mpayukaji
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 940
- 349
Ingawa serikali yetu nayo inahusika kwenye upuuzi huu wa kuacha watu wajenge kwenye mkondo wa maji wakijua fikia kuwa siku ikifika ni mauti kwao, wakazi wa bonde la Msimbazi hawapaswi kutuumiza vichwa kwa yaliyowakuta kwani waliyataka wenyewe. Hivi unapojenga kwenye mkondo wa maji unategemea nini jamani? Tufikie mahali tuanze kutii sheria iwe ya nchi au maumbile. Leo barabara za Kariakoo zimefurika wamachinga. Hivi ikitokea gari likawagonga na kuua mamia tuanze tena kumlaumu Mungu? Kwanini tusifukuze wamachinga wa kihindi na kichina na kuwapa wetu sehemu za kufanyia biashara badala ya barabarani?