Wakati wasanii wetu wanafanya show na wanasiasa, Davido apiga shows na 50 Cent na Chris Brown

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,104
7,857
Mimi ni mtu ninayeamini kuwa changamoto kubwa katika sanaa ya Bongo inaanzia kwa wasanii wenyewe ingawa serikali inachangia sana kwa kiwango kikubwa kuwadumaza, na hii sidhani kama wanasiasa wnafanya kwa bahati mbaya.

Hivi karibuni niliwahi kuleta uzi hapa nikimkosoa Diamond kwa mambo kadhaa, kuna watu wakanishambulia sana kuwa nina chuki binafsi. Ukweli mimi sipo kwenye 'team' yoyote, I just like good entertainment haijalishi ni nani. Ningependa niwaone Diamond, Ali Kiba, Darassa, Harmonize na wengine wanapiga shows MSG na Las Vegas. Ule uzi niliuleta ukiwa nusu ni utani lakini kuna mawazo ya msingi niliyotaka kuwayasilisha. Watu waliuchukulia too serious!

Kuna changamoto kubwa sana katika kushindana na wasanii wa Nigeria katika muziki. Ukiacha suala la uwekezaji mkubwa waliyofanya kwenye industry yao tofauti na sisi, lakini kuna suala la ukaribu kufika Marekani kutoka Nigeria (kwa maana hiyo gharama ziko chini). Wakati sisi tunakwenda Afrika Kusini kurekodi audio na video, wao wanakwenda Marekani.

Pia Sina uhakika mfumo wao wa usambazaji uko vizuri kiasi gani ila ninachojua kuna Wanigeria wengi kwenye vyombo mbalimbali vya entertainment na wanasaidiana kweli kuanzia fursa za shows zinapojitokeza, kutengeneza programs wanazoziita za muziki wa Afrika lakini kiukweli wanapiga za kwao tu, nk. Hili nakumbuka kumsikia Vanessa Mdee akiliongelea. Kuna kazi kubwa ya kufanya kwenye hili suala.

Pia binafsi sidhani kama ni mbinu nzuri kwa wasanii wetu wakubwa kujaribu kufanya kazi na wasanii wakubwa wa Marekani kama Rick Ross, Omarion. Ukiacha faida za kinyumbani za kufanya hivyo (kupata deals za Vodacom, Tigo na ASAS Dairies), sioni hili likiwasaidia kimauzo huko nje wala kuongeza kujulikana kwao. Tusiwaige kina Davido na Wiz Kid, wao wana mikakati yao, na sisi inabidi tuweke ya kwetu.

Kwa maoni yangu, wasanii wetu wangejikita kufanya kazi na underground artists wa nje (kuna ambao wana fans kibao online ila hawasikiki kwenye mainstream media na wanafanya shows nyingi). Nakumbuka Sugu aliwahi kufanya collabo na wasanii fulani underground wa Marekani. Hii kitu inabidi iwe endelevu ili iwe na matokeo chanya. Mdogo mdogo tukifanya hivyo, kwanza itawajengea wasanii wetu ufahamu fulani, network, ubunifu na asikwambie mtu hot tracks zinatengenezwa kwenye studio za kitaa. Wasanii wengi wakubwa wananunua na kuiba nyimbo na styles zilizotengenezwa na wasanii wa underground. Huko ndiyo kwenye ubunifu hasa na watu wenye njaa.

Kingine kujikita kutafuta fursa za kufanya shows kwenye festivals mbalimbali duniani. Hii ni fursa kubwa sana ambayo wasanii wangekaa chini wakaifanyia kazi. Inabidi kutengeneza Swahili Movement itakayoanzia chini chini isambae taratibu halafu ifike siku sisi ndiyo tuwe watu waku set trends kwenye muziki wa Afrika badala ya kuwa watu wa kuiga tu.

La mwisho, hakuna haja ya kuiga umarekani si katika uvaaji wala uimbaji. Inabidi tuwe na utambulisho wetu. Sishauri turudi kuvaa majani na kucheza miguu peku kama kina Mrisho Mpoto, ila tunaweza kuja na vitu fulani tofauti vitakavyotutofautisha na wanigeria na tamaduni zingine. Tuna makabila zaidi ya 100, kuna madini mengi sana ya sauti, beats, rhythm, choruses, uchezaji hadi fashion ambayo bado kabisa hatujayachimbua.

Tujadiliane kwa ustaarabu, leo sijamshambulia mtu.
 
Hivi kuna watu bado wanamsikiliza 50 cent?

Binafsi simsikilizi ila 50 bado ni msanii mkubwa sana. Usishangae siku kumuona Davido kwenye TV show ya Power. Unajua kuna wasanii wangapi DUNIANI wanaweza kuwauza mama zao kupata nafasi ya kuperform na 50 Cent?

Chini hapa ni show ya 50 Cent ambayo Davido alitokea.

 
Binafsi simsikilizi ila 50 bado ni msanii mkubwa sana. Usishangae siku kumuona Davido kwenye TV show ya Power. Unajua kuna wasanii wangapi DUNIANI wanaweza kuwauza mama zao kupata nafasi ya kuperform na 50 Cent?

Chini hapa ni show ya 50 Cent ambayo Davido alitokea.

Duh, yaani kushiriki tu kwenye ile launch ndo basi tena kuna uwezekano wa kushiriki kwenye Power?! Si afadhali ungesema Empire kutokana na mahudhui yake!! Tena usisahau, Season 6 ndo mwisho wa Power though 50C anaonekana kuendelea kuitamani!

Ndo vile tu Empire na yenyewe season ijayo inaweza kuwa ndiyo ya mwisho lakini nilikuwa naona kabisa (na bado naendelea kuona) msanii wa Nigeria akipata scenes mbili tatu.
 
Wewe unafanya kazi gani? Umefanikiwa kwa kiasi gani ukilinganisha na wenzio wanaofanya kazi kama hiyo?

Tutoe maboliti machoni kwetu kwanza.

Wewe baki hivyo hivyo, badala ya kuzingatia ushauri unaotolewa unaangalia anayeutoa ni nani. Embu sikiliza kwanza muziki wa Davido unavyosound bomba kwenye speakers hizo za MSG!!
 
Duh, yaani kushiriki tu kwenye ile launch ndo basi tena kuna uwezekano wa kushiriki kwenye Power?! Si afadhali ungesema Empire kutokana na mahudhui yake!! Tena usisahau, Season 6 ndo mwisho wa Power though 50C anaonekana kuendelea kuitamani!

Ndo vile tu Empire na yenyewe season ijayo inaweza kuwa ndiyo ya mwisho lakini nilikuwa naona kabisa (na bado naendelea kuona) msanii wa Nigeria akipata scenes mbili tatu.

Ni suala la network. Fursa ile ukiitumia vizuri inafungua milango mingine, ndiyo point niliyotaka kusema. Una maana gani maudhui yake? Kwani Kendrick Lamar alitokea kwenye Power kama rapper?
 
Wewe baki hivyo hivyo, badala ya kuzingatia ushauri unaotolewa unaangalia anayeutoa ni nani. Embu sikiliza kwanza muziki wa Davido unavyosound bomba kwenye speakers hizo za MSG!!

Kama wewe binafsi huoni cha kujifunza kutoka kwa Davido kwenye career yako huna tofauti na hao wasanii unaowashauri.

Tena wewe utakuwa ni fala zaidi, unawaponda wenzio kwa kitu ambacho wewe pia unakihitaji.
 
Kama wewe binafsi huoni cha kujifunza kutoka kwa Davido kwenye career yako huna tofauti na hao wasanii unaowashauri.

Tena wewe utakuwa ni fala zaidi, unawaponda wenzio kwa kitu ambacho wewe pia unakihitaji.

Wapi nimesema sina cha kujifunza kutoka kwa Davido? Matusi wote tunayajua, usiniharibie uzi.

joseph1989 karibu mkuu, hahaha!!
 
Ni suala la network. Fursa ile ukiitumia vizuri inafungua milango mingine, ndiyo point niliyotaka kusema. Una maana gani maudhui yake? Kwani Kendrick Lamar alitokea kwenye Power kama rapper?
Sasa mchukue Kendrick Lamar mwanamuziki aliyetokea kwenye series ya Power kisha linganisha na idadi ya wanamuziki waliotokea kwenye Empire... it's all about the game of chance!

Probability ya mwanamuziki kushiriki kwenye Series ya Empire ni kubwa maradufu compared na kushiriki Power hususani kwa msanii kama Davido or anyone from Nigeria!

Kwenye Empire, wanaweza sana kufanya hivyo kwa ajili ya kuleta ladha tofauti.
 
Sasa mchukue Kendrick Lamar mwanamuziki aliyetokea kwenye series ya Power kisha linganisha na idadi ya wanamuziki waliotokea kwenye Empire... it's all about the game of chance!

Probability ya mwanamuziki kushiriki kwenye Series ya Empire ni kubwa maradufu compared na kushiriki Power hususani kwa msanii kama Davido or anyone from Nigeria!

Kwenye Empire, wanaweza sana kufanya hivyo kwa ajili ya kuleta ladha tofauti.

Wewe unaangalia wapi ni rahisi kutokea mimi naangalia wapi ni bomba zaidi kutokea. Ndiyo maana wengi wanatamani kutokea kwenye Power ila hawapati hiyo nafasi.

Power imeiacha mbali sana Empire, muulize mtu yoyote. Sijaangalia Empire toka season ya kwanza.
 
Diamond Jana alifanya show pale taifa baada ya waziri wa Mh Mwakiembe kumuomba aiwaikilishe nchi je,ulitaka akatae?

Wanasiasa wamewapumbaza. Mnaona hamuwezi kuishi bila wao.

Ukiwa unastruggle kutoka hawana habari na wewe, sasa sana ndiyo wanakuongezea vikwazo. Ukishatoka ndiyo wanakushobokea.

I don't respect that.
 
Mimi ni mtu ninayeamini kuwa changamoto kubwa katika sanaa ya Bongo inaanzia kwa wasanii wenyewe ingawa serikali inachangia sana kwa kiwango kikubwa kuwadumaza, na hii sidhani kama wanasiasa wnafanya kwa bahati mbaya.

Hivi karibuni niliwahi kuleta uzi hapa nikimkosoa Diamond kwa mambo kadhaa, kuna watu wakanishambulia sana kuwa nina chuki binafsi. Ukweli mimi sipo kwenye 'team' yoyote, I just like good entertainment haijalishi ni nani. Ningependa niwaone Diamond, Ali Kiba, Darassa, Harmonize na wengine wanapiga shows MSG na Las Vegas. Ule uzi niliuleta ukiwa nusu ni utani lakini kuna mawazo ya msingi niliyotaka kuwayasilisha. Watu waliuchukulia too serious!

Kuna changamoto kubwa sana katika kushindana na wasanii wa Nigeria katika muziki. Ukiacha suala la uwekezaji mkubwa waliyofanya kwenye industry yao tofauti na sisi, lakini kuna suala la ukaribu kufika Marekani kutoka Nigeria (kwa maana hiyo gharama ziko chini). Wakati sisi tunakwenda Afrika Kusini kurekodi audio na video, wao wanakwenda Marekani.

Pia Sina uhakika mfumo wao wa usambazaji uko vizuri kiasi gani ila ninachojua kuna Wanigeria wengi kwenye vyombo mbalimbali vya entertainment na wanasaidiana kweli kuanzia fursa za shows zinapojitokeza, kutengeneza programs wanazoziita za muziki wa Afrika lakini kiukweli wanapiga za kwao tu, nk. Hili nakumbuka kumsikia Vanessa Mdee akiliongelea. Kuna kazi kubwa ya kufanya kwenye hili suala.

Pia binafsi sidhani kama ni mbinu nzuri kwa wasanii wetu wakubwa kujaribu kufanya kazi na wasanii wakubwa wa Marekani kama Rick Ross, Omarion. Ukiacha faida za kinyumbani za kufanya hivyo (kupata deals za Vodacom, Tigo na ASAS Dairies), sioni hili likiwasaidia kimauzo huko nje wala kuongeza kujulikana kwao. Tusiwaige kina Davido na Wiz Kid, wao wana mikakati yao, na sisi inabidi tuweke ya kwetu.

Kwa maoni yangu, wasanii wetu wangejikita kufanya kazi na underground artists wa nje (kuna ambao wana fans kibao online ila hawasikiki kwenye mainstream media na wanafanya shows nyingi). Nakumbuka Sugu aliwahi kufanya collabo na wasanii fulani underground wa Marekani. Hii kitu inabidi iwe endelevu ili iwe na matokeo chanya. Mdogo mdogo tukifanya hivyo, kwanza itawajengea wasanii wetu ufahamu fulani, network, ubunifu na asikwambie mtu hot tracks zinatengenezwa kwenye studio za kitaa. Wasanii wengi wakubwa wananunua na kuiba nyimbo na styles zilizotengenezwa na wasanii wa underground. Huko ndiyo kwenye ubunifu hasa na watu wenye njaa.

Kingine kujikita kutafuta fursa za kufanya shows kwenye festivals mbalimbali duniani. Hii ni fursa kubwa sana ambayo wasanii wangekaa chini wakaifanyia kazi. Inabidi kutengeneza Swahili Movement itakayoanzia chini chini isambae taratibu halafu ifike siku sisi ndiyo tuwe watu waku set trends kwenye muziki wa Afrika badala ya kuwa watu wa kuiga tu.

La mwisho, hakuna haja ya kuiga umarekani si katika uvaaji wala uimbaji. Inabidi tuwe na utambulisho wetu. Sishauri turudi kuvaa majani na kucheza miguu peku kama kina Mrisho Mpoto, ila tunaweza kuja na vitu fulani tofauti vitakavyotutofautisha na wanigeria na tamaduni zingine. Tuna makabila zaidi ya 100, kuna madini mengi sana ya sauti, beats, rhythm, choruses, uchezaji hadi fashion ambayo bado kabisa hatujayachimbua.

Tujadiliane kwa ustaarabu, leo sijamshambulia mtu.
Sawa baba yake na davido tumekusikia
 
Hijajibu swali Narudia tena Diamond aliombwa kupaform kwenye lile tamasha na waziri wa habari Mh Mwakiembe ili aliwakilishe Taifa je,ulitaka akatae?
Wanasiasa wamewapumbaza. Mnaona hamuwezi kuishi bila wao.

Ukiwa unastruggle kutoka hawana habari na wewe, sasa sana ndiyo wanakuongezea vikwazo. Ukishatoka ndiyo wanakushobokea.

I don't respect that.
 
Wewe unaangalia wapi ni rahisi kutokea mimi naangalia wapi ni bomba zaidi kutokea. Ndiyo maana wengi wanatamani kutokea kwenye Power ila hawapati hiyo nafasi.

Power imeiacha mbali sana Empire, muulize mtu yoyote. Sijaangalia Empire toka season ya kwanza.
Kwamba wengi wanatamani kutokea kwenye Power, hao wengi ni akina nani?! Unaweza kuwataja hapa? Au kwavile 50Cent anapiga sana kelele Instagram huku akithubutu kudai hata GoT si lolote mbele ya Power ndo maana unaamini Power ni G.O.A.T Series?

Si ni huyo huyo 50 ambae alitoka povu baada ya Howard Terrence (Lucious) wa Empire kumshinda Omar Hardwick (Ghost) wa Power kwenye tuzo za BET?!

Waigizaji wa Empire wamekuwa nominated kwenye Emmy Awards, People's Choice Awards, Golden Global hadi Grammy kwa kupitia Soundtrack!

Ni wasanii gani kutoka Power waliokuwa nominated kwenye hizo awards?

Sio kwamba naiponda Power, hell no kwa sababu na yenyewe ni my favorite show lakini unachekesha unapodai "watu wanaangalia wapi ni bomba" as if hiyo Empire ni series ya kitoto!!

Halafu nimekuambia Power ndo ishafika ukingoni... sasa inatarajia vipi mtu atoke kupitia Power ambayo hii ni season yake ya mwisho?! Labda sema B.M.F lakini sio Power tena!
 
Kwamba wengi wanatamani kutokea kwenye Power, hao wengi ni akina nani?! Unaweza kuwataja hapa? Au kwavile 50Cent anapiga sana kelele Instagram huku akithubutu kudai hata GoT si lolote mbele ya Power ndo maana unaamini Power ni G.O.A.T Series?

Si ni huyo huyo 50 ambae alitoka povu baada ya Howard Terrence (Lucious) wa Empire kumshinda Omar Hardwick (Ghost) wa Power kwenye tuzo za BET?!

Waigizaji wa Empire wamekuwa nominated kwenye Emmy Awards, People's Choice Awards, Golden Global hadi Grammy kwa kupitia Soundtrack!

Ni wasanii gani kutoka Power waliokuwa nominated kwenye hizo awards?

Sio kwamba naiponda Power, hell no kwa sababu na yenyewe ni my favorite show lakini unachekesha unapodai "watu wanaangalia wapi ni bomba" as if hiyo Empire ni series ya kitoto!!

Halafu nimekuambia Power ndo ishafika ukingoni... sasa inatarajia vipi mtu atoke kupitia Power ambayo hii ni season yake ya mwisho?! Labda sema B.M.F lakini sio Power tena!

Dah kuna watu mnapenda ubishi! Yaani umekomalia jambo nililolisema in passing (na ambalo niko sahihi) umesahau kabisa mada niliyoleta.

Ndiyo maana mnafeli kwenye mitihani halafu mnadai elimu ngumu. Yaani katika yote niliyosema, hili ndiyo umeona uliandikie insha?
 
Back
Top Bottom