Kuna taarifa za chini kwa chini kwamba wengi wa wakaazi wa Pwani wanaishi na kujenga kwenye aridhi ambayo tayari wawekezaji wameshakabidhiwa. Kwa mfano, bwana mmoja hivi karibuni alivamiwa katika eneo lake na wazungu ambao walikuwa wanafanya utafiti wa kiasiu cha mafuta katika eneo la mkoa wa Pwani.
Anasema walikuwa na vifaa vyao walivyosimika katika eneo la shamba lake. Aliamuwa kuwafuata na kuwauliza kulikoni wanaendesha shughuli zao katika eneo lake pasipo idhini yake? Ndipo walipomjibu kuwa wao ni wawekezaji. Na eneo lile lote wamekwiisha kabidhiwa tayari kwa uchimbaji mafuta. Na walichokuwa wanafanya ni kuona eneo la msambao wa mafuta aridhini. Walimwambia eneo lote lile liko juu ya mafuta kuelekea mwambao wa pwani na kwenye delta ya mto Rufiji.
Kama ndivyo ilivyo basi watanganyika tujue tumekwisha uzwa tena. Miradi yote ya wawekezaji katika eneo la madini,gesi asilia,makaa ya mawe, chuma nk. haina manufaa yoyote isipokuwa kwa viongozi wa CCM na serikali yao (kumbuka msemo, CCM ina wenyewe) huku viogozi hao wakigawana utajiri wa raslimali za watanganyika baina ya wazungu, wahindi,waarabu, wachina na watoto wao,rafiki zao,jamaa zao.
Huu ni wakati wa kukataa KABISA UZANDIKI HUU! Katiba mpya ipunguze madaraka ya rais,aridhi imilikiwe na wananchi,badala ya kupangishwa. Muungano ni mlango mwingine wa ufisadi na uzandiki huu.WATANGANYIKA TUAMKE, KUMEKUCHA,MAPAMBAZUKO YAMEISHA PITA!
Anasema walikuwa na vifaa vyao walivyosimika katika eneo la shamba lake. Aliamuwa kuwafuata na kuwauliza kulikoni wanaendesha shughuli zao katika eneo lake pasipo idhini yake? Ndipo walipomjibu kuwa wao ni wawekezaji. Na eneo lile lote wamekwiisha kabidhiwa tayari kwa uchimbaji mafuta. Na walichokuwa wanafanya ni kuona eneo la msambao wa mafuta aridhini. Walimwambia eneo lote lile liko juu ya mafuta kuelekea mwambao wa pwani na kwenye delta ya mto Rufiji.
Kama ndivyo ilivyo basi watanganyika tujue tumekwisha uzwa tena. Miradi yote ya wawekezaji katika eneo la madini,gesi asilia,makaa ya mawe, chuma nk. haina manufaa yoyote isipokuwa kwa viongozi wa CCM na serikali yao (kumbuka msemo, CCM ina wenyewe) huku viogozi hao wakigawana utajiri wa raslimali za watanganyika baina ya wazungu, wahindi,waarabu, wachina na watoto wao,rafiki zao,jamaa zao.
Huu ni wakati wa kukataa KABISA UZANDIKI HUU! Katiba mpya ipunguze madaraka ya rais,aridhi imilikiwe na wananchi,badala ya kupangishwa. Muungano ni mlango mwingine wa ufisadi na uzandiki huu.WATANGANYIKA TUAMKE, KUMEKUCHA,MAPAMBAZUKO YAMEISHA PITA!