Wakazi wa bonde la Msimbazi hawapaswi kuonewa huruma

mpayukaji

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
940
349
Ingawa serikali yetu nayo inahusika kwenye upuuzi huu wa kuacha watu wajenge kwenye mkondo wa maji wakijua fikia kuwa siku ikifika ni mauti kwao, wakazi wa bonde la Msimbazi hawapaswi kutuumiza vichwa kwa yaliyowakuta kwani waliyataka wenyewe. Hivi unapojenga kwenye mkondo wa maji unategemea nini jamani? Tufikie mahali tuanze kutii sheria iwe ya nchi au maumbile. Leo barabara za Kariakoo zimefurika wamachinga. Hivi ikitokea gari likawagonga na kuua mamia tuanze tena kumlaumu Mungu? Kwanini tusifukuze wamachinga wa kihindi na kichina na kuwapa wetu sehemu za kufanyia biashara badala ya barabarani?
 
uko sahihi mkuu, siku zote nina huo mtazamo.wakati mwingine wanadiriki hata kulaumu serikali kwa mambo waliyoyafanya wenyewe kwa kupuuza tu kama hili la kujenga mabondeni. anyway!
 
Unaitwa mpayukaji eh? Hawa watu wanalipa kodi ya jengo. Wamewekewa umeme na wanalipia. Kwanini serikali isilaumiwe?

Serikali imefanya jitihada gani KUHAKIKISHA wanahama huko bondeni? Tusijisahaulishe Watanzania tuna hali ngumu ya maisha. Wewe unaona rahisi kumwambia ahame. Ila yeye anajiuliza akihama ataenda wapi? Na hapo kajibanabana kapata vyumba viwili?
 
Jamani mimi nimezaliwa nakua nakuta hawa watu wanaambiwa wahame, lakini kilasiku wanjenga wapya. Yale ya elininyo yaliwakuta, serikali ikatoa msaada wa kuwaokoa huku ikipiga kelele za kuwahamisha. Sijui hata nisemeje. Nakuja Gundua ni kazi kwelikweli kuongoza uma wa watu.
Je ww kama kiongozi utawafanyaaje hawa?
Je utachukua kodi za wemgine ukawajengee hawa ilihali wengi mikoani hawana huduma za jamii? Huo si utakuwa ufisadi?
 
wakazi wale pia ni tatizo, sawa serikali ina mapungufu yake
lkn kwa hili la bonde la Msimbazi, wananchi nao wanapaswa kulaumiwa.
Kwa wenye kumbukumbu nzuri, Mr.Makamba alilipigia kelele sn jambo hili
mpaka akaamua awahamishe kwa nguvu sjui kitu gani kilitokea hakukamilisha
plan yake. WALIONYWA mapema wakapuuzia, haya yote yasingewapata.
POLENI SANA NDUGU ZANGU ILA UKWELI UNAUMA, BEAR WITH ME
 
Ingawa serikali yetu nayo inahusika kwenye upuuzi huu wa kuacha watu wajenge kwenye mkondo wa maji wakijua fikia kuwa siku ikifika ni mauti kwao, wakazi wa bonde la Msimbazi hawapaswi kutuumiza vichwa kwa yaliyowakuta kwani waliyataka wenyewe. Hivi unapojenga kwenye mkondo wa maji unategemea nini jamani? Tufikie mahali tuanze kutii sheria iwe ya nchi au maumbile. Leo barabara za Kariakoo zimefurika wamachinga. Hivi ikitokea gari likawagonga na kuua mamia tuanze tena kumlaumu Mungu? Kwanini tusifukuze wamachinga wa kihindi na kichina na kuwapa wetu sehemu za kufanyia biashara badala ya barabarani?
aisee unafikiria zaidi kuliko hata viongozi wako,nakuunga mkono upo sawa
 
ukiwatoa huko kura zao utazikosa!
Hiyo mitaji yao!
Maeneo mazur ni tatizo wao kuyapata...majumba ya kupangisha wanapewa wenye uwezo japo zilijengwa kwa wenye hali duni. Sasa wenye hali duni ndio yanayowafika ya kuwafika. Muhim iwekwe sera kila mafuriko yakikaribia au kutokea wasaidiwa haraka na wapewe misaada muhim haraka pia.
 
Serikali haipimi viwanja vya kutosha na bei muafaka kwa wananchi wote kupata,akajenge wapi?
 
Ingawa serikali yetu nayo inahusika kwenye upuuzi huu wa kuacha watu wajenge kwenye mkondo wa maji wakijua fikia kuwa siku ikifika ni mauti kwao, wakazi wa bonde la Msimbazi hawapaswi kutuumiza vichwa kwa yaliyowakuta kwani waliyataka wenyewe. Hivi unapojenga kwenye mkondo wa maji unategemea nini jamani? Tufikie mahali tuanze kutii sheria iwe ya nchi au maumbile. Leo barabara za Kariakoo zimefurika wamachinga. Hivi ikitokea gari likawagonga na kuua mamia tuanze tena kumlaumu Mungu? Kwanini tusifukuze wamachinga wa kihindi na kichina na kuwapa wetu sehemu za kufanyia biashara badala ya barabarani?

Usishangae baada ya mafuriko wote wakarudi tena maeneo yale yale.
 
Siwasikitikii hao bali Ninasikitika kwa ajili ya watoto wao, pia nawasikitikia wale walioathirika ili hali hawakujenga mabondeni na ninsikitika kwa ajili ya miundombinu na usumbufu uliojitokeza na utakaofuata.
 
Ingawa serikali yetu nayo inahusika kwenye upuuzi huu wa kuacha watu wajenge kwenye mkondo wa maji wakijua fikia kuwa siku ikifika ni mauti kwao, wakazi wa bonde la Msimbazi hawapaswi kutuumiza vichwa kwa yaliyowakuta kwani waliyataka wenyewe. Hivi unapojenga kwenye mkondo wa maji unategemea nini jamani? Tufikie mahali tuanze kutii sheria iwe ya nchi au maumbile. Leo barabara za Kariakoo zimefurika wamachinga. Hivi ikitokea gari likawagonga na kuua mamia tuanze tena kumlaumu Mungu? Kwanini tusifukuze wamachinga wa kihindi na kichina na kuwapa wetu sehemu za kufanyia biashara badala ya barabarani?

Wachina na wahindi hayatuhusu na wala sio wa kuwalaumu hawa watu,, acha wafanye biashara zao... muhimu kutii sheria ipasavyo... issue hapa waliojenga kwenye mkondo wa maji wakijua fika kuna madhara yatatokea anytime, na wamachinga wanaokiuka sheria...
 
Serikali haiusiki kivipi wakati li yard la mwebdokasi limejaa maji hadi mabasi yamefunikwa? Nani kawapa uwanja wale? Pia wana umeme na huduma ya maji vyote hivyo ni serikali
Mtukufu mungu wa Tanzania a.k.a mzee wa 1.5 Trillion ndio alikuwa Waziri wa ujenzi wakati terminal hiyo inajengwa.
 
Mimi nafikili wapewe nyumba kulingana Na ukubwa wa familia,nimaskini sana wanaishi kama wako vitani usiku nvua ikianaza radio,TV,magodolo wanafunga juu ya kenchi.
 
Back
Top Bottom