Wakazi wa Buzwagi watawanywa kwa risasi, mabomu

Tuandamane

JF-Expert Member
Feb 2, 2008
1,220
52
Huu si ndio ule unaodaiwa kuwa ni wa mkapa??
Mkapa umefikia hatua hii???



WANANCHI waliohamishwa kupisha ujenzi wa Mgodi wa Buzwagi, wilayani Kahama jana

walitawanywa kwa risasi na mabomu ya kutoa machozi yaliyokuwa yakipigwa na Polisi kuzima jaribio lao la kutaka kurudi kwa nguvu katika makazi yao.


Jaribio hilo ambalo lilitangazwa juzi na wananchi hao lilianza alfajiri jana
baada ya wananchi hao kukusanyika kwa wingi wakiwa na mabango mbalimbali wakitaka
kurudi kwa nguvu kwenye makazi yao ambayo yapo ndani ya uzio wa Mgodi wa Buzwagi.


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Magesa Mulongo alisema kuwa kabla ya wananchi hao kutaka
kuvamia kurudi kwenye makazi yao walisambaza ujumbe kwenye simu za mikononi
ikiwemo simu yake unaodai kuwa umetoka kwa mtu mwenye nguvu ya kushawishi wananchi.


Mulongo alisema katika ujumbe huo, wananchi walidai kwa kuwa hawana uwezo wa kuinunua dola(serikali) ili iwatusaidie, watadai haki yao kwa kuweka rehani damu yao na kwamba ujumbe huo ulisambazwa kwa viongozi mbalimbali wa Serikali.


Alisema wananchi hao tayari wamelipwa fidia kwa asilimia 98, lakini baada ya kutumia vibaya fedha hizo, wamerudi kudai upya kwa maelezo kwamba walipunjwa wakati wa kuingia mkataba wa fidia na Kampuni ya Barrick.


Kufuatia tukio la jana, ambapo watu14 wanashikiliwa na polisi wilayani hapa, Mulongo alifahamisha kuwa wananchi hao walivamia mgodi huo kwa lengo la kuuhujumu.


Alisema licha ya Kamati ya Ulinzi na Usalama kuwazuia kuvamia eneo hilo, waligoma kuondoka kwa madai ya kwamba mpaka Mbunge wao James Lembeli afike mgodini hapo.


Wananchi hao waliokuwa wakipiga makelele wakidai kuwa wamiliki wa mgodi huo
ni makaburu na mafisadi, walidai kuwa mbuge wao aliwaagiza kuwa warudi katika maeneo yao ambayo tayari walikwishalipwa fedha na nyumba zao kubomolewa kupisha ujenzi wa mgodi huo.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya, kampuni ya Barrick ilikwishajenga nyumba 205 za fidia kwa wananchi walioondolewa, lakini nyumba 50 kati ya hizo bado zipo wazi baada ya wenyewe kugoma kuhamia, kwa sababu zisizoeleweka.


Mgodi huo wa Buzwagi umejumuisha vijiji vitatu, ambapo katika kijiji cha Mwendakulima tayari wote wameondoka na Mwime, familia tisa zimegoma huku zikiwa zimelipwa fidia na bado zimo ndani ya uzio wa kampuni hiyo.


Mulongo alisema kuwa katika Kijiji cha Chapulwa familia nne zimegoma kuondoka zikiwa zimelipwa fidia isipokuwa moja ambayo ilikataa kupokea.


Katika tukio la jana wananchi hao wapatao zaidi ya 500 walikuwa wamezingira lango kuu la kuingia mgodini hapo.


Licha Mkuu Wilaya kuwata waondoke wakafanye mkutano katika ofisi za Serikali za Vijiji vyao ili kupata mwafaka wa haki zao, wananchi hao waligoma.

Baada ya kuona vurugu zinakuwa kubwa polisi waliingilia katina walianza kurusha risasi na mabomu ya kutoa hewani ili kuwatawanya wananchi.Katika vurugu hizo watu 14walikamatwa, lakini vinara wa vurugu hizo walitimua mbio kukwepa mkono wa sheria na polisi wanaendelea kuwasaka.


Kuanzia jana mgodi huo upo chini ya ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi kutoka Shinyanga wakishiriana na wa wilayani Kahama.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=5633
 
Huu si ndio ule unaodaiwa kuwa ni wa mkapa??
Mkapa umefikia hatua hii???



WANANCHI waliohamishwa kupisha ujenzi wa Mgodi wa Buzwagi, wilayani Kahama jana

walitawanywa kwa risasi na mabomu ya kutoa machozi yaliyokuwa yakipigwa na Polisi kuzima jaribio lao la kutaka kurudi kwa nguvu katika makazi yao.


Jaribio hilo ambalo lilitangazwa juzi na wananchi hao lilianza alfajiri jana
baada ya wananchi hao kukusanyika kwa wingi wakiwa na mabango mbalimbali wakitaka
kurudi kwa nguvu kwenye makazi yao ambayo yapo ndani ya uzio wa Mgodi wa Buzwagi.


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Magesa Mulongo alisema kuwa kabla ya wananchi hao kutaka
kuvamia kurudi kwenye makazi yao walisambaza ujumbe kwenye simu za mikononi
ikiwemo simu yake unaodai kuwa umetoka kwa mtu mwenye nguvu ya kushawishi wananchi.


Mulongo alisema katika ujumbe huo, wananchi walidai kwa kuwa hawana uwezo wa kuinunua dola(serikali) ili iwatusaidie, watadai haki yao kwa kuweka rehani damu yao na kwamba ujumbe huo ulisambazwa kwa viongozi mbalimbali wa Serikali.


Alisema wananchi hao tayari wamelipwa fidia kwa asilimia 98, lakini baada ya kutumia vibaya fedha hizo, wamerudi kudai upya kwa maelezo kwamba walipunjwa wakati wa kuingia mkataba wa fidia na Kampuni ya Barrick.


Kufuatia tukio la jana, ambapo watu14 wanashikiliwa na polisi wilayani hapa, Mulongo alifahamisha kuwa wananchi hao walivamia mgodi huo kwa lengo la kuuhujumu.


Alisema licha ya Kamati ya Ulinzi na Usalama kuwazuia kuvamia eneo hilo, waligoma kuondoka kwa madai ya kwamba mpaka Mbunge wao James Lembeli afike mgodini hapo.


Wananchi hao waliokuwa wakipiga makelele wakidai kuwa wamiliki wa mgodi huo
ni makaburu na mafisadi, walidai kuwa mbuge wao aliwaagiza kuwa warudi katika maeneo yao ambayo tayari walikwishalipwa fedha na nyumba zao kubomolewa kupisha ujenzi wa mgodi huo.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya, kampuni ya Barrick ilikwishajenga nyumba 205 za fidia kwa wananchi walioondolewa, lakini nyumba 50 kati ya hizo bado zipo wazi baada ya wenyewe kugoma kuhamia, kwa sababu zisizoeleweka.


Mgodi huo wa Buzwagi umejumuisha vijiji vitatu, ambapo katika kijiji cha Mwendakulima tayari wote wameondoka na Mwime, familia tisa zimegoma huku zikiwa zimelipwa fidia na bado zimo ndani ya uzio wa kampuni hiyo.


Mulongo alisema kuwa katika Kijiji cha Chapulwa familia nne zimegoma kuondoka zikiwa zimelipwa fidia isipokuwa moja ambayo ilikataa kupokea.


Katika tukio la jana wananchi hao wapatao zaidi ya 500 walikuwa wamezingira lango kuu la kuingia mgodini hapo.


Licha Mkuu Wilaya kuwata waondoke wakafanye mkutano katika ofisi za Serikali za Vijiji vyao ili kupata mwafaka wa haki zao, wananchi hao waligoma.

Baada ya kuona vurugu zinakuwa kubwa polisi waliingilia katina walianza kurusha risasi na mabomu ya kutoa hewani ili kuwatawanya wananchi.Katika vurugu hizo watu 14walikamatwa, lakini vinara wa vurugu hizo walitimua mbio kukwepa mkono wa sheria na polisi wanaendelea kuwasaka.


Kuanzia jana mgodi huo upo chini ya ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi kutoka Shinyanga wakishiriana na wa wilayani Kahama.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=5633

Huu ni mgodi wa Kikwete kupitia kwa rafiki yake mkubwa Karamagi. Nadhani wale wanaoshauri wanafunzi wa chuoni kukaa kimya tu wakati haki zao zikipotea, wawashauri pia wakazi wa Buzwagi kukaa kimya na kukubali kunyanyaswa na polisi.
 
Huu ni mgodi wa Kikwete kupitia kwa rafiki yake mkubwa Karamagi. Nadhani wale wanaoshauri wanafunzi wa chuoni kukaa kimya tu wakati haki zao zikipotea, wawashauri pia wakazi wa Buzwagi kukaa kimya na kukubali kunyanyaswa na polisi.

Asante sana Mwafrika wa kike, hivi hawa wananchi wakiamua kutotishika na hiyo mitutu watu wangapi watapoteza maisha, naomba kuomba msaada kwa aliekuwepo eneo la tukio atuambie kama kweli kulikuwa na ulazima wa kutawanya watu kwa risasi??? basi hata kuiga kwenye TV jinsi askari wa nchi zilizo indelea wanavowazuia watu na ngao???
 
Asante sana Mwafrika wa kike, hivi hawa wananchi wakiamua kutotishika na hiyo mitutu watu wangapi watapoteza maisha, naomba kuomba msaada kwa aliekuwepo eneo la tukio atuambie kama kweli kulikuwa na ulazima wa kutawanya watu kwa risasi??? basi hata kuiga kwenye TV jinsi askari wa nchi zilizo indelea wanavowazuia watu na ngao???

Kuna mtu atawashauri hapa kuwa wafuate taratibu za kuomba vibali vya polisi na wasiulize maswali chochote kile kinachofanywa na serikali yao.

Ni suala la muda tu kabla wananchi hawajasema kuwa imetosha
 
Kuna mtu atawashauri hapa kuwa wafuate taratibu za kuomba vibali vya polisi na wasiulize maswali chochote kile kinachofanywa na serikali yao.

Ni suala la muda tu kabla wananchi hawajasema kuwa imetosha

Halafu huwezi kuamini kabisa hawa jamaa bado wamelala, hawaoni kabisa kama hii inakuja na imekaribia
 
CCM bwana .Yaani wazungu wanatucheka .Magesa analeta longo longo sawa na kule UD jamani fedha fedheha na haya yana mwisho .Laana hii inatambaa kwa kasi .Nchi ni yetu sote .
 
Hawa maafande wetu hawajajijua kuwa wamekuwa watumwa wa mafisadi.
Kwa nini wasijifunze kwa wenzao Ulaya?Ulaya watu hawatumii glucose nyingi kutawanya maandamano.Tena utaona wanatumia akili kuzuia ili wasisababishe maafa.
Haki za binadamu nadhani ni wakti muafaka wa kuwahubiri hawa maafande wetu watumie mbinu za vita vya majimaji.Yaani akili sana kuliko kutumia glucose nyingi.

Wale wananchi wamedhulumiwa na kila kukicha huyu mkuu wa Wilaya na mbunge wanaimba wimbo usiokoma masikioni mwao kuwa serikali inashughulukia matatizo yenu.

Basi tunakoelekea maafande wengi nao watavunjika miguu kama jana kule UDSM,Maana risasi zitakuwa za kawaida tu kwa wananchi na hawataziogopa.
 
Halafu huwezi kuamini kabisa hawa jamaa bado wamelala, hawaoni kabisa kama hii inakuja na imekaribia

Wao bado wanaamini kuwa watanzani watachukua tisheti na kofia za kijani toka kwa mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata Rostam Azizi wakati wa uchaguzi na ccm itashinda tena kwa 'Kishindo'
 
Hawa maafande wetu hawajajijua kuwa wamekuwa watumwa wa mafisadi.
Kwa nini wasijifunze kwa wenzao Ulaya?Ulaya watu hawatumii glucose nyingi kutawanya maandamano.Tena utaona wanatumia akili kuzuia ili wasisababishe maafa.
Haki za binadamu nadhani ni wakti muafaka wa kuwahubiri hawa maafande wetu watumie mbinu za vita vya majimaji.Yaani akili sana kuliko kutumia glucose nyingi.

Wale wananchi wamedhulumiwa na kila kukicha huyu mkuu wa Wilaya na mbunge wanaimba wimbo usiokoma masikioni mwao kuwa serikali inashughulukia matatizo yenu.

Basi tunakoelekea maafande wengi nao watavunjika miguu kama jana kule UDSM,Maana risasi zitakuwa za kawaida tu kwa wananchi na hawataziogopa.

Serikali ya ccm haijali wananchi wake. Kikwete yuko bize anazunguka dunia, Shein yuko bize na mikasi akifungua bucha za nyama. Pinda ndiyo hivyo tena anajichanganya bungeni kila siku.

Yaani hakuna kinachoendelea. Wanajua jeshi na polisi vipo na ndio maana wamefikia hatua ya kuingilia chaguzi za wanafunzi wa vyuo vikuu ili waweke mapandikizi yao kupitia kwa wasomi ambao pia ni mafisadi na madikiteta (wauaji?) kama Mkandara
 
Wao bado wanaamini kuwa watanzani watachukua tisheti na kofia za kijani toka kwa mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata Rostam Azizi wakati wa uchaguzi na ccm itashinda tena kwa 'Kishindo'

Yani hilo jina tu nikiliona moyo wangu unalipuka kwa hasira, iko siku..... na sema iko siku.....
 
Huu si ndio ule unaodaiwa kuwa ni wa mkapa??
Mkapa umefikia hatua hii???

.......wakafanye mkutano katika ofisi za Serikali za Vijiji vyao ili kupata mwafaka wa haki zao, wananchi hao waligoma


Kuanzia jana mgodi huo upo chini ya ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi kutoka Shinyanga wakishiriana na wa wilayani Kahama.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=5633

Mwafaka mwafaka mwafaka...mpaka lini? next karne?
mbona walichukua migodi hiyo kirahisi na sasa mwafaka...big up buzwagians
 
Ningewashauri waanze kuhangaika kumfata Balali aliko na kutuachia nchi yetu...... tumechoka kutukanwa na kuonwa wajinga

Sidhani kama wanaweza kufanya hili as longer as wana polisi na jeshi na huku wakiwa wamejazana bungeni na spika wao mzee wa vimada - Six
 
yaani inaaibisha. tanzania kila leo tunasifiwa kwa amani tuliyonayo, lakini wanachoshindwa kuelewa hao wanaosifu ni kuwa sio amani ya khiari, kuna uvunjaji wa haki za binaadamu wa kila aina ila mtanzania ni mnyonge sana kulinganisha na nguvu za dola kiasi cha kuwa anabaki kuwa na 'amani'
si tulisikia tume ya haki za binaadamu kutangazwa na kikwete kwa kicheko kingi kwenye picha alipozungukwa na akina mama warembo kila kona, sasa tuone hii tume itafanya kazi gani?
langu jicho
 
yaani inaaibisha. tanzania kila leo tunasifiwa kwa amani tuliyonayo, lakini wanachoshindwa kuelewa hao wanaosifu ni kuwa sio amani ya khiari, kuna uvunjaji wa haki za binaadamu wa kila aina ila mtanzania ni mnyonge sana kulinganisha na nguvu za dola kiasi cha kuwa anabaki kuwa na 'amani'
si tulisikia tume ya haki za binaadamu kutangazwa na kikwete kwa kicheko kingi kwenye picha alipozungukwa na akina mama warembo kila kona, sasa tuone hii tume itafanya kazi gani?
langu jicho

Kumbe uliona hili gaijin? kazi kweli hapa na kisha risasi zitatembea hadi wakome kwa kumzomea Kikwete alivyotembelea Shinyanga kipindi kile!
 
Ukisoma gazeti za leo, kuna listi za watuhumiwa wa kuongoza zali hili.

Funny enough "viongozi" hawa ni watu influencial katika jamii, Waalimu, Shekhe, Wachungaji, Viongozi wa vyama na kazwalika.

Hii ni ishara kamili ya umoja wa Wananchi kutetea haki zao.

Chakusikitisha, hawa jamaa wamepelekwa mahakamani, wakakataa makosa waliyotajiwa, wamewekwa Lupango!

Sasa twapotoza fedha za nini kushikilia waandamanaji Lupango?
 
Ukisoma gazeti za leo, kuna listi za watuhumiwa wa kuongoza zali hili.

Funny enough "viongozi" hawa ni watu influencial katika jamii, Waalimu, Shekhe, Wachungaji, Viongozi wa vyama na kazwalika.

Hii ni ishara kamili ya umoja wa Wananchi kutetea haki zao.

Chakusikitisha, hawa jamaa wamepelekwa mahakamani, wakakataa makosa waliyotajiwa, wamewekwa Lupango!

Sasa twapotoza fedha za nini kushikilia waandamanaji Lupango?

Hili ni swali gumu sana Rev,

Serikali inabidi ijifunze kuwa matumizi ya nguvu sio suluhisho la matatizo ya nchi yetu.
 
shame on you mkapa,damu za watanzania wote wanaokufa kwa matatizo ya umaskini zipo juu yako!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom