananchi. So all in all mageuzi yalianzia miji mikuu na kusambaa miji midogo.

Lakini kwa hapa Tanzania mambo ni tofauti kabisa! watu wa mji mkuu wamelala usingizi mfano wa pono....yaani wanatushinda hata wakazi
wa mikoani na vijijini? Hebu angalia kilichotokea Igunga' CCM imetokea kwenye tundu la sindano, chupu chupu ing'oke!

Yaani ilikuwa tia maji tia maji mtu (ccm) isikate roho pale Igunga. Je wakazi wa jiji la Dar ukiondoa Kawe na Ubungo, tuna matatizo gani? tumelogwa na CCM? Au kunatatizo ambalo limejificha mie sijui? Kwa nini tusiwe kioo cha mageuzi kwa faida ya watanzania wote?.

- Nawasilisha

ccm inapata ushindi katika majimbo mengi ya Dar ambako show za taarab hufanyika sana kila wikiendi.
 
Wakazi wa Ushwahilini dar wanashangaa kila duka la mchaga kuna bendera ya Chadema! Hilo bado lina wapa utata kujua Chadema ni chama cha aina gani! Hawakifahamu vizuri wanaona kama Chadema ni kikundi cha Watokao Kasikazini hasa akina Masawe,Mbowe,Mtei,Mushi,Lema.........ndesamburo!

na sisi tunapatwa na mashaka sana na ccm kuona bendera yao na sanda za kuzikai waharabu zinafanana rangi.

ccm ni tawi la bakwata?
 
Kawe walugaluga kibao kule; wengi wao sio born town....ubungo, wengi ndio wale walio pale udsm ambao wengi wao ni kama walewale wa kawe.....walugaluga!
Mkuu, kuna post yako hapo juu umedai kuwa tabia ya kudharau watu wa maeneo mengine ndiyo imekufanya uichukie CDM! Natumaini hiki ulichoandika hapa siyo dharau kwa watu wa Kawe na Ubungo...
 
Mimi nafikiri dar ni sehemu nzuri ya kufanya demographic studies kujua ni kwanini inakuwa kama mtoa mada alivyoeleza. Research zaidi inatakiwa hapa, siyo kupigiana kelele zisizo na msingi.
 
me nafikiri uchaguzi ukifika tubadilishane haiwezekane dar, dodoma na morogoro hawa watu waendelee kutamba kila kukicha,tuwachukue wana arusha,wakurya na wasukuma wahamie huko inawezekana majotro yameboil bongo zenu na mmebaki na madafu huku mkizani ni vichwa vyenye akili,ccm na moro,ccm na dodoma,ccm na dar kha joto noma
 
Maeneo ambayo yamechukuliwa na CCM ni Ilala ambayo asilimia kubwa ya wakazi ni wahindi na waarabu na wasomali,pia Temeke kwa sehemu kubwa na Kinondoni.


Dar has mwaka jana walipiga kwa UDINI ZAIDI!! PIA WALIPGA KURA KWA KUFUATA WAKWETU!! MJUE VIJANA WENGI HASA WA VYUO WALIRUDISHWA NYUMBANI HADI UCHAGUZI ULIPOISHA, ILA DAWA KWA KWELI NI KUHAMASISHA VIJANA ZAIDI WAJIANDIKISHE THEN WAZEE NA AKINA MAMA WA MIPASHO WATAJIJU!!
 
Back
Top Bottom