Wakazi Keko Mwanga wapanga kuandamana hadi kwa RC wa Dar es Salaam kuhusu mfereji wa maji unaojengwa na Wachina, Injinia wa Temeke alalamikiwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,600
217,997
Taarifa kutoka kwa wakazi hao zinasema kwamba kabla ya mfereji huo usiotumika, makazi yao hayakuwahi kukumbwa na mafuriko makubwa kama yale yaliyotokea hivi Majuzi baada ya mvua kubwa kunyesha, hasa baada ya kuzibwa kwa mifereji ya awali huku mfereji huo mpya ukifungwa bila kutumika licha ya kwamba umejengwa, Maandamano hayo yamepangwa kufanyika kesho.

Baada ya tuhuma hizo tukaamua kufuatilia ambapo tumejiridhisha kwamba ni kweli njia ya maji kuelekea baharini Eneo la BP au PUMA imechukuliwa na mfereji huo uliozibwa ambao haufahamiki utakamilika lini, huku msimu wa mvua ukikaribia, juhudi za kumtafuta injinia wa Manispaa ya Temeke zinaendelea huku kukiwa na tuhuma nzito dhidi yake ya kuwasaidia wakandarasi wa kichina kukwepa ramani ya awali ya mradi huo iliyokuwa kwenye Barabara ya kwenda Uwanja wa Taifa kutokea Tameko ili kuepuka gharama na kuanza kuuchepusha kwenye makazi ya watu, jambo linalopingwa na wananchi.

Taarifa zote za mradi huu ambao umeleta usumbufu mkubwa kwa wananchi ikiwemo kubomoka kwa nyumba zao mvua zinaponyesha pamoja na kusababisha vifo kadhaa vya watu huku taarifa zikifichwa tutazileta hapahapa JF, sasa tumeamua kulivalia njuga jambo ili kuepusha mafuriko ya kijinga.

Itaendelea...
 
Taarifa kutoka kwa wakazi hao zinasema kwamba kabla ya mfereji huo usiotumika, makazi yao hayakuwahi kukumbwa na mafuriko makubwa kama yale yaliyotokea hivi Majuzi baada ya mvua kubwa kunyesha, hasa baada ya kuzibwa kwa mifereji ya awali huku mfereji huo mpya ukifungwa bila kutumika licha ya kwamba umejengwa, Maandamano hayo yamepangwa kufanyika kesho.

Baada ya tuhuma hizo tukaamua kufuatilia ambapo tumejiridhisha kwamba ni kweli njia ya maji kuelekea baharini Eneo la BP au PUMA imechukuliwa na mfereji huo uliozibwa ambao haufahamiki utakamilika lini, huku msimu wa mvua ukikaribia, juhudi za kumtafuta injinia wa Manispaa ya Temeke zinaendelea huku kukiwa na tuhuma nzito dhidi yake ya kuwasaidia wakandarasi wa kichina kukwepa ramani ya awali ya mradi huo iliyokuwa kwenye Barabara ya kwenda Uwanja wa Taifa kutokea Tameko ili kuepuka gharama na kuanza kuuchepusha kwenye makazi ya watu, jambo linalopingwa na wananchi.

Taarifa zote za mradi huu ambao umeleta usumbufu mkubwa kwa wananchi ikiwemo kubomoka kwa nyumba zao mvua zinaponyesha pamoja na kusababisha vifo kadhaa vya watu huku taarifa zikifichwa tutazileta hapahapa JF, sasa tumeamua kulivalia njuga jambo ili kuepusha mafuriko ya kijinga.

Itaendelea...
Wasubiri uchaguzi upite,mshindi aapishwe na walioshindwa wakubali matokeo hapo hata wakiandamana nafuu itakuepo. Wakiandamana kabla tunawajumuisha na watu wenyenia ya kuvuruga uchaguzi.
 
Wasubiri uchaguzi upite,mshindi aapishwe na walioshindwa wakubali matokeo hapo hata wakiandamana nafuu itakuepo. Wakiandamana kabla tunawajumuisha na watu wenyenia ya kuvuruga uchaguzi.
Ohooooo !!
 
Back
Top Bottom